Wakuu, ushauri wa mzee una hekima?

Wakuu, ushauri wa mzee una hekima?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna mzee mmoja alinishauri. na kuniambia; kijana, sikiliza ushuri wangu, kwa sababu nimekula chuvi nyingi; katika maisha yako ya mapenzi:-​
  • Hakikisha unakuwa na mahusiano na mama ntilie;- ili siku utakapokuwa na njaa, na huna sehemu ya kupata chakula, atakuhudumia.​
  • Hakikisha unakuwa na mahusiano na nesi:- ili siku utakapopata matatizo ya kiafya aweze kukusaidia.​
  • Hakikisha unakuwa kwenye mahusiano na askari:- ili pale utakapokamatika uweze kupata mtetezi.​
  • Hakikisha unakuwa kwenye mahusiano na daktari:- ili pale utakapohitaji matibabu akusaidie.​
  • Hakikisha unakuwa kwenye mahusiano na hakimu:- ili pale mambo ya kisheria yatakapohitajika akusaidie.​
  • Hakikisha unakuwa kwenye mahusiano na mwalimu:- ili aje akusaidie kuwalea watoto wako kwa kuwapa elimu bora.​
Wakuu, ushauri wa mzee una hekima?
 
Ushauri wa kijinga,
Maana huwezi kuwa na wanawake sita kwa wakati mmoja,.

Hata kama una hela, tambua Kuna magonjwa.
 
Kuna mzee mmoja alinishauri. na kuniambia; kijana, sikiliza ushuri wangu, kwa sababu nimekula chuvi nyingi; katika maisha yako ya mapenzi:-
Kuna wazee wenye mvi wasio na akili.

Angekuwa na akili angekwambia hakikisha unafanya kazi kwa bidii, wekeza katika miradi mbalimbali, somesha watoto wako shule nzuri na wapatie mahitaji yao ya msingi vizuri.
 
Naona wengi mnekurupuka, mtoa mada hajasema ni uhusiano gani. Hajasema kuhusu uhusiano wa kingono. Kasema mahusiano na yanaweza kuwa ni mahusiano ya kijamii. Babu amemshauri vizuri inatakiwa tuwe na mahusiano mazuri na jamii.
 
Wewe ni mpumbavu kabisa.. usisahau kushika kifua
 
Naona wengi mnekurupuka, mtoa mada hajasema ni uhusiano gani. Hajasema kuhusu uhusiano wa kingono. Kasema mahusiano na yanaweza kuwa ni mahusiano ya kijamii. Babu amemshauri vizuri inatakiwa tuwe na mahusiano mazuri na jamii.
Una akili nyingi sana!
 
Back
Top Bottom