Wakili Peter Madeleka: Kuna changamoto ya mifumo ya utoaji haki jinai

Wakili Peter Madeleka: Kuna changamoto ya mifumo ya utoaji haki jinai

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kesi ya jinai inayomkabili Afisa wa Jeshi la Polisi Fatma Kigondo, anayejulikana kama 'Afande', ikimhusisha na tuhuma za kuratibu ubakaji na ulawiti wa kundi dhidi ya binti wa Yombo Dovya, Dar es Salaam, imeendelea kupata changamoto baada ya kutolewa uamuzi mdogo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Dodoma.

Katika shauri hilo, upande wa mlalamikaji uliomba Mahakama kutoa amri ya kukamatwa kwa mtuhumiwa na kufikishwa mahakamani. Hata hivyo, Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Nyamburi Tungaraja, ameeleza kuwa si jukumu la Mahakama kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha mahakamani. Uamuzi huo ulizua maswali zaidi, hasa baada ya upande wa washtakiwa kutohudhuria mahakamani siku hiyo.

Baada ya kikao hicho cha Mahakama, Wakili wa mlalamikaji, Peter Madeleka, amezungumza na wanahabari na kueleza nia yake ya kupeleka maombi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, ili kufuatilia na kupitia mchakato mzima wa uendeshaji wa kesi hiyo. Wakili Madeleka amedai kuwa kumekuwa na ukiukwaji wa sheria katika usikilizwaji wa shauri hilo.

Wakili huyo pia ametoa malalamiko kuhusu kitendo cha Hakimu Tungaraja kumfokea mahakamani, jambo ambalo aliliona kama kukosewa heshima mbele ya Mahakama, na amekusudia kumpeleka Hakimu huyo kamati ya maadili kwa kitendo alichodai kukifanya.

Madeleka amedai kuwa hana imani tena na Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma na kwamba kutokana na mazingira hayo, hawaoni haja ya kuendelea na shauri hilo mbele ya Mahakama hiyo.

Ingawa kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 16, 2024, upo wasiwasi kuhusu mwenendo wake kutokana na malalamiko ya upande wa mlalamikaji kuhusu kutotendewa haki.

Stori: Jambo TV (Oktoba 15, 2024), Video: Global TV
 
Back
Top Bottom