Wakuu ushauri wenu ni muhimu, nimefilisika

Wakuu ushauri wenu ni muhimu, nimefilisika

Kwanza pole ndugu yangu, pili hayo unayoyapitia nami yananikuta vivyo hivyo toka kumiliki gari hadi kumiliki sendos 2.

Kwanza nakushauri ni kaa chini na shem (hawa ndiyo wa kwanza kujenga / kuharibu) mpe ukweli mshauriane muanze upyaaaaaaaaa. Hapa utapata pa kuanzia.
Usiuze kiwanja bro kamwe ni heri ugange njaa ipo siku yatarudi tu.
Anza mitikas km unaanza upya kabisa,yaani vuruga kila kitu (hapa madeni kuwa km hauna hali ngumu kila mtu anajua) hawa wa maden usihangaike nao labda yale ya assets.
Komaa na bihashara na lengo moja hakika utasimama tena.
Usisahau kumuomba sana Mungu bro.
Pia jipe Moyo Hauko Pekee Ako unaepita hali hiyo.

Watu tumemiliki bmw x3 leo hii dereva boda boda nayo naunga unga.
[emoji122]
 
Kwanza pole ndugu yangu, pili hayo unayoyapitia nami yananikuta vivyo hivyo toka kumiliki gari hadi kumiliki sendos 2.

Kwanza nakushauri ni kaa chini na shem (hawa ndiyo wa kwanza kujenga / kuharibu) mpe ukweli mshauriane muanze upyaaaaaaaaa. Hapa utapata pa kuanzia.
Usiuze kiwanja bro kamwe ni heri ugange njaa ipo siku yatarudi tu.
Anza mitikas km unaanza upya kabisa,yaani vuruga kila kitu (hapa madeni kuwa km hauna hali ngumu kila mtu anajua) hawa wa maden usihangaike nao labda yale ya assets.
Komaa na bihashara na lengo moja hakika utasimama tena.
Usisahau kumuomba sana Mungu bro.
Pia jipe Moyo Hauko Pekee Ako unaepita hali hiyo.

Watu tumemiliki bmw x3 leo hii dereva boda boda nayo naunga unga.

Mkuu na wewe chanzo ni kumiliki gari tu ndio mwanzo wa kuanguka?
 
Kwanza nianze kwa kumshukuru muumba wa mbingu na nchi kwa kuzidi kutupa afya makini sote kwa mapenzi yake.

Naamini siku zote Mungu hatupi tunachotaka bali unachostahili nimekulia maisha ya kijijini yenye uchumi wa kati yaani Nusu shibe robo mlo mmoja kwa miaka mingi takribani 16ya kuzaliwa.

Nimepitia vingi japo nimeishi kidogo sana uhalisia wa shida na hustles za kibabe sijapita sana zile za kutisha ama kupambana Nusu roho kutaka tengana na mwili ni ups and Downs za kidunia Tu ndio nimepitia zaidi

Nisijielezee sana nachoomba apa zaidi ni Ushauri kwa sasa ndio naingia 30 kwenye maisha yangu sina mengi ya kujutia zaidi ya kushukuru kwa Neema chache nilizopatia na kulaumu ndugu kwa kutamani umasikini.uwe na mimi.

Baada ya shule niliendelea na hustles za mtaani mdogo mdogo hatimaye nikaanza kujikimu na vijisenti vidogo kusaidia ndugu wenye uhitaji Simu zilikua hazikauki nikaendelea kupambana miaka ikasogea nikawa dalali wa viwanja na mashamba namimi nikaweza bahatika kumiliki kiwanja mjini.

Mambo yakaendelea nikanunua kagari kadogo kakutembelea nikaona umri usinibane nikamwita mwenzangu kuishi pamoja nikafanya Mambo ya mahari na miamala mingine ya kiutamaduni basi siku zikasogea.

