Wakikataa kumfanyia ibada ya mazishi nduguyo Niite Mimi nitamfanyia bure kabisa

Wakikataa kumfanyia ibada ya mazishi nduguyo Niite Mimi nitamfanyia bure kabisa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
WAKIKATAA KUMFANYIA IBADA YA MAZISHI NDUGUYO, NIITE MIMI NITAMFANYIA BURE KABISA.

Na, Robert Heriel
Kuhani

Huna haja ya kuwa mnafiki Kwa kuogopa hautazikwa.
Tupo ambao tunajua kuendesha Ibada za namna yoyote Ile na zikafanikiwa Kwa kiwango cha juu Kabisa.
Kwanza elewa kuwa hata usipozikwa hakipungui au kuongezeka kitu.

Tutakuzika Kwa upendo wala hatutataka kujua Historia yako, matendo yako, sijui ulikuwa Nani au lolote kukuhusu wewe.
Sisi tutakachohitaji ni uthibitisho umekufa Basi. Tutakuzika Kwa Imani unayoitaka wewe. Kwa kitabu unachokitaka wewe.
Iwe ni Biblia, iwe ni Quran, iwe ni Voodoo, iwe ni Mila na tamaduni za kiafrika tutakuzika ulale Kwa amani, japo tunajua hakuna Amani yoyote mtu akifa kwani hatambui neno lolote.

Yaani watu mpendwa wao amekufa ninyi badala muone namna ya kuwasaidia na kuwatia moyo, wapo kwenye majonzi, ninyi mnaleta mambo Yenu ya kikafiri na kipagani ya kufa kufaana. Ati marehemu alikuwa Blah!blah! Blah! Yaani hakuna mantiki yoyote. Zaidi ya tabia ya ubinafsi wa baadhi ya watu. Wewe Baba au Mama yako au mtoto wako angekufa ungesema hizo Blah!Blah! Zako?

Taikon na Makuhani wote hatutachaji hata shilingi Mia moja ya wafiwa.
Mtu au kikundi cha watu kisikutishe kuwa hakitakuzika ikawa ndio sababu ya kukupeleka peleka watakavyo.

Misiba sio sehemu ya kukomeshana,
Misiba sio sehemu ya kulipana kisasi tena Kwa watu wanaojiita wa Mungu.
Misiba sio sehemu ya kuhukumiana,
Kama kiongozi WA dini mkimuita aje kuendesha Ibada akakataa Kwa sababu yoyote Ile, hameni hilo dhehebu, kimbieni huo utamaduni upesi.
Dini inaongozwa na maandiko matakatifu wakati madhehebu ndio huongozwa na sheria za binadamu Kama Mimi na Wewe tuu.
Mwambie huyo kiongozi WA dini yako akuonyeshe andiko la kwenye Biblia au Quran linalozuia maiti isizikwe Kwa sababu yoyote Ile. Mwambie asikuonyeshe sheria za madhehebu Bali sheria za Dini.
Asipokuonyesha hameni upesi, hampo sehemu sahihi.

Mambo ya kuyaelewa kuhusu ibada ya mazishi;
1. Mwanaume yeyote aliyekichwa cha familia au Ukoo anayejua Mila na desturi na Imani. Anaweza kuendesha Ibada ya mazishi.

2. Mwanaume mwenye umri kuanzia miaka 25 anaweza kuendesha Ibada ya mazishi ikawa sio kosa.

3. Sio lazima maandiko ya Biblia au Quran kutumika siku za mazishi.
Maneno yoyote ya kujenga na kufariji wakati mazishi yanaweza kutumika. Ila ingefaa zaidi Maneno yatolewe kulingana na utamaduni wa watu husika. Kama ni Wapare yatolewe mafundisho na hadithi za kipare zenye Mafunzo na maonyo na faraja.

4. Mwanamke hatoruhusiwa kuongoza ibada za mazishi labda Katika mazingira maalumu. Mfano, Yupo porini na mtoto ikatokea mtoto amefariki, basi Mama anaweza endesha mazishi hayo bila shida yoyote Ile.

