Wakenya wanaoishi nje ya nchi hutuma trilioni 10 nchini kwao, Watanzania hutuma bilioni 700, tukifata ushauri wa Lowassa kuhusu elimu, tutafikia Kenya

Hapo Hakuna uhusiano na shule. Wakenya wengi wapo nje ya nchi Yao kulinganisha na watanzania.
Yaan mt
Mtoa, mada ulichoongea sio kweli. Hakuna uhusiano wowote kuwa, nje ya nchi na kuwa, msomi. Unaweza kuwa, nje, ya nchi unabeba maboksi, unapaka rangi za maghorofa, unaosha wabibi na wababu.Je huo ni usomi??? Mtoa mada nawe pia sio msomi sasa. Unaongea vitu irrelevant kabisa.
 
Ni suala la tamaduni binafsi na uamuzi wa mtu husika, na kijumla watanzania hatupendani, hatuaminiani na sababu ni kutapeliana na kudhulumiana

Mtu yupo radhi aende nje hata miaka kumi na zaidi asitume hata senti na aweke akiba npaka atakaporejea na akifanya hivyo basi ni vinchenchi kadhaa tu, sababu wengi yameshawakuta unatuma hela ujengewe unakuta malonyalonya unataka hiki hukuti kabisa

Ila tungekuwa walau tuna ubinadamu mbona zingetumwa nyingi tu ila ndio hivyo tena
 
akili za kimatako hizi, India ndio inaongoza kupokea pesa nyingi za Diaspora wao, India ndio inaongoza Duniani, Vipi kuna Vita India? Hizi ndio akili wakina Makona wanapeda, akili za mavi
 
Mungu saidia nchi ina wajinga wa kutisha sana
 
Ishu sio elimu,ishu ni ubinafsi kwani ujui wabongo tunavyobaniana kutoka nje.
Tupo radhi kuwabania watu wasiende nje kufanya kazi.
Mfano madada wa KAZI wangapi wamebadilisha maisha ya kwao kwa kufanya kazi TU nje.
 
Tanzania hii hapana kabisa.
Yaani wewe pambana tu ili utoke kivyako vyako. Chuki, ubinafsi na roho mbaya vimeanzia kwenye familia, jamii, mpaka taifa.

Serikali ya Tanzania haitaki kabisa watu wake wasafiri nje (nenda kaumbe passport ndio utajua mtiti wake), na watu wakisafiri nje serikali inawaona kama wasaliti kwa nchi yao, inachukia kuona mtanzania aliyeko nje akileta pesa au mali hapa Tanzania (yaani unaonekana kama unaleta magendo), mtu akipata uraia wa nje na uraia wa tanzania ina mnyang'anya papo hapo.

Serikali ya CCM inajivunia mnoo kuwa na wananchi wanyonge, washamba, wajinga, waoga na maskini, hivyo Diaspora (watu wanaonekana kama werevu, jasiri, wenye kipato cha uhakika) wanaonekana kama kundi hatari kwa maslahi ya taifa.
 
Tanzania imeshika Mkia pamoja na Burundi Kwa kupokea pesa(remittance ) Kiduchu sana zinazotokana na Wananchi wake waliko Nje ya Nchi (Diaspora).

Kwa wale msiofahamu remittance zinahesabika ni Kati ya vyanzo vya Fedha za kigeni kama Dola nk Kwa Nchi.Pia ni vyanzo vikuu vya kukuza uchumi Kwa njia ya uwekezaji na Utalii.

Sasa Kwa Tanzania kuwa ya Mwisho kiukweli inafedhehesha.Licha ya kuachana na ujamaa Kwa zaidi ya miaka 25 Sasa ila athari zake Bado ni kubwa sana kwenye fikra na mtizamo wa watu.

Ujamaa umesababisha Watanzania Kila kitu ni kulaumu na kulalamikia Serikali hata pale inapofungua fursa Bado watu wanataka wasukumwe au waoneshwe.

Aidha Bado taasisi za kiserikali zimekaa kiudhibiti na kukomoana badala ya kuwa wawezeshaji.Kupata passport Kwa Tanzania ni anasa maana Kuna vikwazo na urasimu isivyo kawaida.

