Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,909
- 32,414
Vyama vikuu sita (6) vya wakulima wa mikoa minne (4) inayolima Korosho kwa wingi hapa nchini wamesema wanatarajia kutoa shilingi milioni 11 ili kumchukulia fomu Rais Samia Suluhu Hassan ya kugombea nafasi ya URais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani (2025), ambapo watamchukulia fomu hiyo pindi muda utakapofika, sambamba na kumuwekea mafuta kwenye gari lake wakati wa kampeni kwa kumshukuru kwa aliyowafanyia wakulima wa korosho katika utawala wake.
Soma Pia: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Wakulima wa mkoa wa Pwani (CORECU) Musa Mng'ereza amesema hayo kwa niaba ya Wenyeviti wenzake wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Rufiji, mkoani Pwani ambapo amesema, "kwa mapenzi yao wakulima wa korosho wa maeneo hayo wameamua ifikapo mwaka 2025 watamchangia pesa ya kuchukua fomu na pesa ya mafuta".
Amevitaja vyama vitakavyoshiriki kuchanga fedha hizo kuwa ni pamoja na CORECU, RUNALI, Lindi Mwambao, TANECU, MAMCU na TAMCU vyama kutoka mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma
Source Jambo tv
Soma Pia: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Wakulima wa mkoa wa Pwani (CORECU) Musa Mng'ereza amesema hayo kwa niaba ya Wenyeviti wenzake wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Rufiji, mkoani Pwani ambapo amesema, "kwa mapenzi yao wakulima wa korosho wa maeneo hayo wameamua ifikapo mwaka 2025 watamchangia pesa ya kuchukua fomu na pesa ya mafuta".
Amevitaja vyama vitakavyoshiriki kuchanga fedha hizo kuwa ni pamoja na CORECU, RUNALI, Lindi Mwambao, TANECU, MAMCU na TAMCU vyama kutoka mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma
Source Jambo tv