Walaka wa I Kwa Wajasiriamali wote/Wafanya biashara/Wajasirimali watarajiwa

Walaka wa I Kwa Wajasiriamali wote/Wafanya biashara/Wajasirimali watarajiwa

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
Habari za Mwaka mpya wakuu,

Mwaka mpya nazani ndo umeanza wakuu na uko speed sana.

Kuna maswala ya muhimu sana ya kuyafanyia kazi kama Watanzania na kama wajasirimali.

1. ISHU YA UJASIRIMALI
Kwa kweli tuna kazi moja ngumu sana katika swala zima la ujasiriamali, tunatakiwa kukimbia wakati wenztu wanatembea wenzetu wako very far na that is why so far wanaelekea kututawala, Ishu ya Kenya kuwa mwekezaji No mbili Tanzania si ishu ya kufurahia hata kidogo ni fedheha ya hali ya juu kabisa, kwa nini sisi tusiwe wawekezaji wakubwa Kenya?

Last year nilkuwa na safari ndefu sana huko kenya ambayo ilinichukua kwenye kufika kwenye miji mikubwa karibia yote ya kenya kama vile KISUMU, ELDORET, NAIROBI, NAIVASHA sikufika tu MOMBASA.

Katika miji hii yote na wengine walio fika huko ni mashahidi.

1. Sikuweza kuona bidhaa ya Tanzania hata moja.

2. Maduka yote yamejaa bidhaa za kenya tupu.

3. Hata pombe wanakunywa za kwao Tusker Lager kusapoti kiwanda chao,huwezi wakuta wanakunywa sijui Serengeti,

Ila kwa Tanzania ni kinyume chake hata ukienda Mtwara au Mbeya utakuta bidhaa za Kenya.

Huwezi kuta bidhaa za Tanzania hata kwenye miji inayo pakana na Tanzania, sikuwezo ona kabisa.


UFUGAJI WA KUKU KENYA.

Kenya wako mbali sana Africa mashariki na kati kwa ufugaji wa kuku na hii si kwa bahati mbaya bali jamaa wana mikakati ya hali ya juu kabisa kabisa, jamaa wamejpanga vilivyo na hawana utani kabisa, na moja ya sababu kubwa kwa nini kenya wako juu sana kwenye kuku ni kwamba.

1. Kenya wana kula sana kuku kuliko Tanzania, hii haina ubishi, wakati sisi ni nyama nyekundu Kenya wanakula sana white meet ya kuku. ukitembelea migahawa yao mingi ni kuku watu wanaagiza tofauti na Tanzania ambapo sisi kuku ni kwa bahati mbaya tu. hii ndo moja ya sababu

Na Kuku jogoo ambaye kwenye anauzwa hadi Tsh 30,000/ huku kwetu utaambiwa Tsh 15,000/

BIASHARA YA SUPERMARKET na ISHU YA NAKUMAT KUCHUKUA SHOPRITE.

Hawa jamaa ni kweli kwamba wana Malls nyingi sana na hii ni kwa sababu wana utamaduni wa kununua vitu supermarket, nui vigumu sana miji mingi ya kenya hasa mikubwa kukuta maduka ya rejareja, ni machache sana, Mji kama Kisumu unaweza zunguka mji mzima ukakutana na maduka matano tu ya bidhaa za reja reja, haza za kula tofauti na maduka ya simu na kazalika ambayo ni kama huku tu.

Hii inawapa advantage na hata NAKUMAT anavyo chukua maduka ya Shoprite si kwa bahati mbaya jamaa wana nguvu sana huko kwao na si zani kama kuna Supermarket ya kuweza kushindana nao hapa Tanzania,

UZALENDO

Jamaa nao wanatuzidi sana kwenye swala la uzalendo, wanapenda sana vitu vy nchi yao, wanapenda sana nchi yao, ni vigumu kukuta wakenya sijui wamevaa urembo una rangi za bendera za USA tofauti na sisi mtu anatundika Bendera ya USA anazani ni ujanja kumbe ni ujnga wa hali ya juu kabisa,

Hata TV huwezi wakuta sijui wanatazama TV za Bongo Na hata EATV sijui kwa nini wanaitwa hivyo make hakuna mtu anatazama hiyo TV na hata hawaijui,

NINI TUFANYE?