Mungu akajalia familia ikakua tukapata na mtoto wa kiume nikafungua na kaduka mke akawa anauza siku zikazidi kusonga.

MAMBO YANABADILIKA
Mishe za mtaani zikaanza kua ngumu gari ya kutembelea nikaifanya Tax dereva kawa kwikwi nikawa naendesha mwenyewe Mambo yakazidi kua tyiti tairi zinakwisha, service inahitajika na trafiki wananikamata daily utazania wanatumwa kwangu tu

Udalali ukawa mgumu na mambo yakawa mazito basi nikawaza kufanya biashara zingine angalau niokoe jahazi.

Nikauza gari baada ya kupata wazo la uvuvi nikatengeneza mitumbwi kwa kushirikiana na jamaa mwingine hapa tuliingia partnership ya biashara tugawane faida baada ya kurudisha mtaji.

PICHA INAANZA KUUNGUA.
Biashara ikawa haieleweki leo unapata faida ya laki ndani ya wiki unakuwa una hasara ya laki kadhaa imani ya kupata ikashamiri nikaanza kukopa naweka pesa kuongeza mtaji.

NAZIDI KUPOTEA
Nikaanza kukodisha mitumbwi ya mashine unalipia mashine na mtumbwi 400k kwa mwezi hapo unaweka mafuta, unanunua mitego ama ndoano + chambo kusudi kazi ianze kazi inakuwa kama ni kubahatisha leo faida laki tatu ukirudi siku ingine faida kidogo ama hasara laki 2.

MAMBO YANAHARIBIKA ZAIDI
Kazi za uvuvi zinahitaji ushirikina uliotukuka ni SIRI watabisha ila ndio Ukweli nikaanza kushiriki na kutoa pesa kwa wategaji waweke Mambo kwa bibi sawa. hapa Mambo yakawa yanaenda Nusu Nusu yaani ile Mungu saidia sina imani na kesho lakini unafanyaje ushaambiwa ndio lazima.ufanye kusudi ufanikiwe kama wenzio.

Bwana wewe Mambo yakazidia ugumu nikaanza kuhama mialo WAPI bila bila mikopo ikaongezeka nikashindwa kulipa mingine marafiki wakapotea kwa madeni na wengine baaada ya kubadili lifestyle kuhamia visiwani.

NASITISHA BIASHARA YA UVUVI.
nikaamua kuacha uvuvi na kupaki mitumbwi huku deni la niliofanya nae partnership bado anadai pesa yake nikimweleza hali halisi haelewi kabisa nyuma MARAFIKI nao wananidai na sioni dalili ya kuwalipa

NAAMUA KURUDI KUKAA NYUMBANI NA FAMILIA.
Hapa napata ugumu zaidi dukani kwa mwezi faida ni kama 150000 mpaka laki 2 na 30000 elfu, familia ndio tunategemea duka kwa.kila kitu kodi, chakula na mengineyo mtaji ukaanza kupungua mchana na usiku mwisho nashtuka naona pakushika tena panapotea na sijui nifanyeje?

WAY OUT.
Nimewahi kufanya utalii kwa kipindi fulani na kupata pesa nikiwa NYUMBANI nilikokulia nikiwaza KURUDI naanzaje KURUDI mtaani kwa wazazi sina connection na wadau wa hizo Mambo tena nimetoka huko mda naendaga tu kusalimia. NAANZAJE na utalii ni kazi ya msimu!

DUKA liko mbioni kufilisika kabisa mda sio mwingi tena naanzaje na kodi nayo ikiisha tena naendeleaje?

NIUZE KIWANJA?
Woga unaingia biashara mpya nitakayoanza ikibuma MWISHO utakuaje? Wife ndio atakimbia na mtoto arudi kwao! Ama atakimbia aniache na mtoto nimpeleke akakae na Babu na bibi? hapa sijui mbele itakuaje?

