Wale tuliounganishwa na kifurushi cha DStv Business halafu wakatubadilikia tukutane hapa tujifariji

Wale tuliounganishwa na kifurushi cha DStv Business halafu wakatubadilikia tukutane hapa tujifariji

Christopher Wallace

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2015
Posts
1,479
Reaction score
3,788
Wiki chache zilizopita mawakala wa DStv walitushawishi tujiunge na Dstv business kwa kifurushi cha Work Essential ambacho tulikuwa tunalipa 28,000/= na kupata mechi za EPL, La Liga, Serie A, Europa League na mechi chache za Uefa Champions League.

Sasa kumbe ulikuwa mtego, watu tukaunganishwa kwa wingi kwa kigezo cha kutuma namba ya dikoda, namba ya simu na tin namba na wengineo walidaiwa hadi leseni ya biashara.

Hatimae tukaungwa tukaanza kula burudani kwa elfu 28 ndio elfu 28 tu.

Kifurushi kikaisha muda wake bhana, kuunga tena inagoma? Ikabidi niwapandie hewani DStv, wakaniambia kifurushi cha elfu 28 hakipo, hivyo unatakiwa ulipie kifurushi cha elfu 81 kile wanakiita Work Ultra.

Nikawaambia siwezi, basi niondoeni kwenye DStv business ili nijiunge na vifurushi vya kawaida wanasema kwasasa hawana hiyo huduma.

Naamini sipo peke yangu, kama umekutana na hiyo kadhia karibu jukwaani tufarijiane...
 
Mkuu hauko peke yako hata mimi nimepigwa na kitu kizito mno, wanasema hakuna huduma ya kurejesha kwenye Normal labda ununue dekoda mpya. Aiseee Dstv wameniweza kuhusu hili.
Nimeenda ofisini kwao kabsa wakasema hawawezi kurudisha kwenye normal maana ule ni mkataba. Ukitaka ufurahi tena Lazima ununue dekoda nyingine.
Wale vijana ni washezi sana, wametuingiza kwenye mtego wa kipuuzi sana kwa taarifa yao mimi siwezi kulipia elfu 81 bora ninunue kingine.
 
Mkuu hauko peke yako hata mimi nimepigwa na kitu kizito mno, wanasema hakuna huduma ya kurejesha kwenye Normal labda ununue dekoda mpya. Aiseee Dstv wameniweza kuhusu hili.
Nimeenda ofisini kwao kabsa wakasema hawawezi kurudisha kwenye normal maana ule ni mkataba. Ukitaka ufurahi tena Lazima ununue dekoda nyingine.
Wale vijana ni washezi sana, wametuingiza kwenye mtego wa kipuuzi sana kwa taarifa yao mimi siwezi kulipia elfu 81 bora ninunue kingine.
Kwenye hili nawapa hongera sana Azam, yaani ukinunua kifurushi jana yake kwa mfano, labda cha elfu 23,000 halafu leo ukabadili mawazo na kutaka kifurushi cha 36,000 basi unawapigia na unawaeleza na kuwapa namba ya Decoder then unaongeza 13,000 wanakubadilishia chap...
 
Unataka utumie DSTV wakati uwezo wako ni wa Star Times?
Unataka umiliki iphone kwa bei ya itel kuweni serious wajameni.
Kitonga ni mbaya,waliwajaza na mkajazika.
Dada mwajuma kila siku nakuambia uwe unatumia kichwa kufikiria badala ya masaburi, kitonga gani wakati tulikuwa tunalipa pesa zetu
 
Mkuu hauko peke yako hata mimi nimepigwa na kitu kizito mno, wanasema hakuna huduma ya kurejesha kwenye Normal labda ununue dekoda mpya. Aiseee Dstv wameniweza kuhusu hili.
Nimeenda ofisini kwao kabsa wakasema hawawezi kurudisha kwenye normal maana ule ni mkataba. Ukitaka ufurahi tena Lazima ununue dekoda nyingine.
Wale vijana ni washezi sana, wametuingiza kwenye mtego wa kipuuzi sana kwa taarifa yao mimi siwezi kulipia elfu 81 bora ninunue kingine.
Na nimeshanunua dikoda nyingine hii na hapa nakula burudani nikisubiria kombe la dunia
 
Kwenye hili nawapa hongera sana Azam, yaani ukinunua kifurushi jana yake kwa mfano, labda cha elfu 23,000 halafu leo ukabadili mawazo na kutaka kifurushi cha 36,000 basi unawapigia na unawaeleza na kuwapa namba ya Decoder then unaongeza 13,000 wanakubadilishia chap...
Mkuu hata hiyo huduma ya ku-upgrade na ku-downgrade Dstv ipo sema tunachojadili sisi ni kitu kingine kabisa
 
Back
Top Bottom