Wale tusiompenda Kocha Amunike, Kikosi chake alichokichagua na tunaoiombea mabaya Taifa Stars ili ifungwe tujuane tafadhali

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mimi nakuwa Namba Moja kwa Mtu nisiyempenda kabisa Kocha wa Taifa Stars Emanuel Amunike, Kikosi chake Kibovu alichokichagua na ambaye kila Siku huwa napiga Dua ya Kuiombea mabaya Timu hii ifungwe kwa Aibu huko Mashindanoni AFCON 2019 nchini Misri.

Naomba na wale wengine mlio kama Mimi mjitokeze hapa ili tujuane mapema ili ikiwezekana tuanze Kupanga Mikakati ya kwenda Kumpokea huyu Kocha na Mabango pale JNIA Siku wakirejea na Makapu yao ya Magoli na ikiwezekana hata Kumpopoa na Mawe au Mayai Viza ili ajue kuwa hatumtaki na atuachie Timu yetu.

Tujadili.
 
Hebu weka kikosi chako ulichopenda kiwe....

1. Aishi Manula
2. Erasto Nyoni
3. Abdi Banda
4. Aggrey Morris
5. Kelvin Yondan
6. Jonas Mkude
7. Simon Msuva
8. Ibrahim Ajib
9. John Boko
10. Mbwana Ally Samatta ( Captain )
11. Shiza Kichuya

Kwa Kikosi changu hiki na kwa Hamasa Kubwa iliyopo nina uhakika hawa akina Senegal, Algeria na Kenya wangesimama na Taifa Stars ingetinga katika 16 Bora. Na hiki Kikosi nimekipanga Kiufundi kabisa nikizingatia Umuhimu wa Wachezaji, Uwezo wao na Uchezaji wao hasa wakiwa ama ndani au nje ya Watanzania. Na kwa sasa Tanzania hatuna Kikosi Imara na Bora kama hiki ambacho nimekitaja hapa na ukibisha basi utakuwa tu unapenda Mabishano.
 
Timu ikifungwa aibu ni kwa Amunike?
Yaani kutijumuishwa Banda , Ajibu na Mkude ndio unahitimisha kuwa kikosi ni kibovu?
Hao Mkude na Banda wapo kwenye soka zaidi ya miaka mitano je wameonyesha nini special kiasi hicho?
 
zaidi ya kona aliyowafunga yanga kuna nini zaidi kwa kichuya!?...ajibu mvivu,mkude huwa anaomba kocha apunguze mazoezi
 
Kikosi chako kibovu kama kauli zako!! Hicho kikosi kipeleke SIMBA DAY
 
zaidi ya kona aliyowafunga yanga kuna nini zaidi kwa kichuya!?...ajibu mvivu,mkude huwa anaomba kocha apunguze mazoezi
Kati ya watu walioharibu maana ya neno "sifa" ni huyo Kichuya. Sijui "sifa" anazopewa ni za nini?
 
Lini ulifanya mazoezi na hicho kikosi ukaona kiko vizuri au majina yamekuvutia?.
 


Acheni Upumbavu ninyi, Hili ni Taifa letu hatupaswi kulihujumu kwa namna yoyote ile huyo Amnunike amekuja ataondoka na atatuacha hapa Tanzania tusichukiane au kupandikiza Chuki bila sababu za Msingi!
 
Kichuya huyu hafai hata kuchezea ndanda
 
Siwezi kuiponda /kudharau kitu chochote kinachowakilisha Taifa langu kwakutafuta sifa mitandaoni!!
 
Nchi inashika nafasi ya 131katika viwango vya soka ulimwenguni kisha unatarajia tufanye Maajabu! Miaka 38 nchi haijafuzu kwa mashindano haya eti leo tukifungwa lawama anapewa Amunike! Kisa? Ajibu, Mkude hawapo kikosini! Wanakipi cha ajabu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…