Wakuu ushauri wenu ni muhimu, nimefilisika

Wakuu ushauri wenu ni muhimu, nimefilisika

Kwanza nianze kwa kumshukuru muumba wa mbingu na nchi kwa kuzidi kutupa afya makini sote kwa mapenzi yake.

Naamini siku zote Mungu hatupi tunachotaka bali unachostahili nimekulia maisha ya kijijini yenye uchumi wa kati yaani Nusu shibe robo mlo mmoja kwa miaka mingi takribani 16ya kuzaliwa.

Nimepitia vingi japo nimeishi kidogo sana uhalisia wa shida na hustles za kibabe sijapita sana zile za kutisha ama kupambana Nusu roho kutaka tengana na mwili ni ups and Downs za kidunia Tu ndio nimepitia zaidi

Nisijielezee sana nachoomba apa zaidi ni Ushauri kwa sasa ndio naingia 30 kwenye maisha yangu sina mengi ya kujutia zaidi ya kushukuru kwa Neema chache nilizopatia na kulaumu ndugu kwa kutamani umasikini.uwe na mimi.

Baada ya shule niliendelea na hustles za mtaani mdogo mdogo hatimaye nikaanza kujikimu na vijisenti vidogo kusaidia ndugu wenye uhitaji Simu zilikua hazikauki nikaendelea kupambana miaka ikasogea nikawa dalali wa viwanja na mashamba namimi nikaweza bahatika kumiliki kiwanja mjini.

Mambo yakaendelea nikanunua kagari kadogo kakutembelea nikaona umri usinibane nikamwita mwenzangu kuishi pamoja nikafanya Mambo ya mahari na miamala mingine ya kiutamaduni basi siku zikasogea.

Mungu akajalia familia ikakua tukapata na mtoto wa kiume nikafungua na kaduka mke akawa anauza siku zikazidi kusonga.

MAMBO YANABADILIKA
Mishe za mtaani zikaanza kua ngumu gari ya kutembelea nikaifanya Tax dereva kawa kwikwi nikawa naendesha mwenyewe Mambo yakazidi kua tyiti tairi zinakwisha, service inahitajika na trafiki wananikamata daily utazania wanatumwa kwangu tu

Udalali ukawa mgumu na mambo yakawa mazito basi nikawaza kufanya biashara zingine angalau niokoe jahazi.

Nikauza gari baada ya kupata wazo la uvuvi nikatengeneza mitumbwi kwa kushirikiana na jamaa mwingine hapa tuliingia partnership ya biashara tugawane faida baada ya kurudisha mtaji.

PICHA INAANZA KUUNGUA.
Biashara ikawa haieleweki leo unapata faida ya laki ndani ya wiki unakuwa una hasara ya laki kadhaa imani ya kupata ikashamiri nikaanza kukopa naweka pesa kuongeza mtaji.

NAZIDI KUPOTEA
Nikaanza kukodisha mitumbwi ya mashine unalipia mashine na mtumbwi 400k kwa mwezi hapo unaweka mafuta, unanunua mitego ama ndoano + chambo kusudi kazi ianze kazi inakuwa kama ni kubahatisha leo faida laki tatu ukirudi siku ingine faida kidogo ama hasara laki 2.

MAMBO YANAHARIBIKA ZAIDI
Kazi za uvuvi zinahitaji ushirikina uliotukuka ni SIRI watabisha ila ndio Ukweli nikaanza kushiriki na kutoa pesa kwa wategaji waweke Mambo kwa bibi sawa. hapa Mambo yakawa yanaenda Nusu Nusu yaani ile Mungu saidia sina imani na kesho lakini unafanyaje ushaambiwa ndio lazima.ufanye kusudi ufanikiwe kama wenzio.

Bwana wewe Mambo yakazidia ugumu nikaanza kuhama mialo WAPI bila bila mikopo ikaongezeka nikashindwa kulipa mingine marafiki wakapotea kwa madeni na wengine baaada ya kubadili lifestyle kuhamia visiwani.

NASITISHA BIASHARA YA UVUVI.
nikaamua kuacha uvuvi na kupaki mitumbwi huku deni la niliofanya nae partnership bado anadai pesa yake nikimweleza hali halisi haelewi kabisa nyuma MARAFIKI nao wananidai na sioni dalili ya kuwalipa

NAAMUA KURUDI KUKAA NYUMBANI NA FAMILIA.
Hapa napata ugumu zaidi dukani kwa mwezi faida ni kama 150000 mpaka laki 2 na 30000 elfu, familia ndio tunategemea duka kwa.kila kitu kodi, chakula na mengineyo mtaji ukaanza kupungua mchana na usiku mwisho nashtuka naona pakushika tena panapotea na sijui nifanyeje?

