Wakuu nimechanganyikiwa - daktari yupi yuko sahihi?

Mara ya mwisho, niliingia ktk period 8 july, 2013, mwezi uliofuata sikuona siku zangu.

last menstrual cycle yako kama ilikuwa tarehe 8 July 2013 hesabu zinaniambia delivery date itakuwa tarehe 15 April 2014. Kuwa mvumilivu mama ingawa kunatokea mabadiliko kidogo kutokana na mabadiliko ya siku katika mwezi. E.g mwenzi mfupi na mrefu.
 

Asante Dina!
 
Last edited by a moderator:
kama trh za last menstrual cycle ni sahihi bac dr wa pili hayupo sahih
 
Wote wapo sahihi kulingana namna ulivyowaeleza. Calculation ya edd huwa inavary sana na hata walioiweka walisema its not obsolete! Wanawake wengi ukiwauliza siku zao za mwisho kwenda mwezini huwa wanataja tarehe ambayo alitegemea kuona na hakuona. Hui inasogeza mwezi mmoja mbele zaidi ya yule atakayetaja exact date ambayo alianza siku zake za mwisho kabisa. Daktari au nurse asopouliza kwa umakini zaidi anajikuta ameandika tarehe ambazo sio! By the way hongera kwa kufika mpaka wiki hizo.
 
Mara ya mwisho, niliingia ktk period 8 july, 2013, mwezi uliofuata sikuona siku zangu.

Kwa tarehe hiyo mpaka sasa una 39 weeks and 3 days. That means siku yoyote unaweza kuanza uchungu. Inakubidi kuwa makini uchungu ukikuanza maana huyo daktari wako wa hicho kijiji hana mawazo ya kwamba uko term. Usicheze mbali na hospitali.
 

Huyu anaonekana hawajajipanga na huyo mume wake. Mambo ya kubadirisha daktari siku za mwisho kabisa yamepitwa na wakati. Mtu aliyemakini atataka awe na daktari mmoja kipindi chote cha ujauzito mpaka atakapojifungua. Hii inarahisisha ufuatiliaji was mimba na maendeleo ya mama.
 
Dah....kweli tuwaheshima na kuwapenda mama zetu. Watoto wanne wote mama amerisk maisha yake na kukubali kisu. Hivi georgina george wataalamu wote wameridhika kwamba kamwe hutaweza kujifungua kwa njia ya kawaida? hebu mkabidhi mwenye enzi mungu kwa huyu kwani yeye kila jambo linawezekana. Wana JF wenzangu hebu tumuombee huyu mama kwenye sala zetu mungu ampe uwezo wa kujifungua kwa njia ya kawaida na salama. Kisu mara nne sio masihara
 
Last edited by a moderator:
Hongera kwa hatua uliyofikia. Kwa tarehe ya mwisho ulipoona hedhi uliyoitoa yaani tar8 July 2013, daktari wa kwanza yupo sahihi ijapokuwa kunaweza kuwa na variation ya siku chache. Lakini kwa ushauri wangu fanya maandalizi yote muhimu mapema na nenda clinic iliyo karibu mara unapoona kuna mabadiliko ya aina yoyote ile. Mungu akutangulie katika hili.
 

Mwenzangu...halafu kuishia na kuambiwa discrepancy ya mwezi mzima! Mbaya zaidi kama mwishoni ameishia kwenye huduma zisizo na uhakika sana....na jinsi issue za uzazi zisivyo lelemama.
 

Hiyo sala ifanye peke yako aise. Ingekuwa ni mimba ya pili ningekusaidia. Scar mara tatu aafu tuanze kumjaribu Mungu? Mimi namuombea ampate mtoto wake na yeye wakiwa wazima.

But, wonders never end!! Don't wait for wonders
 
Last edited by a moderator:
Mwenzangu...halafu kuishia na kuambiwa discrepancy ya mwezi mzima! Mbaya zaidi kama mwishoni ameishia kwenye huduma zisizo na uhakika sana....na jinsi issue za uzazi zisivyo lelemama.

Smart woman akishajijua ni mjamzito tu yuko tayari kutumia gharama yoyote ile ili mradi safari ya yeye na kijacho iwe salama. Mwenzenu kaamua kurudi kwa mama yake.
 

Mkuu Nyalotsi, kadi ya clinic inaonyesha history yote ya attendance yangu pamoja na vipimo vya Utra-Sound, sioni kama kuna tatizo sana.
 
Last edited by a moderator:

Kwa hiyo ndo umekuja nishitaki humu siyo eeeh,,,Sasa nakusubir hyo cku ya OP ndo utanielewa mii nan
 

Ameeen!
 
Kwa tarehe hiyo mpaka sasa una 39 weeks and 3 days. That means siku yoyote unaweza kuanza uchungu. Inakubidi kuwa makini uchungu ukikuanza maana huyo daktari wako wa hicho kijiji hana mawazo ya kwamba uko term. Usicheze mbali na hospitali.

Duuuh, mbona roho inaanza kudunda! Wiki nzima sipati usingizi hasa kuanzia saa 8 usiku hadi saa 10 alfajiri.
 
Mkuu Nyalotsi, kadi ya clinic inaonyesha history yote ya attendance yangu pamoja na vipimo vya Utra-Sound, sioni kama kuna tatizo sana.

Sisemei kuhusu hiyo tarehe na ultrasound. Discrepancy kati ya watu wawili imekuchanganya wewe wakati ungekuwa na yule uliyeanza naye usingepatwa na hali hii.
 
Last edited by a moderator:
Mara ya mwisho, niliingia ktk period 8 july, 2013, mwezi uliofuata sikuona siku zangu.

Kwa kurejea tarehe ulizotaja, mimba ulipata kwenye tarehe 22/07/2013, mimba yako sasa ina umri wa wiki 38 na tarehe tarajiwa ya kujifungua ni 14/04/2014, na inaweza kufikia hadi tarehe 28/04; hongera sana, nani kama mama?. Hesabu hii inategemea kwamba mzunguko wako wa hedhio ni wa kawaida, yaani siku 28. Kuhusu hao madakitari wawili, wewe rejea ushauri wa Mheshimiwa Rais wetu: Akili ya kuambiwa, changanya na yako!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…