MARAFIKI NJE YA Tanzania!
Nilipokua nafanya utalii nilipata friends Korea, Japan na Australia ambao bado tunawasiliana naweza kwenda nchi zao nikapata hosting. Je nikifanikiwa kuuza kiwanja na kupata nauli nikaenda kutafuta maisha mbele itasaidia? Mke na mtoto nyuma Tz inakuaje ?
USHAURI wenu WAKUU,

Wanaonijua hawaamini kama kweli Mambo yote yamenipitia ndani ya mda mfupi hivi nimefikia hatua Hii sina uhakika na kesho wanahisi naigiza lakini ndio hivyo TATIZO bado niko very positive na sijaonyesha kukataa tamaa jumapili nilikutana na mtu . mwenye shida nikamsaidia Asee Wife alinishangaa sana na kuona nimepagawa baada ya kutoa kiasi cha pesa kwa muitaji wakati NYUMBANI hakuna pesa yeyote ya dharura wala msalia mtume.

maisha mtihani ila mimi ni kama napitia MAGAZIJUTO NIKISONGA MBELE NAKOSEA KIDOGO TU NARUDISHWA NYUMA KABISA.

USHAURI NA Uzoefu wenu ni muhimu sana pia msisahau na sala zenu kwani yeye muweza mwenye nguvu hajawahi shindwa na gumu lolote.MAWAZO mengi niliyonayo kama mbadala naona yananichanganya zaidi na siyaelewi kabisa kwani naona kama nikurudi Utoto
Awali ya yote, naomba nikupe pole mkuu kwa hayo unayoyapitia!

Ila ninafurahi kuona still you're strong, hakika ni watu wachache sana, wanaoweza kuendelea kuwa +ve kwenye viatu vyako!

Ushauri wangu:
Hapo ulipo, naona best alternatives zote unazo! But unatakiwa UTULIZE TU AKILI....for sure utatoka hapo ulipo, kama matani vile!

All the best chief.
 
Ndugu yangu pole sana brother,
Kaka wewe bado ni tajiri kwa nn unakata tamaa?
Angalia ulipojikwaa usiangalieulikoangukia
Wapo wengi huangushwa na Mungu kisha huinuliwa upya na kuvikwa uimara dhabiti
Kaka angalia sababu za kufikia hapo kisha jipange upya

Ibada+bidii=mafanikio

Nakutakia kila la kheri
 
1570610051434.png

Kumiliki BMW mpaka bodaboda ni kweli? Au ndo ngano za kiswahili.

imebidi nijaribu kuitafuta angalau inayofanana.
mkuu inawezekana kabisa unaamua kuuza ili uongeze mtaji katika biashara na ghafla inakata unafanyaje? naelewa watu wengi waliokuwa na mawe na wakaanguka
 
