Wakulima hawapaswi kusherekea sherehe za Uhuru Desemba 9

Wakulima hawapaswi kusherekea sherehe za Uhuru Desemba 9

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Wakulima wanahali mbaya kuzidi hata enzi za mkoloni. Uhuru wao bado kufika.

1. Wakati wa mkoloni kulikuwa na bodi za mazao, lengo lake ilikuwa ni kupanga bei na kumnyonya mkulima. Tulipopata uhuru zikaendelea na kuwekwa kitu kingine kinaitwa vyama vya ushirika. Hivi vinanunua mazoa kwa bei ya chini halafu vinauza nje na kisha vinapiga faida. Bei ya dunia ya mazao inaweza kupanda lakini vyama hivi havipandishi. Gharama za uzalishaji zinapozidi kukua watu wanaamua kuacha kulima au kuuza kwa magendo. Kama wakulima wa kahawa Kagera.

2. Mkulima ndiye mtu ambaye hana uhuru auze wapi matunda ya jasho lake. Hana uhuru huo kabisa. Serikali inamlazimisha kuuza kwa vyama vya ushirika nk, na kwa wale wa chakula imekuwa ikifunga mipaka.

3. Mkulima ndiye anayelipa madeni ya nchi lakini siye anayefaidika na mikopo hiyo. Serikali inakopa pesa na kujenga hospitali, barabara za lami, mifumo ya maji nk maeneo ya mijini. Lakini watu hawa wa mjini hakuna wanachozalisha kikaingiza pesa za kigeni kulipa madeni, kama kipo ni kidogo mno. Nchi inategemea kuuza kahawa, pamba, korosho, chai nk ili kupata pesa za kigeni kulipa madeni. Hivyo aneyefaidika na mkopo halipi na anayelipa hafaidiki nao.

Mkulima bado hajawa huru.
 
Umedanganya na hujui Nini maana na malengo na shughuli za Ushirika.
Chama Cha Ushirika wa mazao (AMCOS) kinapopata faida nani anafaidika nayo?
 
Nasapoti point namba 3.

Ni kweli, mkulima ni miongoni mwa wananchi wanaoumia, kwa kulipa mikopo ya nchi kupitia mazao yao hasa ya biashara.

Bei za mazao mfano tumbaku katika soko la dunia, huwa inakua juu, lakini serikali inachukua chake mapema, halafu mkulima anabaki na hela ndogo ambayo itamfanya aendelee kulima na kuishi katika umaskini maisha yake yote!

Mkulima wa tumbaku angekuwa tajiri nchi hii kama angekuwa anapewa kikubwa kuliko kinachochukuliwa na serikali.
 
Kushukuru kama amcos wanalipa kidogo, maana mie nilisha poteza zaidi laki saba, awajanilipa na sina cha kuwafanya, mikutano hadi kwa DC, hamna kitu!
 
Umedanganya na hujui Nini maana na malengo na shughuli za Ushirika.
Chama Cha Ushirika wa mazao (AMCOS) kinapopata faida nani anafaidika nayo?
Kama wakulima wangekuwa wanafaidika ungeona hata hali zao zimeboreka, je umefika vijijini ukaona hali zao zikoje ?? Au unaziogopa tope za huko ??
 
Kifupi kesho ni sherehe za uhuru wa ccm kutawala zaidi ya miaka 60
 
Back
Top Bottom