Wakili CHADEMA athibitisha Mnyika kuitwa Polisi Kinondoni, RPC asema hana taarifa

Wakili CHADEMA athibitisha Mnyika kuitwa Polisi Kinondoni, RPC asema hana taarifa

Naona humu badala ya kujibu mada na kuchangia , vijana tayari wamekula ya ksamulu(Bangi)matusi Tena!
 
Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika ameitwa polisi kutoa maelezo kuhusu taarifa ya kutekwa kwa Mshauri wa Chadema Bw. Kibao ambaye baadaye alikutwa ameuawa na mwili wake kutupwa maeneo ya Ununio Jijini Dar es Salaam.

Ni jambo jema Mnyika akatoe maelezo ya kina kuhusu namna alivyopata taarifa hiyo. Aidha ni vema akaambatana na mawakili wa chama ili asije akawekewa maneno mdomoni na pia kupelekwa kusikojulikana!
 
Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika ameitwa polisi kutoa maelezo kuhusu taarifa ya kutekwa kwa Mshauri wa Chadema Bw. Kibao ambaye baadaye alikutwa ameuawa na mwili wake kutupwa maeneo ya Ununio Jijini Dar es Salaam.

Ni jambo jema Mnyika akatoe maelezo ya kina kuhusu namna alivyopata taarifa hiyo. Aidha ni vema akaambatana na mawakili wa chama ili asije akawekewa maneno mdomoni na pia kupelekwa kusikojulikana!
Kama Mimi ni myika na Sheria ikininirusu siendi kwa wauaji
 
Polis nao vichwa boga mbona wanaanza mbele kwenda nyuma washamuita sativa ?
 
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika ametakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Oysterbay Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano, Wakili wa chama hicho amethibitisha...
Yale mambo ya kishenzi ya Magufuli bado yanaendelea!
 
Nashauri asiende peke yake,maana anaweza kupotea tuuu na tusijue aliko,polisi wakiulizwa waseme hawakumwita wao😃😃
 
Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika ametakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Oysterbay Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano, Wakili wa chama hicho amethibitisha.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Septemba 12, 2024 Wakili wa Chadema, Hekima Mwasipu amesema kiongozi huyo ameitwa na Ofisa Upelelezi wa Mkoa (RCO) wa kipolisi wa Kinondoni, japo hawakuambiwa anaitiwa nini.

“Ni sahihi kwamba Mnyika ameitwa. Tuliletewa taarifa kwamba anaitwa, lakini kwa sasa yupo mkoani Tabora. Nitampeleka kesho (Septemba 13, 2024),” amesema.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mtatiro Kitinkwi alipoulizwa kuhusu wito huo, amesema hana taarifa kwa kuwa yupo nje ya kituo chake cha kazi.

Kuhusu sababu za wito huo, Wakili Mwasipu amesema hawajaambiwa, lakini wanahisi ni uchunguzi wa matukio ya utekaji.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

“Kuna siku Mnyika alieleza kuwa matukio ya utekaji yachunguzwe, kwa hiyo nadhani ndio wameanza uchunguzi wao,” amesema.

Hata hivyo, Mnyika alipotafutwa kwa simu hakupokea.

Taarifa za wito wa Mnyika zilianza kusambaa jana usiku Septemba 11, 2024 baada Meya wa zamani wa Kinodnoni na Ubungo, Boniface Jacob kuandika kwenye ukurasa wake wa X akisema; “Nimetaarifiwa kuwa Jumanne Septemba 10, 2024 Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kupitia RCO Kinondoni waliwapigia simu mawakili wa Chadema kwamba wanamhitaji Katibu Mkuu, John Mnyika kwa mahojiano.”

Mwananchi

Vipi ndiyo hao wasiojulikana lakini wanafahamika Polisi ndiyo walioandika barua hiyo kwa katibu mkuu wa CHADEMA kisha yaliyowapata Deusdedith Soka, Mbise na Mlay yamfike John John Mnyika waseme hawajui alipo Katibu Mkuu wa CHADEMA baada ya kupokea wito toka polisi.
 
Huku mtaani sisi tunapambana na hali zetu ila haiwi habari.

Wanasiasa wakiguswa hata na Jani tu wanalia lia na kutaka dunia nzima tulie pamoja nao.

Wanasiasa wabinafsi mno.

Wanasiasa ni kakikundi flani cha matapeli tu wanaojipa mamlaka juu ya wengine.
 
Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika ameitwa polisi kutoa maelezo kuhusu taarifa ya kutekwa kwa Mshauri wa Chadema Bw. Kibao ambaye baadaye alikutwa ameuawa na mwili wake kutupwa maeneo ya Ununio Jijini Dar es Salaam.

Ni jambo jema Mnyika akatoe maelezo ya kina kuhusu namna alivyopata taarifa hiyo. Aidha ni vema akaambatana na mawakili wa chama ili asije akawekewa maneno mdomoni na pia kupelekwa kusikojulikana!
Kama Rais ameshasema ataunda kwanini aende?
 
Nashauri Mnyika Ahojiwe Mbele Ya Vyombo Vya Habari Kwa Uwazi.
 
Back
Top Bottom