Wakuu nimechanganyikiwa - daktari yupi yuko sahihi?

Salaam wana JF!

Nilileta uzi hapa wakati fulani mwezi April, 2014 kwa ajili ya kuomba ushauri wa kitabibu baada ya kuwa njia panda; rejea uzi wangu: [thread]9203690[/thread].

Namshukuru mwenyezi Mungu kwa yote kwani nilifanyiwa OP tarehe 13 May, 2014; OP ilichukua saa tatu na hivi sasa naendelea kuuguza mshono nikiwa na maumivu ya tumbo japo si makali sana!

Kwa namna ya pekee, nachukua fursa hii kuwashukuru wafuatao kwa mchango wao wa mawazo na ushauri:

Asheengai, ZeMarcopolo, raymg, BALAKI, The Boss, IBM2014, Mamndenyi, Shadya9, Dina, King Kong III, Vinci, nestor83, Mama Mdogo na wengine wengi ambao sikuweza kuwataja hapa.
Mwenyezi Mungu awabariki sana! Japo bado sijaweza kupata nguvu za kuandika sawa sawa, lakini nimeona nitoe shukrani zangu kwenu.

Asanteni sana wana JF!
 
Japo sikubahatika kupata kile nilichokua natafuta, lakini nashukuru kwa yote!
 
Karibu na tunakutamania kheri katika yote though umetuachia njiani kuwa tufunge kibwebwe kipi kusherehekea ujio wake...
 
karbu georgina, baby girl tena nn! but hongera kwa kujifungua salama
 
powa georgina,

kila la kheri. upone kabisa...

 
Pole kwa maumivu na hongera sana kwa mtoto, ipokee kama zawadi toka kwa mungu. nakutakia afya njema
 

Ninaamini mwenyezi mungu ni mkubwa na utakaa sawa tu soon pia atafanikisha uyatakayo ni kuzidi kumuomba tu, wish all the best
 
Nilikuwa sijasoma mahali kuwa mtoto gani amepatikana.....though bottom line ni kuwa mtoto ni mtoto....

Hi Dina! Ndiyo maana nimeandika kuwa, nashukuru kwa yote.
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana, georgina george "Mlee mtoto katika njia impasayo, naye hataiacha hata atakapokuwa mzee" Mithali 22:6
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…