Wakili Jebra Kambole amesema "Bado wanashikiliwa kituo cha polisi na hawajapewa dhamana Lakini tumeshapeleka kesi mahakamani kuomba waletwe mahakamani pamoja na wakili Philip Mwakilima, Boniface Mwabukusi na Nickson Kiliwa."
Mwimbaji huyo Sifa Boniventure Bujune (25) ni Mkazi wa Isyesye anatuhumiwa kuimba wimbo unaojulikana kwa jina la “Tanzania Inaelekea Wapi?” unaodaiwa kuwa na maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kisha kuurusha katika Mitandao ikiwemo YouTube
Alikamatwa Septemba 13, 2023 akiwa Isyesye-Mbeya na bado anaendelea kuhojiwa kwa hatua zaidi za kisheria
Pia soma
Mbeya: Msanii wa Nyimbo za Injili, Sifa Bujune ashikiliwa kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi