Wakristo tujifunze kwa ndugu zetu Waislamu, wakati wa kufuturu unapata futari popote pale kwa urahisi bila bughuda, manyanyaso au kusubiri mwaliko

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Nasema Kwa dhati ya moyoni ndugu zetu ni wakarimu sana kutuzidi.

Mimi ni Mkiristo lakini nitumie fursa hii kuwapongeza sana Waislamu walio kwenye mfungo Kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa baina Yao na wengineo wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan.

Kwao utapata futari bila kujali Imani yako au kuulizwa unakotokea tena bila manyanyaso au kuulizwa mwaliko

Ukweli wanatimiza amri ya upendo kikamilifu kama ilivyoagizwa kwenye Vitabu vitukufu

Ndugu zangu wakiristo tunamengi ya kujifunza kutoka kwa ndugu zetu Waislamu
 
Njaa mbaya sana
 
  1. M'moja anafunga , m'moja anabadilisha muda wa kula!
  2. Wana abudu "mungu" tofauti hawawezi fanana!
  3. Wana imani tofauti.
  4. Wana abudu Mungu na "miungu" tofauti!
 
Mimi ni Mkiristo lakini nitumie fursa hii kuwapongeza sana Waislamu walio kwenye mfungo Kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa baina Yao na wengineo wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Acha kuwaza kula kula. Waza namna ya kuwasaidia wahitaji, sio wafuturuji. Funga, hela au mali unayookoa nenda kamsomeshe VETA mtoto walau mmoja wa familia iliyokwama. Ukarimu sio kwa mambo ya muda mfupi kama futari
 
Mbona neno lipo wazi? "asiyefanya kazi asile" kwa nchi yetu pamoja na yote ukijituma swala la kula halihitaji harambee.
 
kitu kingine mkuu usichokijua tofauti yetu na waislamu , wakristo wengi hatufungi kula kama waislamu wengi hufanyanyo bali sisi tumejikita kufunga matendo yetu maovu na kijikita kuomba toba na kusali sana huku ukiwa mtu wa kusaidia wengine wasiojiwezi ndio wakristo wengi mfungo wao upo hivyo tofauti na waislamu wao pia hufanya vyote wakristo hapo wanavyofanya ila kwenye kufunga hufunga mpk kula na ni lazima kwa muislamu kufanya hivyo labda uwe na shida binafsi na ukipona utazifidia siku hizo mbeleni huko ndio maana huwezi ona wakristo wamekaa wanafuturu wote sehemu moja kama waislamu hufanya kukaq nje ya nyumba zao na kula futari yao kwahiyo hatutaweza kufanana ....sema tu uache uroho 😂 mleta mada
 
Hujaongea baya ila ona unavoshambuliwa,yaani watu wanaongozwa sana na hisia kuliko fikra!
 
Acha kuwaza kula kula. Waza namna ya kuwasaidia wahitaji, sio wafuturuji. Funga, hela au mali unayookoa nenda kamsomeshe VETA mtoto walau mmoja wa familia iliyokwama. Ukarimu sio kwa mambo ya muda mfupi kama futari
Sasa kama umeshindwa kumsaidia mtu sahani ya wali ya buku 2 ndio utaweza kumlipia ada ya milioni?
 
Watasema wewe ni muislamu unajipigia promo
 
Nani amekum Nani amekuambia waislamu wanafunga kula? Ndiyo mnavyofundishwa huko sunday school?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…