5. Mtu huweza kuzikwa muda wowote na wala hakuna muda maalumu wa kuzika. Hata hivyo inafaa mwili uzikwe mapema zaidi mara baada ya mtu kufariki.

6. Ibada yoyote ya mazishi haina maana yoyote Kwa Maiti/marehemu. Isipokuwa ni kwaajili ya waliobaki hai.
Tunazikwa ili tusinuke na kusumbua waliohai. Maiti haisikii hiyo harufu mbaya na wala haijui lolote kati ya yale tunayoufanyia.

7. Mtu akifa amekufa hakuna mambo ya misukule.
8. Kujenga kaburi sio Kwa ajili ya Marehemu Bali kwaajili ya waliohai.
Hakuna lolote utakaloweza kulifanya kwaajili ya maiti/marehemu.
Mambo ya kuweka misalaba au Alama Fulani ni Imani za mizimu.

9. Kuna wazazi au watu wanatabia ya kutishia watu Kwa kusema; usinizike au usije kwenye kaburi langu"
Kauli hiyo mara nyingi haina maana yoyote isipokuwa huwa inatumiwa kutishia watu wajinga wasio na Uelewa wa mambo hayo.
Maiti haina inachomiliki hivyo haina kaburi wala haina msiba. Wenye makaburi na Misiba ni waliohai.

10. Viongozi wa dini wanaotishia kutokuzika watu hutumia ujinga wa waumini wao kuwatishia.
Hakuna anachokipata kiongozi WA dini anapoendesha ibada ya mazishi na wala maiti haitopata kitu chochote wala ninyi mliofiwa hamtapata lolote.
Hakuna tofauti ya mnyama na binadamu linapokuja suala la kifo.

Hivyo hata Mimi nikija kufanya ibada ya mazishi sio Kwa sababu ya Hiyo maiti wala sio Kwa sababu ya Mimi mwenyewe Bali kwaajili ya kutoa maneno yenye kujenga Kwa ajili ya Sisi tulikuwa hai. Jambo ambalo mtu yeyote katika familia yenu anaweza kulifanya.
Na pointi yangu iko hapo, kuwa sio lazima Aje mtu Fulani kufanya ibada ya mazishi ya nduguyo au mpendwa wako/wenu. Mtu yeyote hapo kwenye aliyemwanaume anaweza fanya ibada hiyo na ikawa pouwa tuu.

Tukio muhimu kuliko lilikuwa ni kifo na sio Mazishi. Ndio maana wapo watu hufa bila kufanyiwa mazishi, wengi huliwa na wanyama, wengine walikufa Kwa Moto au baharini.

Mazishi yapo Kwa ajili ya;
1. Kuleta uhusiano miongoni mwa waliobaki na sio kutafutana maneno maneno.
Mazishi yanatumika kuondoa tofauti na migogoro iliyopo kwenye familia, ukoo na jamii. Na sio kuibua uhasama na kuchochea maugomvi kisa mtu aliyekwisha kufa.

2. Kujua na kuthibitisha mwisho wa Mtu Fulani na kujua mahali alipozikwa ingawaje hakuna umuhimu wowote.

3. Kumuombolezea Marehemu na kuonyesha upendo Kwa wafiwa.
Sasa sio mlete chuki na visasi, hizo ni tabia za kishetani.

Mwisho; Nduguyo akifa na ikatokea changamoto ya namna hiyo kwamba dhehebu lako halitaki kumzika nduguyo, nawe ni mwanaume, basi chukua jukumu la kuendesha Ibada ya mazishi, mzike nduguyo Kwa Amani.
Kama huwezi tafuta Rafiki au jamaa mwenye uwezo wa kufanya hivyo. Kama hayupo basi Niite Taikon nitakamilisha hiyo misheni ya kuhitimisha uwepo wa ndugu yako Duniani Kwa kumhifadhi kaburini.
Kisha hama Hilo dhehebu mara moja wala usifikiri mara mbili.