hongera sana kwa kujianika hapa!
uzi umetufaa wengi tulioandika na wasioandika na wapo wengine watasimama tena kwa ajiri ya uzi huu hongera sana kwa kupata kibali na kujifunua na pia wadau walioweza kutoa ushauri mbalimbali katika uzi huu.
nafikiri uliona kuwa huna shati lakini wadau wamekuonyesha shati umevaa ila hujachomekea tu!
sasa na mimi nianze kukushauri kwa kadri ninachofikiri naweza.
  1. kwanza usikate tamaa yupo mzee alipata utajiri akiwa na umri wa miaka 75 na mpka sasa bado yupo na akaoa mke mwingine anakula hela yake umri huo alikuwa nao mwaka 2004 sasa unaweza kuona ana umri gani 30 kitu gani kwako?
  2. wengi tutakuelekeza jinsi ya kusimama lakini leo tubadili tukuelekeze kwanza wapi ulianguka ili usianguke tena
    1. matumizi yako yalikuwaje? kama yaliongezeka kuliko kipato lazima uanguke kipindi cha selikali hii purchasing power kwa watu wengi imepungua kiasi kuwa watu wengi wamekuwa wanunuzi wa vitu muhimu na ziada wananunua kwa kiasi kidogo pale inapobidi sasa kama unafanya biashara ya vitu visivyo vya lazima lazima mauzo yashuke lakini wakati huo huo mke anakwambia hataki kusikia umewatoa watoto English medium school kwa hiyo lazima ule mtaji.
    2. shughuli za udalali zinaendana na dili kiasi kwamba kwa kipindi hiki zimebaki chache na udalali huwa wanamatumizi makubwa sijui kwanini sasa zikikata lazima ziyumbe. lakini pia kwa kazi hiyo hiyo inawezekana mliwadhurumu watu wakaweka kinyongo kwa njia moja au nyingine nafsi zinazolalamika huaribu mafanikio kwa njia moja au nyingine.
    3. uchaguzi mbovu wa biashara ni chanzo pia cha kutofanikiwa. yako mambo mengi lakini yakuzingatia lakini vifuatavyo vinaweza kuwa msaada kwako
      1. ujuzi na maarifa pia muda wa kufanya shughuli uliyoichagua kuna uwezekano haukuwa na maarifa ya kutosha na muda wa kutosha kuifanya biashara uliyoichagua hivyo kukufanya kuiendesha kwa gharama kubwa sana kuliko mapato
      2. soko la bidhaa ulizokuwa unauza lilikuwaje na hapa unaangali uhitaji wa bidhaa na wauzaji wengine ukoje na wauzaji wengine wanakuzidi nini na wewe unawazidi nini na unabadilikaje kurikabili soko
      3. upatikanaji wa faida ukoje? si swala la kununua bidhaa 900/- na kuuza 1200/- je gharama gani zinaendana na uendeshaji wa biashara wengi hawahesabu gharama za mafuta ya gari chakula mchana na vocha za simu kama zinahusu biashara.
      4. mtaji uliwekaje? kuwa na mtaji mkubwa au mdogo husababisha pia kuanguka kwa biashara mfano wafanyakazi wengi wakianzisha biashara wanaweza wasione faida au hasara kwa kuwa huwa wanajikuta wanashindwa kutenganisha fedha binafsi na za biashara. pia wengine wanashindwa kutenga au kujua mtaji unaohitajika katika uendeshaji na vifaa vya kudumu over investment ni shiiida kwa biashara.
      5. kiasi gani ulipanga biashara igharamie mahitaji ya familia yako
    4. baada ya kuona vigezo vya kuchagua la msingi sasa lazima tuangalie jinsi ya mpangilio sikawa shughuli zote lazima kujua zipi ni za mwanzo kabla ya kuanza biashara na pia kuanzia ununuaji/uzalishaji mpaka uuzaji kipi kinaanza na kitahitaji kiasi gani cha fedha
    5. usimamizi ni muhimu ulismamiaje biashara yako na wengi tunakwama hapa
      1. usimamizi wa fedha za mauzo - mfano ukiwa na duka au daladala familia ikihitaji fedha ya dharura kwa haraka tegemea wewe kuhusika sasa je ukishatoa unarudisha?
      2. usimamizi wa mikopo
        1. mikopo ya bidhaa
          1. mikopo kwa wateja; hatuwezi kuuza bila kukopesha lakini tuelewe kwamba tunapokopesha tunawagharamia wateja na tusipokuwa makini tunapunguza mtaji wa kujiendesha bila kujua sasa je tumeweka kiwango cha mwisho cha kukopesha wateja? hivyo mikopo huangusha biashara.
          2. mikopo kwa waleta bidhaa hii inahitajika lakini wakati mwingine inaweza kusababisha ufuatiliaje mbovu kwa madeni ya wateja pia utumiaji mbovu wa bidhaa ghafi. pia malipo kwa wanaoleta bidhaa ni muhimu wakalipwa kwa makubaliano ili waendelee kuleta bidhaa.
        2. mikopo ya fedha kwenye taasisi za fedha na mikopo gharama zilikuwaje za mikopo kuna uwezekano riba zikasababisha kuanguka kwa biashara madeni yakizidi husababisha biashara kuanguka
      3. jinsi gani ulijipanga kwa dharura zisizo tarajiwa risk management hii ni shiiiida mfano kwa wale wanaofanya biashara ya kukopesha vijijini wameathirika kwa kiasi fulani na fedha za Magufuli huko kijijini
yapo mengi lakini kwa kuanzia hiki kinaweza kukusaidia baadaye nitakuja na success story nini kipo katika game.
 