1. UZALENDO
Ni lazima kwanza Watanzania wawe wazalendo na vitu vyao, wajivunie vitu vyao hata kama ni vibaya kiasi gani, china alianza hivyo hivyo, tunatakiwa kupenda vya kwetu, na si kupenda vya wengine tunazani sifa wakati wao hawapendi vya kwetu.

2. UJASIRIMALI KWA UJUMLA WAKE
Tunatakiwa kufanya kazi kufa na kupona, kama wewe ni mjasirimali basi pambana kufa na kupona, Ujasirimali si lele mama, si showoff, watu wanachukulia kama sifa fulani lakini sio hivyo tunatakiwa kujitoa viulivyo ili tuweze kufanikiwa.

- TUWE WABUNIFU
Ubunifu ndo kitu kitaweza kutuokoa, ni lazima tuwe wabunifu la sivyo ni hakuna kitu, wenzetu ndo kitu kinawasaidia,

MFANO: WEWE UNAFUGA KUKU. Je ulisha jiuliza utaongezaje walaji wa Kuku ili basi upate soko? au unawaza kuuza tu?

Tuache kujikita kwenye sales pekee,sales ni ishu ya muda tu ni lazima tujikite kutengeneza soko na si kujikita kuuza tu,

3. TUACHE MANENO MENGI NA VITENDO 0
Tunapenda sana maneno, Watanzania tunafanya biashara za maneno, huku janvini kwenyewe ni mfano tosha, tuko kw amaneno tu lakini kiuharisia hakuna kitu,
Watu wanapenda kutafuta sifa za kuja kusifiwa humu kwamba sijui wanafuga kuku, Nguruwe Bata na kazaila, wakuu tupige kazi sifa hazitatusaidia

Ni lazima vitendo vifanye kazi zaidi

4. MITANDAO
Ni lazima watu wajenge mitandao ya biashara na club za ujasiriamali, huku kila mtu naona yuko kivyake vyake, ok ni sawa but huwezi furukuta mbele ya wenzako, ni lazima wabongo tujenge hiyo mitandao

Wenzetu hutumia siku za wikendi kukutana na kubadilioshanaa mawazo huku wikenda tuna ulizana tukanywe wapi au wapi tukacheki mechi.

Ni lazima watu wafahamiane wasaidiane wajenge umoja ambao unaweza kutusaidia kusongo mbele na hata kupambna na competitors kutoka nje.

Ni lazima watu sasa wajenge mitandao/club na wawe wanakutana mara kwa mara tusipende kujifungia ndani wakati huko nje watu wanapiga kazi na wako mbali sana


5. TUPENDE KUINGIA GHARAMA KUFANYA TAFITI AU KUJIFUNZA KWA AJILI YA KUBORESHA BIASHARA ZETU.

-Tunapenda sana vitu vya Bure, mtu kahangaika katunga kitabu chake mtu anakitaka bure, tuache mambo ya bure, ili ufanikiwe ni lazima na wewe utoe pesa, Unakuta kuna semina za labda za kufuga kuku au Bata, mtu ana taka ahudhurie bure au aende and then alipwe, huu ni uwenda wazimu.

Ni lazima utafute taarifa au elimu ya biashara yako mahali kokote kule inako patikana kwa gharama yoyote ile, tusikae halafu mtu anakuja kupost huku kuuliza kama sabuni zina soko au la, huu ni ujinga,

Ni lazima uwekeze vya kutosha ili ufanikiwe ni lazima ugharamike, hakuna mafanikio ya bwerere.

6. TUWE SIRIASI
Watu hatuko siriasi, kuna post inaweza anzishwa ukaona kabisa kwamba hatuko siriasi hata kidogo,

“If you don’t build your dream, someone else will hire you to help them build theirs.” Dhirubhai Ambani
 
Safi sana mkuu Chasha japo ulipotea ila naona umerudi vizuri mwaka huu.

Kweli asilimia kubwa ya wabongo ni watu wa porojo tu, na ujasiriamali wa nyuma ya keyboard.

Wanaofanya tafiti na kujikita hasa katika kuzalisha na kuuza ni wachache mno, unaweza kuanzisha mada hapa kuulizia ishu fulani cha ajabu wakichangia wawili watatu tu tayari watu kibao wanaanza kuulizia mashammba huko yanapatikanaje, yaani wanahamasika kirahisi mno bila hata kufanya research halafu ukiwapa data wanasoma wanasepa wanasubiri next thread.

Ni wakati sasa wa kuamka na kufokasi katika vitu vichache unavyoweza kuvimudu kuliko kutaka kufanya kila kitu mwisho wa siku hufanikishi hata moja.
 