Wito Kwa madhehebu ya Dini, niwaombe viongozi wa dini muondoe baadhi ya sheria mlizojitungia kususa maiti za waumini wenu. Hakuna sababu yoyote ya kususia Kuzika maiti.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Sahih kbsa, wachungaji na wainjilisit wakekuwamiungu watu
 
Huu upuuzi wa kutishana kuzika ni kqajili ya kutisha waumini wa makanisa kuchangia michango na sadaka,
 
Linapokuja suala la Kifo hakuna tofauti kati ya Mnyama au Mtu wala Maskini au Tajiri.
 
Kwani mababu zetu walizikwa kwa ibada? Mtu unaogopa eti kanisa halitakuzika!!! Ila kwa maajabu ukiwa na pesa utazikwa na kanisa. Dini ni biashara, turudi kwenye maziko ya jadi.
 
Mtu ni kama mnyama akifa amekufa hakuna kipya kinacho endelea pale, mbwembwe za viongozi wa dini kupigia kelele/maombi maiti ni ujinga mtupu.

: Huu ujinga haupaswi kuwa tishio kwa waumini wao walio hai.
 
Mtu ni kama mnyama akifa amekufa hakuna kipya kinacho endelea pale, mbwembwe za viongozi wa dini kupigia kelele/maombi maiti ni ujinga mtupu.

: Huu ujinga haupaswi kuwa tishio kwa waumini wao walio hai.
Siku ya mazishi Kuna maneno makali hutolewa na viongozi wa dini utadhani wenyewe hawana dhambi
 
Kweli tupu. Nikifa nitakutafuta uje unizike

giphy.gif
 
Issue siyo kuzikwa, ila issue ni Je, umekufa katika imani aliyoiacha YESU KRISTO?, Au umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani?

Kama umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani maisha yako ya huko uendako yanakosa SECURITY.

Demokrasia ni jambo zuri katika maisha ya KISIASA na aina nyingine za maisha, katika IMANI tunazo AMRI za MUNGU ambapo ukitaka kwenda kwa MUNGU ni lazima uzizingatie na hakuna mbadala.

NB:
Mtu yeyote akifa katika jamii lazima atazikwa. Ila mtu atajisikia salama zaidi akifa katika imani halisi aliyoiacha YESU kwa Mitume wake na siyo vinginevyo.
 
Issue siyo kuzikwa, ila issue ni Je, umekufa katika imani aliyoiacha YESU KRISTO?, Au umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani?
Kama umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani maisha yako ya huko uendako yanakosa SECURITY.
Demokrasia ni jambo zuri katika maisha ya KISIASA na aina nyingine za maisha, katika IMANI tunazo AMRI za MUNGU ambapo ukitaka kwenda kwa MUNGU ni lazima uzizingatie na hakuna mbadala.
NB:
Mtu yeyote akifa katika jamii lazima atazikwa. Ila mtu atajisikia salama zaidi akifa katika imani halisi aliyoiacha YESU kwa Mitume wake na siyo vinginevyo.

Kwa hiyo wewe Kwa Uelewa wako mtu akizikwa na Dini Fulani ndio anakuwa na uhakika wa kwenda peponi?

Kinachompeleka mtu mbinguni au sehemu nzuri ni matendo yake, na wala sio Imani yake.

Zingatia Imani hujengwa na matendo.
 
Issue siyo kuzikwa, ila issue ni Je, umekufa katika imani aliyoiacha YESU KRISTO?, Au umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani?
Kama umekufa katika mikono ya tapeli wa kiimani maisha yako ya huko uendako yanakosa SECURITY.
Demokrasia ni jambo zuri katika maisha ya KISIASA na aina nyingine za maisha, katika IMANI tunazo AMRI za MUNGU ambapo ukitaka kwenda kwa MUNGU ni lazima uzizingatie na hakuna mbadala.
NB:
Mtu yeyote akifa katika jamii lazima atazikwa. Ila mtu atajisikia salama zaidi akifa katika imani halisi aliyoiacha YESU kwa Mitume wake na siyo vinginevyo.
maisha gani tena anayo yaendea uko mbeleni??? mtu akifa amekufa kama kuna maisha mtu akifa siku ya mwisho mungu atawafufua wakina nani sasa na anakuja kufanya nini kama watu teali yupo nao mbinguni??
 
Back
Top Bottom