Hapo kwenye madeni pananihusu sana, Niko kwenye sama situation nanahisi safe plan kwasasa nikutoyalipa ila napata stress sna kufikiria jamaa watanielewaje
Mimi mbinu niliyotumia ni hii.
Taasisi zinazonidai hizo nakomaa nalipa zote bila kukopa tena yaani kama ni CRDB au Brac nikulipa na kufuta deni kabisa.
Haya madeni ya washkaji, yaani ya boss niazime 500,000 kesho narudisha, hizo kiukweli nimejumlisha maden ya wana yote nimejua nadaiwa sh kadhaa, nimewaweka jamaa pending tena kwa kuwaambia ukweli (samahani kaka sitaweza kukulipa sasa hadi wakati nikikaa poa hata kwa riba).
Aelewe asielewe nitakuja walipa kwasasa nakomaa kusimama
 
Mkuu pole sana.. Nilikuwa nahisi mimi pekee ndo muhanga wa kutoka class ya juu kwenda chini ila kupitia story yako nimejiona nipo kwenye right track.
Bro yaani mimi kwasasa nimejipa moyo tu. Nilikata tamaa sana hadi sumu nimekunywa, lakini kwasasa tuambiane tu ukweli si pekee etu tupo wengi hivyo tujikaze.
Then watu wanafikiri kufilisika ni jambo gumu sana.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Hawajui inaweza ikawa ni dakika tu.
 
Mkuu kubali hali iliyopo, sahau ulichokuwa nacho anza upya. Kama Kuna fursa ya kufanya na inahitaji mtaji usisite kuuza hicho kiwanja kwani Kila kitu tulicho nacho tuko nacho kwa sababu tulikitafuta palipokuwepo na fursa, suala la mambo kwenda kombo wala siyo mkosi, maana wakati tunakuwa nacho Kuna wengine wanakuwa hawana hivyo ni hali ya mzunguko wa Maisha. Tujifunze kushughuri kwa Kila Khali.
 
Daah maisha weeee, haya in mapito tu na tumepitia wengi, utavuka
 
Hii awamu waliokuwa wanaishi kwa dili (kama madalali) wanaisoma namba sana. Kwa ufupi hauko peke yako anguko hili ni kwa wengi kama walivyoeleza waliotangulia ni kwamba kwa jinsi hali ya Maisha ilivyo ngumu watu wamepunguza sana matumizi yasiyo ya lazima na pesa imekuwa ngumu sana. Siku hizi mahoteli hayana wateja wazinzi na wasafiri wamebadilisha sehemu za kulala wanalala kwa ndugu zao na wazinzi wamewarudia wake zao. Vituo vya mafuta haviuzi, Maduka ya nguo hayauzi, vyakula vya anasa watu hawala, baa zimepunguza mauzo, taxi hamna abiria, yaani kila kona watu wanalia maumivu hauko peke yako mzee baba. Kila mtu kachoka kwa namna yake
 
Kwanza nianze kwa kumshukuru muumba wa mbingu na nchi kwa kuzidi kutupa afya makini sote kwa mapenzi yake.

Naamini siku zote Mungu hatupi tunachotaka bali unachostahili nimekulia maisha ya kijijini yenye uchumi wa kati yaani Nusu shibe robo mlo mmoja kwa miaka mingi takribani 16ya kuzaliwa.

