Raj kapool
JF-Expert Member
- Jun 29, 2018
- 1,352
- 2,160
.......Na ilipelekea wachezaji wa Yanga kugoma kule Mombasa kwenye klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati nafikiri ilikuwa mwaka 1984 wakidai acheze Elisha John.Aamin. Ingawa hawa wachezaji walicheza katika vipindi viwili tofauti. Wakati Yanga Fadhili Bwanga alivuma miaka ya 1970s akiwa Dar Young Africans, Elisha John alitingisha miaka ya mwanzo ya 1980s akitokea Coastal Union kwenda Simba SC kisha Young Africans
Usajili wa Elisha John kutoka Simba kwenda Yanga ulivunja rekodi ya fedha ya uhamisho pamoja na kwamba soka lilikuwa la ridhaa wakati huo huku akiwa analipwa mshahara mnono tofauti na wenzie kitendo kilicholeta mtafaruku kwenye timu ikiwepo kuletwa mgomo baridi miongoni mwa wachezaji wengine
Upo sahihi kabisa mkuu. Tena mashindano yale Yanga ilikua iko vizuri sana maana walianza kwa kuwachapa mabingwa wa Zambia wakati huo Nkana Red Devils bao 2-0.......Na ilipelekea wachezaji wa Yanga kugoma kule Mombasa kwenye klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati nafikiri ilikuwa mwaka 1984 wakidai acheze Elisha John.
Nakumbuka Elisha alipewa na Yanga shilingi laki moja 1983 wakati anatoka Simba, ilikuwa hela nyingi sana wakati ule. Baadaye Elisha baada ya mambo kumuwia vigumu Yanga aliamua kutimkia Uarabuni.