WAY OUT.
Nimewahi kufanya utalii kwa kipindi fulani na kupata pesa nikiwa NYUMBANI nilikokulia nikiwaza KURUDI naanzaje KURUDI mtaani kwa wazazi sina connection na wadau wa hizo Mambo tena nimetoka huko mda naendaga tu kusalimia. NAANZAJE na utalii ni kazi ya msimu!

DUKA liko mbioni kufilisika kabisa mda sio mwingi tena naanzaje na kodi nayo ikiisha tena naendeleaje?

NIUZE KIWANJA?
Woga unaingia biashara mpya nitakayoanza ikibuma MWISHO utakuaje? Wife ndio atakimbia na mtoto arudi kwao! Ama atakimbia aniache na mtoto nimpeleke akakae na Babu na bibi? hapa sijui mbele itakuaje?

MARAFIKI NJE YA Tanzania!
Nilipokua nafanya utalii nilipata friends Korea, Japan na Australia ambao bado tunawasiliana naweza kwenda nchi zao nikapata hosting. Je nikifanikiwa kuuza kiwanja na kupata nauli nikaenda kutafuta maisha mbele itasaidia? Mke na mtoto nyuma Tz inakuaje ?
USHAURI wenu WAKUU,

Wanaonijua hawaamini kama kweli Mambo yote yamenipitia ndani ya mda mfupi hivi nimefikia hatua Hii sina uhakika na kesho wanahisi naigiza lakini ndio hivyo TATIZO bado niko very positive na sijaonyesha kukataa tamaa jumapili nilikutana na mtu . mwenye shida nikamsaidia Asee Wife alinishangaa sana na kuona nimepagawa baada ya kutoa kiasi cha pesa kwa muitaji wakati NYUMBANI hakuna pesa yeyote ya dharura wala msalia mtume.

maisha mtihani ila mimi ni kama napitia MAGAZIJUTO NIKISONGA MBELE NAKOSEA KIDOGO TU NARUDISHWA NYUMA KABISA.

USHAURI NA Uzoefu wenu ni muhimu sana pia msisahau na sala zenu kwani yeye muweza mwenye nguvu hajawahi shindwa na gumu lolote.MAWAZO mengi niliyonayo kama mbadala naona yananichanganya zaidi na siyaelewi kabisa kwani naona kama nikurudi Utoto
pole sana kaka usikate tamaa.
 
Mkuu Mshukuru Mungu sana kwa maana bado kakupa akili ya kushtua ubongo wako mapema hivyo nafasi bado unayo, Tatizo unaingiza hofu ya kushindwa mapema.

Pia nirudi nyuma angalia kwenye maisha yako ya nyuma au ya udalali kuna mtu huenda ulimdhulumu kwa namna moja au nyingine?

Madalali mnakuwaga na katabia fulani siyo kazuri..... Piga maombi mlilie Mungu yatakwisha, tukisema kila mtu aandike hapa uenda wewe uko afadhali!!. [emoji3447]
 
Kwanza nianze kwa kumshukuru muumba wa mbingu na nchi kwa kuzidi kutupa afya makini sote kwa mapenzi yake.

Naamini siku zote Mungu hatupi tunachotaka bali unachostahili nimekulia maisha ya kijijini yenye uchumi wa kati yaani Nusu shibe robo mlo mmoja kwa miaka mingi takribani 16ya kuzaliwa.

Nimepitia vingi japo nimeishi kidogo sana uhalisia wa shida na hustles za kibabe sijapita sana zile za kutisha ama kupambana Nusu roho kutaka tengana na mwili ni ups and Downs za kidunia Tu ndio nimepitia zaidi

Nisijielezee sana nachoomba apa zaidi ni Ushauri kwa sasa ndio naingia 30 kwenye maisha yangu sina mengi ya kujutia zaidi ya kushukuru kwa Neema chache nilizopatia na kulaumu ndugu kwa kutamani umasikini.uwe na mimi.

