Wakuu msaada sehemu ya kuwapeleka wageni wangu Moshi

Kama wana maokoto shazi wapeleke kilimanjaro tinted camp. Vivutio watapata muongozo hapo
Hhapo kwenyewe nusu ya show itabidi nisimamie Mimi.
Shukran sana!
 
Hhapo kwenyewe nusu ya show itabidi nisimamie Mimi.

Shukran sana!
Wapeleke Kilimakyaro utakuja kunishukuru.

Hakuna mbabaishaji anafika huko na utakuta wazungu kibao wanakula maisha huko juu mlimani huku mji wote wa Moshi mnauangalia kwa chini kama bakuli tu.

Nakumbuka nilikodi bajaji kwa chini ya sh 10,000 kunipeleka kule juu na unakuwa na namba za Bajaj ukitaka kutoka unampigia anakufuata.

Sijakutajia mambo ya land cruiser kwa sababu najuwa hao ni wanafunzi halafu kwa Watalii kama hao bajaji ni Bonge ya adventure kwao.
 
Kuna mdau mahali fulani katoa hizi hints kwa wageni wakiwa Moshi na gharama ziko affordable sana.
1. Marangu waterfalls (hiking, swimming, history/culture)
2. Materuni waterfalls (Hiking&swimming(on waterfall)
3. Chemka hot spring (swimming on nature spring)
4. Miwaleni (Hiking, biking, camping, swimming)
5. TPC park (Hiking, Biking, Utalii wa wanyama)
6. Mountain Kilimanjaro National park (kuna geti la Marangu, Mashame, Kibosho)
7. Mwika wildlife (Hiking, historical site, Chaga culture)
8. Rau Forest (Utalii, Hiking).
9. Sarval wildlife (utalii wa wanyama)


Kwa vyakula na vinywaji.
1. Moshi pazuri
2. Mr. Price
3. YMCA
4. Uhuru Hostel (Hakuna pombe, pametulia, wanajua kuchoma nyama na wana malazi)
5. Kili home
6. Bikers
7. Polisi Mess
8. Mimis
9. Endoitaliano (pana vyakula vya kitalii sana, katika ya mji)
10. Amuz
11. Maikoz
12. Pub alberto
13. Moshi centre club
14. Red stone (hapa pana disco kubwa)
15. Malindi
16. Kilimanjaro Cafe union
17. Mwembe
18. Fresh coach Restaurant (Ni katikati ya mji, pametulia, hakuna pombe)
19. Uhuru Park (Ni katikati ya mji)
 
Nje ya mada.
Mkuu inaonekana kuna namna unawapata hao wazungu na unaitumia hiyo njia kujipatia kipato. Kama ni hivyo unaweza weka njia ya jinsi ya kuwapata ili kwa vijana tulio mji huu na sisi tupate chochote kitu, nawasilisha.
 
Ukitoa Huo Mlima Kilimanjaro Pa Kawaida Tu
 
Pub Alberto sasahivi haipo, labda Mimi's, Moshi pazuri na redstone Pamoja na hugos
 
Kwanini uwapeleke Moshi,,? Huko kila mtu mjuaji p,a,k "mpigaji" p,a,k " tapeli,,

Walete Mwanza,, hawatasahau trip yao na watakupongeza sana,,

Saanane Island, Bujola Museum, Bismarck Rock, Lake Victoria, Rubondo National Pack,, na mengine ya kushangaza,, bei ni ya kizarendo kabisa,,

Kuhusu Hotels,, za bei ndogo ndio usiseme sasa maana Mwanza sio ajabu kupata Lodge ya 10,000 self, full furnished, hot & cold water, Dstv, full security with CCTV ,, secure parking na chakula cha bei poa pia,,
 
wapeleke pale wachaga walipokanyaga mafuta ya kupata hela... zungusha peleka mpka matejo waonyeshe miti ya miraa inavyokua watoto wa chuga... wapeleke mererani wasimulie kesi ya bilionea msuya... wapeleke meserani wakaone nyoka... warudishe rau mtoni, huo mto una maji machache lkn haukauki, ukimaliza wapitishe kibosho wakaone Mbege kwa Olomi, waonjeshe hii kitu tamu kutoka Moshi.. usiku ukawalaze pale Memorio
 
Nilikua naaminishwa watu wa Kanda ya ziwa ni washamba na limbukeni,ila nilikua siamini sababu niliosoma nao shule hawakua washamba sana. Ila wewe Kwa comment yako tu nimejua ni mshamba sana na limbukeni. Ficha ujinga wako.
 
Mshamba.
 
Nilikua naaminishwa watu wa Kanda ya ziwa ni washamba na limbukeni,ila nilikua siamini sababu niliosoma nao shule hawakua washamba sana. Ila wewe Kwa comment yako tu nimejua ni mshamba sana na limbukeni. Ficha ujinga wako.
Kama imekuuma vaa uende,,
 
Kuna sehemu inaitwa njoro,kama sio pasua hapo Moshi mjini,naamini kwa utalii wandani watainjoi sana,good luck mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…