Tetesi: Wakuu wa mikoa, wakurugenzi na viongozi mbalimbali wa serikali wahoji kurudisha posho za Mwenge

Wanajua mpango Wa Rais kubana matumiz hiyo kusudi rudisha tuuuu eeee maaana hamna namna
 

Unayosema yawezekana ni kweli lakini aliyewateua ndio kasema mrudushe, na tatizo la hawa wateule sijui kama wewe ni miongoni mwao kama sio samahani, huwa ni waoga kusema ukweli au kumwambia mkuu kuwa hivyo sivyo, sasa haisaidii kulalama mitandaoni, mmetumia au lah, kasma imepitishwa na bunge au lah mkubwa kasema rudisheni, La sivyo msirudishe atengue uteuzi iwe aibu kwenu au mrudishe na mjiuzulu ili mkuu atambue kuwa mmechukia na mtaonekana mashujaa. Kwani matumizi yakigeuzwa kutoka posho kwenda maendeleo kuna kosa gani almradi ijulikane imeenda kufanya shughuli gani ya maendeleo.
Poleni kama mlifikiri mlipoteuliwa mnaenda kutunisha matumbo mtaambulia magonjwa ya moyo na stress kibao kwa kutojua kesho kutaamkaje.
 
Lete source


Hivi Makonda aliposema kuna mawaziri wanaomuuliza anatafuta nini, je alitoa chanzo cha taarifa alizoletewa?
Serikali ilitakiwa itangaze kabla kwamba hakutakuwapo na watu kutoka nje ya mkoa wakati wa kuzima mwenge maana walishazoeshwa kufanya hivyo, ndio maana wapinzani walikuwa wanashauri mwenge ukakae mlima kilimanjaro au ufutwe
 
Wanatakiwa wajitokeze hadharani sio kulalamika kwa kujifichaficha.
 
Watafute tafsiri sahihi ya "kuisoma namba"ndipo kama yafaa waanze kulalama !
 
kweli kabisa wanapaswa walalamike....Haya maamuzi ya kurudisha yangetakiwa kufanya mapema kabla hawajapewa pesa..
 
Hakuna busara katika kurudisha fedha ambazo zimeshaanzatumika...Ukizingatia kuwa wengine tayari walishafika kwenye eneo la tukio..

Nadhani busara ya kawida ni kuacha kukurupuka...
Hii inaonesha kabisa kuwa kuna one man show... Na ni utaratibu mbaya sana tunaweza kujikuta tunarudi miaka 50 nyuma...
 
Ngoja watifuane na watafunane walimpenda wenyewe Nduli IDD Amini


kwa hakika hapa mkuu anatakiwa afikirie kwanza mawazo mengine...la sivyo atatafuta mgomo baridi bure...hakuna kitu kibaya kiongozi kufanya kazi na watu wako wa chini wasiporidhishwa na wewe.. wanafanya ilimradi siku ziende uondoke madarakani
 
Hivi kuzima tu mwenge kuna bajeti yake na kubwa hivyo!
 
Kwani kurudisha lazima ambaye hataki aache hapo atamjua Mh.John magufuli ni nani
 
Hivi kuzima tu mwenge kuna bajeti yake na kubwa hivyo!
Kumbe ulikuwa hujui kuuzima mwenge ni gharama zaidi ya kuzima moto unaowaka kwenye ghorofa la kitega uchumi?Na ulikuwa hujui kwa nini wale wapinzani wa chama tawala walikuwa ant-mwenge?[emoji2] Kuuzima mwenge ni zaidi ya kuzima jengo lililopigwa bomu shauri yako.
 
kwa hakika hapa mkuu anatakiwa afikirie kwanza mawazo mengine...la sivyo atatafuta mgomo baridi bure...hakuna kitu kibaya kiongozi kufanya kazi na watu wako wa chini wasiporidhishwa na wewe.. wanafanya ilimradi siku ziende uondoke madarakani
Atakayebainika atakula ban.
 
Si mumwambie ukwl boss wenu kama anawaonea? Hachen kulalamika kama hachieni vyeo tunajua nyie no makada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…