Baada ya shule niliendelea na hustles za mtaani mdogo mdogo hatimaye nikaanza kujikimu na vijisenti vidogo kusaidia ndugu wenye uhitaji Simu zilikua hazikauki nikaendelea kupambana miaka ikasogea nikawa dalali wa viwanja na mashamba namimi nikaweza bahatika kumiliki kiwanja mjini.

Mambo yakaendelea nikanunua kagari kadogo kakutembelea nikaona umri usinibane nikamwita mwenzangu kuishi pamoja nikafanya Mambo ya mahari na miamala mingine ya kiutamaduni basi siku zikasogea.

Mungu akajalia familia ikakua tukapata na mtoto wa kiume nikafungua na kaduka mke akawa anauza siku zikazidi kusonga.

MAMBO YANABADILIKA
Mishe za mtaani zikaanza kua ngumu gari ya kutembelea nikaifanya Tax dereva kawa kwikwi nikawa naendesha mwenyewe Mambo yakazidi kua tyiti tairi zinakwisha, service inahitajika na trafiki wananikamata daily utazania wanatumwa kwangu tu

Udalali ukawa mgumu na mambo yakawa mazito basi nikawaza kufanya biashara zingine angalau niokoe jahazi.

Nikauza gari baada ya kupata wazo la uvuvi nikatengeneza mitumbwi kwa kushirikiana na jamaa mwingine hapa tuliingia partnership ya biashara tugawane faida baada ya kurudisha mtaji.

PICHA INAANZA KUUNGUA.
Biashara ikawa haieleweki leo unapata faida ya laki ndani ya wiki unakuwa una hasara ya laki kadhaa imani ya kupata ikashamiri nikaanza kukopa naweka pesa kuongeza mtaji.

NAZIDI KUPOTEA
Nikaanza kukodisha mitumbwi ya mashine unalipia mashine na mtumbwi 400k kwa mwezi hapo unaweka mafuta, unanunua mitego ama ndoano + chambo kusudi kazi ianze kazi inakuwa kama ni kubahatisha leo faida laki tatu ukirudi siku ingine faida kidogo ama hasara laki 2.

MAMBO YANAHARIBIKA ZAIDI
Kazi za uvuvi zinahitaji ushirikina uliotukuka ni SIRI watabisha ila ndio Ukweli nikaanza kushiriki na kutoa pesa kwa wategaji waweke Mambo kwa bibi sawa. hapa Mambo yakawa yanaenda Nusu Nusu yaani ile Mungu saidia sina imani na kesho lakini unafanyaje ushaambiwa ndio lazima.ufanye kusudi ufanikiwe kama wenzio.

Bwana wewe Mambo yakazidia ugumu nikaanza kuhama mialo WAPI bila bila mikopo ikaongezeka nikashindwa kulipa mingine marafiki wakapotea kwa madeni na wengine baaada ya kubadili lifestyle kuhamia visiwani.

NASITISHA BIASHARA YA UVUVI.
nikaamua kuacha uvuvi na kupaki mitumbwi huku deni la niliofanya nae partnership bado anadai pesa yake nikimweleza hali halisi haelewi kabisa nyuma MARAFIKI nao wananidai na sioni dalili ya kuwalipa

NAAMUA KURUDI KUKAA NYUMBANI NA FAMILIA.
Hapa napata ugumu zaidi dukani kwa mwezi faida ni kama 150000 mpaka laki 2 na 30000 elfu, familia ndio tunategemea duka kwa.kila kitu kodi, chakula na mengineyo mtaji ukaanza kupungua mchana na usiku mwisho nashtuka naona pakushika tena panapotea na sijui nifanyeje?

WAY OUT.
Nimewahi kufanya utalii kwa kipindi fulani na kupata pesa nikiwa NYUMBANI nilikokulia nikiwaza KURUDI naanzaje KURUDI mtaani kwa wazazi sina connection na wadau wa hizo Mambo tena nimetoka huko mda naendaga tu kusalimia. NAANZAJE na utalii ni kazi ya msimu!

DUKA liko mbioni kufilisika kabisa mda sio mwingi tena naanzaje na kodi nayo ikiisha tena naendeleaje?

NIUZE KIWANJA?
Woga unaingia biashara mpya nitakayoanza ikibuma MWISHO utakuaje? Wife ndio atakimbia na mtoto arudi kwao! Ama atakimbia aniache na mtoto nimpeleke akakae na Babu na bibi? hapa sijui mbele itakuaje?