Nimepitia vingi japo nimeishi kidogo sana uhalisia wa shida na hustles za kibabe sijapita sana zile za kutisha ama kupambana Nusu roho kutaka tengana na mwili ni ups and Downs za kidunia Tu ndio nimepitia zaidi

Nisijielezee sana nachoomba apa zaidi ni Ushauri kwa sasa ndio naingia 30 kwenye maisha yangu sina mengi ya kujutia zaidi ya kushukuru kwa Neema chache nilizopatia na kulaumu ndugu kwa kutamani umasikini.uwe na mimi.

Baada ya shule niliendelea na hustles za mtaani mdogo mdogo hatimaye nikaanza kujikimu na vijisenti vidogo kusaidia ndugu wenye uhitaji Simu zilikua hazikauki nikaendelea kupambana miaka ikasogea nikawa dalali wa viwanja na mashamba namimi nikaweza bahatika kumiliki kiwanja mjini.

Mambo yakaendelea nikanunua kagari kadogo kakutembelea nikaona umri usinibane nikamwita mwenzangu kuishi pamoja nikafanya Mambo ya mahari na miamala mingine ya kiutamaduni basi siku zikasogea.

Mungu akajalia familia ikakua tukapata na mtoto wa kiume nikafungua na kaduka mke akawa anauza siku zikazidi kusonga.

MAMBO YANABADILIKA
Mishe za mtaani zikaanza kua ngumu gari ya kutembelea nikaifanya Tax dereva kawa kwikwi nikawa naendesha mwenyewe Mambo yakazidi kua tyiti tairi zinakwisha, service inahitajika na trafiki wananikamata daily utazania wanatumwa kwangu tu

Udalali ukawa mgumu na mambo yakawa mazito basi nikawaza kufanya biashara zingine angalau niokoe jahazi.

Nikauza gari baada ya kupata wazo la uvuvi nikatengeneza mitumbwi kwa kushirikiana na jamaa mwingine hapa tuliingia partnership ya biashara tugawane faida baada ya kurudisha mtaji.

PICHA INAANZA KUUNGUA.
Biashara ikawa haieleweki leo unapata faida ya laki ndani ya wiki unakuwa una hasara ya laki kadhaa imani ya kupata ikashamiri nikaanza kukopa naweka pesa kuongeza mtaji.

NAZIDI KUPOTEA
Nikaanza kukodisha mitumbwi ya mashine unalipia mashine na mtumbwi 400k kwa mwezi hapo unaweka mafuta, unanunua mitego ama ndoano + chambo kusudi kazi ianze kazi inakuwa kama ni kubahatisha leo faida laki tatu ukirudi siku ingine faida kidogo ama hasara laki 2.

MAMBO YANAHARIBIKA ZAIDI
Kazi za uvuvi zinahitaji ushirikina uliotukuka ni SIRI watabisha ila ndio Ukweli nikaanza kushiriki na kutoa pesa kwa wategaji waweke Mambo kwa bibi sawa. hapa Mambo yakawa yanaenda Nusu Nusu yaani ile Mungu saidia sina imani na kesho lakini unafanyaje ushaambiwa ndio lazima.ufanye kusudi ufanikiwe kama wenzio.

Bwana wewe Mambo yakazidia ugumu nikaanza kuhama mialo WAPI bila bila mikopo ikaongezeka nikashindwa kulipa mingine marafiki wakapotea kwa madeni na wengine baaada ya kubadili lifestyle kuhamia visiwani.

NASITISHA BIASHARA YA UVUVI.
nikaamua kuacha uvuvi na kupaki mitumbwi huku deni la niliofanya nae partnership bado anadai pesa yake nikimweleza hali halisi haelewi kabisa nyuma MARAFIKI nao wananidai na sioni dalili ya kuwalipa

NAAMUA KURUDI KUKAA NYUMBANI NA FAMILIA.
Hapa napata ugumu zaidi dukani kwa mwezi faida ni kama 150000 mpaka laki 2 na 30000 elfu, familia ndio tunategemea duka kwa.kila kitu kodi, chakula na mengineyo mtaji ukaanza kupungua mchana na usiku mwisho nashtuka naona pakushika tena panapotea na sijui nifanyeje?

