Pre GE2025 Wakulima wa korosho kumchangia Rais Samia pesa ya form urais 2025

Pre GE2025 Wakulima wa korosho kumchangia Rais Samia pesa ya form urais 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Vyama vikuu sita (6) vya wakulima wa mikoa minne (4) inayolima Korosho kwa wingi hapa nchini wamesema wanatarajia kutoa shilingi milioni 11 ili kumchukulia fomu Rais Samia Suluhu Hassan ya kugombea nafasi ya URais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani (2025), ambapo watamchukulia fomu hiyo pindi muda utakapofika, sambamba na kumuwekea mafuta kwenye gari lake wakati wa kampeni kwa kumshukuru kwa aliyowafanyia wakulima wa korosho katika utawala wake.

Soma Pia: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Wakulima wa mkoa wa Pwani (CORECU) Musa Mng'ereza amesema hayo kwa niaba ya Wenyeviti wenzake wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Rufiji, mkoani Pwani ambapo amesema, "kwa mapenzi yao wakulima wa korosho wa maeneo hayo wameamua ifikapo mwaka 2025 watamchangia pesa ya kuchukua fomu na pesa ya mafuta".

Amevitaja vyama vitakavyoshiriki kuchanga fedha hizo kuwa ni pamoja na CORECU, RUNALI, Lindi Mwambao, TANECU, MAMCU na TAMCU vyama kutoka mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma
Source Jambo tv


 
Umasikini ni mtaji mkubwa sana wa CCM, Na CCM hawako tiyali kuona umasikini unaisha katika Taifa hili. Hao wanao changa pesa ukifika kwao ndio utajua what is Poverty.
Unachanganya umasikini na ujinga au elimu duni.....inataka kumanisha kwamba Kenya hamna umasikini au Uganda wanaunafuu kutuzidi, kinacho sumbua nchi yetu ni elimu duni na unafiki.
 
Kuna wale chawa wa mama wakiona hbr km hii mioyo Yao kwatuuuuu..

Ngoja wa come
 
Wanelewa gharama ya fomu ya urais ni kiasi gani?

Wanajua wangapi wameshamchangia?
 
Back
Top Bottom