MARAFIKI NJE YA Tanzania!
Nilipokua nafanya utalii nilipata friends Korea, Japan na Australia ambao bado tunawasiliana naweza kwenda nchi zao nikapata hosting. Je nikifanikiwa kuuza kiwanja na kupata nauli nikaenda kutafuta maisha mbele itasaidia? Mke na mtoto nyuma Tz inakuaje ?
USHAURI wenu WAKUU,

Wanaonijua hawaamini kama kweli Mambo yote yamenipitia ndani ya mda mfupi hivi nimefikia hatua Hii sina uhakika na kesho wanahisi naigiza lakini ndio hivyo TATIZO bado niko very positive na sijaonyesha kukataa tamaa jumapili nilikutana na mtu . mwenye shida nikamsaidia Asee Wife alinishangaa sana na kuona nimepagawa baada ya kutoa kiasi cha pesa kwa muitaji wakati NYUMBANI hakuna pesa yeyote ya dharura wala msalia mtume.

maisha mtihani ila mimi ni kama napitia MAGAZIJUTO NIKISONGA MBELE NAKOSEA KIDOGO TU NARUDISHWA NYUMA KABISA.

USHAURI NA Uzoefu wenu ni muhimu sana pia msisahau na sala zenu kwani yeye muweza mwenye nguvu hajawahi shindwa na gumu lolote.MAWAZO mengi niliyonayo kama mbadala naona yananichanganya zaidi na siyaelewi kabisa kwani naona kama nikurudi Utoto
Ushauri.. usiende kwa mganga tena
 
Mtoa mada cheki huu uzi hapa chini unaweza angalau kukutia moyo na ukajua unayoyapitia hauko peke yako mkuu.

Ni uzi poa sana.

 
Uvuvi ulikuwa unafanyia sehemu gani?
Kama bado una engine za mitumbwi uwezi kulala njaa kwa Dar unaweza ukawa unaikodisha kwa siku sh 15000.

Pia kama una mitumbwi mingi ya mbao iuze baki na mashine kisha nenda Pangani ukawekeze kwa kununua fiber boat hata ya million 7. Engine utafunga ulizonazo.

Pangani utafanya biashara ya kubeba watalii boti zipo chache sana. Ukiwa na fiber utakodishwa kwenda Zanzibar na kwa mtalii 1 bei ni dolla 25.

Ukiwa pale pale Pangani utabeba watalii wa ndani na nje kuwapeleka Mauya kucheki mamba na wengine kuwazungusha baharini.
 
Kumiliki BMW mpaka bodaboda ni kweli? Au ndo ngano za kiswahili.
Ah..unashangaa ki BMW? nina jamaa yangu ilikuwa anaishi kigamboni mjengo wa maana ana malori ya mchanga saa hz dereva Dangote ninachomkubali tu yule mwamba huwa havurugwi anajua sana kujiposition na kwa spidi yake ipo siku atarudi kwenye mstari maana anapiga udereva huku anafanya biashara japo mtaji si mkubwa ila ile spirit yake inambeba halikatagi tamaa lile jamaa sijui limeumbwaje!
 
Wengi tumepitia huko ila hakuna kukata tamaa, sahivi mambo mukide mukide, amini nakuambia sasa hivi utanyanyuka
 
USIKATE TAMAA. Mweke Mungu mbele. Kaa na mkeo mweleze yote mpeane mawazo. Lakini mfanye sala na dua sana Mungu atafungua tu njia. Hao marafiki zako uliowapata kwenye utalii waambie unataka kuanza biashara ya kuwauzia vitu vidogo vidogo ambavyo watalii wanapenda- batiki, vinyago, n.k. Wakutumie hela uwapelekee. Unaweza kushangaa ukianza na ka mtaji ka laki moja "UTATOKA" Kikubwa USIKATE TAMAA na mwamini Mungu
 
Kwanza pole ndugu yangu, pili hayo unayoyapitia nami yananikuta vivyo hivyo toka kumiliki gari hadi kumiliki sendos 2.

Kwanza nakushauri ni kaa chini na shem (hawa ndiyo wa kwanza kujenga / kuharibu) mpe ukweli mshauriane muanze upyaaaaaaaaa. Hapa utapata pa kuanzia.
Usiuze kiwanja bro kamwe ni heri ugange njaa ipo siku yatarudi tu.
Anza mitikas km unaanza upya kabisa,yaani vuruga kila kitu (hapa madeni kuwa km hauna hali ngumu kila mtu anajua) hawa wa maden usihangaike nao labda yale ya assets.
Komaa na bihashara na lengo moja hakika utasimama tena.
Usisahau kumuomba sana Mungu bro.
Pia jipe Moyo Hauko Pekee Ako unaepita hali hiyo.

