Wakurugenzi na Maafisa 6 wa AICC wasimamishwa kazi kwa ubadhirifu

Wakurugenzi na Maafisa 6 wa AICC wasimamishwa kazi kwa ubadhirifu

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
IMG_20240409_120003_033.jpg

Wakurugenzi na Maafisa 6 wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) wamesimamishwa kazi kwa muda kuanzia Aprili 3, 2024 ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

Baadhi ya tuhuma hizo ni pamoja na kukiuka taratibu na kanuni za uendeshaji wa Mashirika ya Umma

Waliopumzishwa ni

1. CPA Savo Mung'ong'o (Mkurugenzi wa Fedha na Masoko)
2. Mhandisi Victor Kamagenge (Mkurugenzi wa Miliki na Miradi)
3. Mkunde Mushi (Mkurugenzi wa Mikutano na Masoko)
4. Festo Mramba (Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu na Utawala)
5. CPA Augustine Karadoga (Mhasibu Mkuu)
6. Catherine Kilinda (Meneja JNICC)

Taarifa ya AICC imesema taratibu nyingine za Kisheria zilizochukuliwa zitatangazwa baadaye.
 
Kama ni waTanzania, basi sina shaka na tuhuma dhidi yao...😜
 
mbona mawaziri wanapiga na hawasimamishwi uwaziri? kimsingi Tanzania wanaoneaga dagaa tu ila mapapa huwa hayaguswi, hiyo serikali ya mama yenu anayetajwa kila saa kuliko hata Mungu ina matatizo sana na kwa kipindi hiki ndio watu wanapiga hela kuliko kipindi kingine chochote kuwahi kutokea Duniani.
 
marehemu wanapumzishwa,, wezi nao wanapuzishwa mapumziko yaendelee serikali ya mapumziko tu wezi watazidi kuongezeka.
 
Back
Top Bottom