Last edited by a moderator:
Safi sana mkuu Chasha japo ulipotea ila naona umerudi vizuri mwaka huu.

Kweli asilimia kubwa ya wabongo ni watu wa porojo tu, na ujasiriamali wa nyuma ya keyboard.

Wanaofanya tafiti na kujikita hasa katika kuzalisha na kuuza ni wachache mno, unaweza kuanzisha mada hapa kuulizia ishu fulani cha ajabu wakichangia wawili watatu tu tayari watu kibao wanaanza kuulizia mashammba huko yanapatikanaje, yaani wanahamasika kirahisi mno bila hata kufanya research halafu ukiwapa data wanasoma wanasepa wanasubiri next thread.

Ni wakati sasa wa kuamka na kufokasi katika vitu vichache unavyoweza kuvimudu kuliko kutaka kufanya kila kitu mwisho wa siku hufanikishi hata moja.

Mkuu sijapotea ila mambo ndo mengi sana na Bado nitaendelea kuto onekana si kwamba ndo nimerudi,

Ni kweli kabisa, tunatakiwa kupigana kufa na kupona, na si kupigana tu tunatakiwa kuwa na strategies kari sana ni lazima watu wawe na malengo na si kufanya ilimuradi unafanya, Ni lazima tuwe na uhakika na kile tunacho fanya na nilazima tuwe wabunifu kwa kile tunacho fanya pia.

Tuko nyuma sana asikumbie mtu, tunahitaji kukimbia tena kwa speed kubwa sana, ni lazima tuamke sasa, maneno yanatosha.
 
Bro... umesema vema sana, na hakika unakereka na hali halisi. Wengi watachangia na kusema ndivyo tulivyo,,, wakati wakenya wanatupora ajira, wanatupora dada zetu....kuna siku tutakosa ya kuwaeleza watoto wetu.

But tunaweza, naomba fanyia kazi suala la mitandao na club za ujasiriamali, nna hakika tutaungwa mkono na wengi wenye nia dhabiti. Mara nyingi huwa tunaogopa kuanzisha, but vikianzishwa twajitokeza, na hapo ndo tutajua wakina nani wako serious.....kweli huu mwaka upo speed mno tuamke...
 
naunga mkono kwa 100%. nimekua naongea na vijana wenzangu kila mara kuwaeleza hili kila tunapokaa na kujadili mambo muhimu ya ujasiriamali lakini inakua ngumu kwa maana wengi wa watanzania haswa vijana wa mjini tumekua tunachukulia suala la kilimo au ufugaji kua ni la pembeni na kwamba since una kazi yako kilimo unataka kufanya iwe ni second opt hii si sawa mwisho wa yote unakuta hufanikiwi kwa sababu hukuweka nguvu zako za kutosha kwenye jambo unalolifanya.embu tujiulize kaburu anatoka south africa anakuja kufuga kuku tanzania au anakuja kufuga ng'ombe lakini kwa sababu anafuga vizuri kwa anapata masoko hata ya majirani zako ambao ulikua unawauzia wewe wale kuku wako ambao hukuwalisha vizuri.
mwisho kabisa ili kutoka katika hili ni muhimu sana kujiunga ktk vikundi vidogo vya ujasiriamali kwa ajili ya kupata ushauri na pia ni rahisi kumuita mtaalamu kuja kuwafundisha baadhi ya mambo yanayohusu mnanolifanya.
 
elimu nzuri sana nashukuru umenifungua macho
 
elimu nzuri sana nashukuru umenifungua macho

Mkuu ndo kama hivyo, inatakiwa tukomae sana, tuache kufanya mambo kwa kufuata mkumbo, ni lazima watu wawe na malengo, na si kufanya mambo ilimuladi wakuone
 
Hapo kaka umesema kweli, uzalendo ndo issue kubwa kwao, hizo supermaket utakuta 80% bidhaa za kwao nd only 20% impoteded, kingine ni ubora wa bidhaa za kwao zina hadhi ya kimataifa je za kwetu zina hadhi gani? Twapenda pesa kuliko kuboresha bidhaa zetu, sijui kwanini tunapenda xana bidhaa adhimu na kwa bei lahisi
Upedekezo wangu ni
1. Tuboleshe bidhaa zetu zifikie kiwango cha kimataifa
2. Tuconsume local product
 