Watu tumemiliki bmw x3 leo hii dereva boda boda nayo naunga unga.
Ni kama vile uko ndotoni kuna mda nawaza ivi Mimi ndie yule kevi niliekuwa nauwezo wa kutumia laki kwa siku. leo Hii nikitumia elfu 5 najitafakari.
 
Kweli maisha ni fumbo la imani yakigeuka mpaka mwenyeWe unajishangaa Mimi mapito yangu nimeandika kwa ufupi sana kuna mengi sana ndani yake nimepitia starehe nikiwa na miaka 16-19 nakaa na watalii kutembelea maeneo ya utamaduni mbuga za wanyama na Bata tu asubuhi mpaka asubuhi. iyo ikapitaga baada ya kufeli kupata visa ya USA nikaona bora nikasome zangu chuo nikaacha utalii.

nkafunguaga asasi nikaachana nayo baada ya kufanya registration nikafanya airbnb nikatulia nikapiga day worker kama sales nyota ikangaa nikanunua vitu vitu budget ya home kwa siku ikawa ni 35k extended family. Mambo yakawa hot....nikapiga mazao....Ukiwa na pesa unaweza kufanya vitu..vingi.sana au niseme unaweza kufanya chochote kila muda naamini.utajiri ni SIRI iko siku pesa zitanirudia tena kwa kasi sitoziruhusu ziiondoke tena
Haupo peke yako mkuu mimi nimekuja hadi kuomba msaada wa laptop humu wakati zamani nilikua na uwezo wa kununua hata laptop 10 kwa mara moja,kuhusu gari hapo ndii usiseme...kubali matokeo kwani hapo sio kituo hilo ni tukio tu.

Kwenye universal laws naona kosa jingine umelifanya siku ya jumapili umevunja sheria inautwa THE LAW OF CORRESPONDANCE (sheria ya usawa& ulinganifu). Amini Dunia yetu ya nnje ni matokeo ya Dunia yetu ya ndani.kitu kikubwa kinaundwa na vitu vidogo vidogo.

Show gratitude for what you have,shukuru kwa kile ulicho nacho kwani usiposhukuru ulimwengu utakunyang'anya usicho kithamini..Jumapili umeshindwa kukithamini kile kidogo ulicho nacho ukaamua kukitoa chote manaake hujaweka usawa..hakikisha unavyosaidia kuna kitu kitu unabaki nacho.

Mimi nilipoteza marafiki,mpenzi,majirani mpaka baadhi ya ndugu nilikata tamaa nikatamani kujiua si unajua sisi wahehe tena,badae nilivyogundua sina nilichopungukiwa mwilini nipo safi nikajiona fala nikawa tayari kufanya kazi yoyote bila kijari elimu wala nafasi nillikuwa nayo hapo nyuma..Mungu si athumani bado yupo pamoja nami.

a moja,gari ya kutembelea,navyosema gari sio vits,paso,duet,starlet..hakuna maisha matamu kama opportunity inakuja kukiwa na preparation.

Nikukumbushe tu kwamba hakuna ulichopoteza ila umejifunza
 
Maisha haya acheni,kama mm ups and down za kutosha,madeni ndio usiseme ila kukopa kwangu ni katika harakati za kutaka kujiinua tena na nina amini nikiinuka sitarudi chini Inshaallah,ila ndg ukiwaamini na kiwakabidhi biashara kukuangusha ni faster
 
Kama ukiangalia vizuri..kosa lilianzia kwenye kuoa...!!

Kama walau ungesubiri kidogo naamini ungkuwa mbali

Vijana tukianza kufanikiwa mengi huja kichwan....!!lakini hasa huja la kukaa na mwanamke ndan...!!sio ubaguzi....lkn inashauriwa pale kabla ya kuoa hakikisha umepata chanzo cha kudumu cha pesa na pia makazi ya kudumu

Lakn pia tusiharakishe mambo kwa haraka bali kaa na mtu ukimsoma na mkipanga maisha.

Tengenezeni maisha yenu pamoja....andaeni future ynu na watoto kisha mambo mengne yafuate

Ila pia angalia na aina ya mwanamke....!!ukikosea tu mke....ndugu utauza ufuta mpk popo wtakucheka
 
Back
Top Bottom