WAY OUT.
Nimewahi kufanya utalii kwa kipindi fulani na kupata pesa nikiwa NYUMBANI nilikokulia nikiwaza KURUDI naanzaje KURUDI mtaani kwa wazazi sina connection na wadau wa hizo Mambo tena nimetoka huko mda naendaga tu kusalimia. NAANZAJE na utalii ni kazi ya msimu!

DUKA liko mbioni kufilisika kabisa mda sio mwingi tena naanzaje na kodi nayo ikiisha tena naendeleaje?

NIUZE KIWANJA?
Woga unaingia biashara mpya nitakayoanza ikibuma MWISHO utakuaje? Wife ndio atakimbia na mtoto arudi kwao! Ama atakimbia aniache na mtoto nimpeleke akakae na Babu na bibi? hapa sijui mbele itakuaje?

MARAFIKI NJE YA Tanzania!
Nilipokua nafanya utalii nilipata friends Korea, Japan na Australia ambao bado tunawasiliana naweza kwenda nchi zao nikapata hosting. Je nikifanikiwa kuuza kiwanja na kupata nauli nikaenda kutafuta maisha mbele itasaidia? Mke na mtoto nyuma Tz inakuaje ?
USHAURI wenu WAKUU,

Wanaonijua hawaamini kama kweli Mambo yote yamenipitia ndani ya mda mfupi hivi nimefikia hatua Hii sina uhakika na kesho wanahisi naigiza lakini ndio hivyo TATIZO bado niko very positive na sijaonyesha kukataa tamaa jumapili nilikutana na mtu . mwenye shida nikamsaidia Asee Wife alinishangaa sana na kuona nimepagawa baada ya kutoa kiasi cha pesa kwa muitaji wakati NYUMBANI hakuna pesa yeyote ya dharura wala msalia mtume.

maisha mtihani ila mimi ni kama napitia MAGAZIJUTO NIKISONGA MBELE NAKOSEA KIDOGO TU NARUDISHWA NYUMA KABISA.

USHAURI NA Uzoefu wenu ni muhimu sana pia msisahau na sala zenu kwani yeye muweza mwenye nguvu hajawahi shindwa na gumu lolote.MAWAZO mengi niliyonayo kama mbadala naona yananichanganya zaidi na siyaelewi kabisa kwani naona kama nikurudi Utoto
Tatizo la waafrica wanakata tamaa haraka sana miaka 30 tuu umejikatia tamaa,,anzia ulipo songa mbele mtegemee mungu achana na waganga njaa hao ndo chanzo cha wewe kurudi nyuma.never giver up man.
 
Bro yaani mimi kwasasa nimejipa moyo tu. Nilikata tamaa sana hadi sumu nimekunywa, lakini kwasasa tuambiane tu ukweli si pekee etu tupo wengi hivyo tujikaze.
Then watu wanafikiri kufilisika ni jambo gumu sana.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Hawajui inaweza ikawa ni dakika tu.
Yaan kunawakat naona nikama maisha yananilazimisha nitembee juu ya maji bila kuzama
 
Duh mkuu uko na shida kichwani, umaskini ndiyo mawazo yako ukiamka mchana hadi usiku yaani unauishi na kuutukuza, ukimbie umaskini kama ukoma.
Ushauri be honest print haya maelezo yako kama yalivyo nenda nayo kwa mtaalamu wa saikolojia muulize huyu mtu ana shida gani??[emoji169]
Mtaalam wa Saikolojia mwenyewe anategemea hela za wenye msongo wa mawazo ndo aishi.
 
Back
Top Bottom