Mkuu chasha,Heri ya Mwaka Mpya! Shukrani kwa kukumbushanai,Binafsi nimehamacka kuwa JF kutokana na Mada zilizokuwa zinawekwa humu Ila wakwongwe mme2kimbia,2naomba mrudi tunawategemea sana! Khs Uzalendo wa Bidhaa ze2,Kwanza 2kubali %kubwa YA Bidhaa ze2 hazina ubora wakimataifa,Namteja anaponunua Bidhaa anataka aone thamani ya Pesa yake so kwanza 2jikite kuboresha bidhaa uzalendo utakuja2 Juzi nilinunua Karanga huwa wanachanganya na Mayai LEBO inaonyesha Expire dec28 Muuzaji anasema zimetengezwa jana OVYO sn!
 
Naamini ombi langu lakurudi mara kwa mara Jukwaani kutupa machache mtalizingatia! Watz bado tuna Safari ndefu sana! Kum-badilisha mtu Fikra C issue ndogo ukichukulia enzi ya Nyerere kila kitu ilikuwa inafanya Serikali hata kuchimba CHOO mtu hajui tulikuwa tunawekewa hadi maBWANA AFYA baada miaka mingi kupita angalau watu wanelimika ss so Tuckate tamaa ktk watu 10 watakao pata ELIMU wakielewa wawili ni cmbaya!
 
Kupenda bidhaa za nje ya nchi ni ulimbukeni uliopitilliza.
 
Mkuu ndo kama hivyo, inatakiwa tukomae sana, tuache kufanya mambo kwa kufuata mkumbo, ni lazima watu wawe na malengo, na si kufanya mambo ilimuladi wakuone

Nimependa sana mada.

Nimependa sana hii ya club, nakuomba uganyie kazi tuanzishe tukutanem tujifunze, tujikwamue na umaskini.
 
Mkuu unaweza kunitumia hii thread kwenye email yangu pliz
email: aba.pelhama@yahoocom
imenikosha nakutoa usingizini, nisaidie plizzz, mi mgeni kwenye computer.
 
Nimependa sana mada.

Nimependa sana hii ya club, nakuomba uganyie kazi tuanzishe tukutanem tujifunze, tujikwamue na umaskini.

Mkuu hii inakuwa nzuri endapo inahusisha watu wa karibu Mfano kama Uko Dar basi watu wa Dar na kama uko Arusha basi watu wa Arusha, Moshi na Manyara na mikoa mingine hivyo hivyo,

Hii itasaidia kupunguza gharama kwa sababu mara nyingi watu wanaweza kuwa wanakutana kila baada ya wiki mbili au mwezi,
Najua watu wanaweza ona haina maana yoyote ile but umuhimu wake ipo siku watu watauona, Wabongo tunapenda tuonekane kila mmoja yuko bise kivyake vyake huku akiwa amejufungia ndani kumbe huko nje watu wanafanya vitu vipya,

sawa
 
Asante mkuu kwa thread yaani nimeangalia jiko langu blue band/prestige margarine,drinking chocolate,fish masala,Royco mchuzi mix, sausage, soya sauce, tomato sauce na etc Made from Kenya. Duu but Made in Tanzania nimekuta Asali,kiberiti na mafuta ya Alizeti.

Tuna kazi kubwa sana ya kufanya watanzania, kwangu naona fursa nyingi.But mkuu kamaliza yote hapo juu.
 
Mkuu hii inakuwa nzuri endapo inahusisha watu wa karibu Mfano kama Uko Dar basi watu wa Dar na kama uko Arusha basi watu wa Arusha, Moshi na Manyara na mikoa mingine hivyo hivyo,

Hii itasaidia kupunguza gharama kwa sababu mara nyingi watu wanaweza kuwa wanakutana kila baada ya wiki mbili au mwezi,
Najua watu wanaweza ona haina maana yoyote ile but umuhimu wake ipo siku watu watauona, Wabongo tunapenda

tuonekane kila mmoja yuko bise kivyake vyake huku akiwa amejufungia ndani kumbe huko nje watu wanafanya vitu vipya,

sawa


Iwe club ya ujumla kisha kuwe na matawi kwa mikoa, hii itakuwa vyema sana, inawezakena hata kupanga safari ya kutembeleana kimkoa kujifunza. Mi nafikiri anzisha thread yenye conditions watu tujiunge halafu kila mtu aseme yuko wapi.
 
Back
Top Bottom