Wale ambao huwa mnakwenda kwa waganga wa kienyeji kimya kimya hii kitu inawahusu

Wale ambao huwa mnakwenda kwa waganga wa kienyeji kimya kimya hii kitu inawahusu

Mjomba side

Member
Joined
May 3, 2024
Posts
72
Reaction score
96
Mshikaji wangu mmoja baada ya kumaliza Chuo mwaka 2014 na kukosa Kazi, aliingia kwenye biashara za M Pesa, Tigo Pesa na bank. Mpaka mwaka 2020 alikuwa amejenga nyumba kubwa na kuanzisha familia.

Kijiwe chake kilikua sana na kitu nilichokiona pale ilikuwa ni nidhamu. Jamaa alikuwa anafungua Mapema sana na Kufunga saa sita usiku. Kitu pekee niliona Kama red flag ni Imani za kishirikina na niliwahi kumwambia kabisa haya mafanikio yako ni juhudi sio uganga lakini hakuwahi kuamini.

Mwaka 2023 alitoa Pesa zake zote bank Kama million 50 hapo na kuzipeleka kwa Mganga kwa ahadi za kuzifanya ziwe million 100. Ghafla akawa hapatikani. Baada ya wiki moja mwili wake ulikutwa mtoni ukiwa umechinjwa na kutobelewa macho.

Postmortem ilionyesha kwamba mwili ulikuwa kama na masaa machache baada ya kifo. Inaonekana walikaa naye kama wiki moja Kabla ya kumchinja.

Mke wake alipoenda bank alikuta deni la bank huku account in 200k tu. Yule Mganga alikuwa suspect na kukamatwa baada ya kufanya marekebisho ya nyumba, kununua Gari na vitu Vya thamani kwa muda mfupi tu lakini pia yeye kuwa wa Mwisho kuwasiliana na marehemu na baadhi ya Simu za Kazi za marehemu kukutwa kwake.

Lesson: Waganga wangekuwa na dawa ya pesa wangetengeneza pesa zao kwanza.
 
Watanzania Tunaongoza kuamini ushirikina mnoo tena sana.

Hata kila kazi ukigusa utaambiwa bila ushirikina hutoboi.

Mara wachezaji wanalogana, mara vilabu vya mpira vinaloga, Mara walimu wanalogwa, mara biashara zinahitaji kafara au zindiko, Mara siasa bila kuloga hufanikiwi.

yaani ukimkosa mtanzania kwenye kuamini uganga basi utamkuta kabobea kwenye kuamini manabiii ambao nao ni Wale wale waganga wanaotumia dini.

Hebu chunguza watu wangapi wanao amini Chuma ulete. Watu wanatumia hela kijinga wanasingizia chuma ulete
 
Mshikaji wangu mmoja baada ya kumaliza Chuo mwaka 2014 na kukosa Kazi, aliingia kwenye biashara za M Pesa, Tigo Pesa na bank. Mpaka mwaka 2020 alikua amejenga nyumba kubwa na kuanzisha familia.

Kijiwe chake kilikua sana na kitu nilichokiona pale ilikua ni nidhamu. Jamaa alikua anafungua Mapema sana na Kufunga saa sita usiku. Kitu pekee niliona Kama red flag ni Imani za kishirikina na niliwahi kumwambia kabisa haya mafanikio yako ni juhudi sio uganga lakini hakuwahi kuamini.

Mwaka 2023 alitoa Pesa zake zote bank Kama million 50 hapo na kuzipeleka kwa Mganga kwa ahadi za kuzifanya ziwe million 100. Ghafla akawa hapatikani. Baada ya wiki moja mwili wake ulikutwa mtoni ukiwa umechinjwa na kutobelewa macho.

Postmortem ilionyenya kwamba mwili ulikua Kama na masaa machache baada ya kifo. Inaonekana walikaa naye kama wiki moja Kabla ya kumchinja

Mke wake alipoenda bank alikuta deni la bank huku account in 200k tu. Yule Mganga alikua suspect na kukamatwa baada ya kufanya marekebisho ya nyumba, kununua Gari na vitu Vya thamani kwa muda mfupi tu lakini pia yeye kua wa Mwisho kuwasiliana na marehemu na baadhi ya Simu za Kazi za marehemu kukutwa kwake.

Lesson: waganga wangekua na dawa ya pesa wangetengeneza pesa zao kwanza.
Hapoo mwisho ndio ilikuwa swali langu mkuu huwa nikiona post za wagangaa nauliza waliopenya walifika kwa waganga wakaona wanavyoishii.....

Niliwahii kwenda na jamaa bagamoyo kufika mazingira niliooona nikaishia kumsubiria kwenye gariii

Aliporudi akaulizaa mbona mpwa umebaki ndani jamaa yuko vizuri nkamwambia sasa kama huyu bwana anaweza kudouble 20mil kwa nn aishi nyumba ya aina hii aisee
Mengine tunamsiingizia shetan...
 
Back
Top Bottom