Ukiangalia Nchi za wenzetu huko wanapigana Kufa kupona hawaogopi kifo kuhama na kwenda Nje ya Nchi ambako wanaamini wanaweza pata maisha Bora zaidi mfano Wasomali,Waethiopia,Wakenya , Nigerians nk ila huwezi sikia Mtanzania amekamatwa Nje ya Nchi kama mhamiaji haramu sana sana utawakita kwenye ugaidi usio na faidia kwao ,Taifa na familia.

Watanzania tufunguke maana fursa za Maisha zinapatikana mahala popote.Huwa naona matangazo ya scholarships kibao ila Wabongo hawajitokezi Kwa kiwango hicho kutokana na hofu zisizo na msingi.πŸ‘‡πŸ‘‡

View: https://www.instagram.com/p/C3QYv4pNXlw/?igsh=MWcyMWw0b2Q3Njk3cQ==
My Take
Ndugu zangu Wabongo tubadilike,Maisha Bora yanahitaji kuwa aggressive vinginevyo tutaishia kulaumu,kutegemea miujiza na maigizo ya Wanasiasa na watafuta fursa.

Tusiogope ushindani tukapambane,tusomeshe Watoto Wetu kupambana Duniani,tunazidiwa mbali sana na Majirani zetu kwenye nyanja mbalimbali na ndio maana tunaogopa free movements of trade and Labour.πŸ‘‡πŸ‘‡


View: https://twitter.com/BusInsiderSSA/status/1712116594938122403?t=leN8oacL4sBM9PdmHoZk9g&s=19
 
Ccm ime-invest ktk ujinga. Jana nimemsikia kiongozi wao mmoja kipindi cha The Big Agenda starTv- pumba tupu-. Anaulizwa ccm ni jambo gani wanaloweza kusema wamefanikiwa sana ktk miaka 47, anasema ni kudumisha amani na utulivu. Hivi Kenya hakuna amani? Rwanda hakuna amani? Au nje ya afrika mashariki, Botswana, Egypt, Vietnam, mMalasya etc hakuna amani? Yaani ccm wanatuambia ili tuwe na amani lazima tuwe masikini. Sasa unaambiwa jirani yako tu Kenya diaspora wana-remit trillion 10 while wa kwako wana-remit trillion 0.7 unjitetea eti sisi tuna amani. Hii ni akili au tope?
 
Ningeona Egypt au SA hapo juu kabisa, hoja yako ingeweza make sense, bali naona zile nchi zenye Njaa
wanaotegemea remittances ni omba omba
 
Kimsingi wa Kenya wametuzidi sana...
Wa Tanzania wengi marekani...hufanya kazi kwa wa Kenya...bila wakenya waTanzania hatuna maisha.
 
Bila shaka..lipo tatizo la tafsiri ya Amani.
 

Unajua TZ kuna vitu tunavichukulia powa lakini vinatugharimu. Swala la watanzania kuchangia pato la taifa lipo wazi. tukiambiwa turuhusu uraia pacha, tunaona kama watakuja kuiondoa CCM madarakani. Tanzania inabidi ipambane vijana wake wajitafutie fursa huko nje. Leo mtu akiongelea swala la kutafuta maisha nje, mjadala unahamia kwenye changamoto na mambo mengine ya ujinga. hatuangalii ni faida zipi.

Tuamke, tutengeneze mazingira wezeshi vijana waingie kitaa huko kati wakatafute maisha. ukweli ni kwamba wakiwa nje, wata support familia zao, watawekeza nk. Hivi wewe unaweza kuwekeza hela unayoipata kwa jasho, kwenye nchi inayokuvizia? wakiona una passport ya US au kwingine...wao wanaona fursa ya dola 100 ya visa.

Ungetegemea hawa viongozi wenye uelewa watusaidie lakini wapi...wanalinda kibarua na maslahi ya watoto wao.

Ukweli siku zote ni kwamba Masikini ni fursa kwa wenye pesa, akili na madaraka!

Watanzania tubadilike!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…