Wale 'Waswahili' ambao 'mlinidhihaki' pale niliposema kuwa Mchezaji Pape Ousmane Sakho ni Hazina na kamwe asiachwe Simba SC mpo wapi leo?

Wale 'Waswahili' ambao 'mlinidhihaki' pale niliposema kuwa Mchezaji Pape Ousmane Sakho ni Hazina na kamwe asiachwe Simba SC mpo wapi leo?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Yaani kabisa GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE niseme Jambo au Kitu fulani halafu nikosee au nisiwe na uhakika nalo? au nimpende Mchezaji fulani kama nimpendavyo Khalid Aucho, Yanick Bangala, Jonas Mkude na Pape Ousmane Sakho halafu nikosee au wasiwe Wazuri kama nilivyowaona na Kuwasoma Kiuwezo?

Asante sana Mwenyezi Mungu (Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo) kwa Kunibariki na Kipaji kikubwa cha kufanya Critical Observation kuhusu Mtu au Jambo au Tukio fulani na kuwa na Jicho Kali kabisa la Kimaono na Kiufundi.

Ni Mimi ndiyo nilikuwa Mtetezi Mkuu wa Kiungo Jonas Gerald Mkude Mitandaoni pale 'Waswahili' wengi waliposema hatufai tena Simba SC na kwamba aachwe ila nikawa nasema Tanzania nzima bado sijaona Kiungo mwenye kila Kitu (Complete Defensive Midfielder) kama Yeye (Mkude) na asamehewe asiachwe na hatimaye leo ananijibia Kimatendo kwa Kucheza vizuri Uwanjani huku sasa akiwa ni 'more matured' na amekuwa na Nidhamu ya hali ya Juu na ndiyo Mhimili Mkuu wa Simba SC kwa sasa (Watu wa Mpira tunasema kuwa Mkude ndiyo mwenye Simba SC yake) Kudadadeki.

Na hivi majuzi tena niliibuka hapa hapa JamiiForums na kuwa Mtetezi Mkuu wa Mchezaji Pape Ousmane Sakho (Raia wa Senegal ) kuwa kamwe asiachwe Kikosini Simba SC na nikaenda mbele Kumchambua Kiufundi cha Kusikitisha kama Kawaida 'Waswahili' wakajitokeza na kuanza Kunidhihaki mpaka Kunitukana kuwa sijui Mpira, ila namshukuru Mwenyezi Mungu katika Mechi zake Tatu au Nne tu alizocheza Sakho ameshanijibia kwa 'Waswahili' kile nilichokuwa nakisema na namtetea.

Na kwa taarifa yenu tu 'Waswahili' huo 'Uwezo' wa Ajabu ( wa Hali ya Juu ) anaouonyesha sasa Mchezaji Pape Ousmane Sakho ni 45% tu ila tegemeeni Makubwa kutoka Kwake kwani ni Mchezaji mwenye Kipaji cha Hali ya Juu kabisa na ili umpate Sakho Mmoja yakupasa Uwaunganishe akina Ntibazonkiza, Mayele, Fei Toto na Moloko.

Haya 'Waswahili' karibuni tena muanze Kunipinga, Kunidhihaki na Kunitukana, ila msisahau tu kuwa Mwenyezi Mungu alinibariki vingi sana GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ambavyo nyie kutokana na 'Uswahili' wenu hakuona haja ya Kuwatunuku navyo na ifike mahala muwe mnakubali kuwa Binadamu ( Wanadamu ) tunatofautiana hasa katika 'Talanta' fulani fulani.
 
vip unamzungumziaje na wale wachezaji wanaofanya majaribio wanatufaa au?
 
sifa na utukufu ni vyako Gentamycine

[emoji120]
Amina Mkuu na Ashukuriwe zaidi Mwenyezi Mungu na namuomba huu 'Uwezo' na hii 'Talanta' ya Kipekee 'aliyonitunuku' nayo basi 'awatunuku' na Wengine pia ili wasiendelee kuwa 'Waswahili' kama walivyo sasa.
 
Sakho ni wakawaoda tu. Umachachari wake hauna utofauti na ule wa Kisinda.
 
vip unamzungumziaje na wale wachezaji wanaofanya majaribio wanatufaa au?
Uongozi wa Simba SC ubadilike na uache nao kufanya 'Uswahili' Kwetu Sisi Mashabiki.

Sihitaji kumtizama Mchezaji kwa dakika 90 au Mechi 3 au 5 ila Kwangu Mimi GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE nikimuona tu Mchezaji kwa dakika 5 mpakae 15 zinatosha kujua Uwezo wake.

Namheshimu sana Kiungo Shiboub ila kwa sasa na anavyocheza nitaulamu mno Uongozi wa Simba SC ukimsajili kwani Simba SC ya sasa ina Viungo wazuri wa Kumzidi.

Huyu Mchezaji Moukoro Tenena ( Ivory Coast ) ndiyo bure ( hovyo ) kabisa kwani nae anazidiwa Vitu vingi na Mzawa Yusuph Mhilu.

Poti wangu Crescetius Magori najua 'unanifolo' na kunisoma sana hapa JamiiForums tafadhali achaneni na Shiboub na huyo Moukoro bali mwambie Mo aache Ubahili ( Ulugume ) wake na atusajilie Majembe ya maana siyo Vituko hivi.
 
Mhilu sijui Nan alimsajil maana Sion Kama Ana sifa za kuwa club kubwa Kama Simba.
Shibobo Ni wa kawaida kabisa kwa Simba ya Sasa.
Moukoro kwa maono yangu naona Kama Ana kitu fulan kizuri ,touches zake sio haba Ila shida Ni umri wake.

Swala la sakho Ni kweli wengi walimbeza Sana hasa wa upande wa pili ,sijui Hawa watani zetu wapoje wao Ni kuponda kila kitu Cha Simba Ajabu Sasa wanataka kujifananisha na hao hao wanaowaponda.

Kuna chizi mwingine alifikia hatua et Simba kwasasa Ni ya kawaida Zaid mpinzani wa kweli wa yanga Ni Azam[emoji23][emoji23][emoji23] dah nchi ngumu Sana hii.

Yaan et kisa mimi Ni Simba nijitoe ufahamu niseme Aucho ,Bangala, Yassin ,Kibwana,Ni wachezaji wa kawaida wakati moyo wangu unakir wazi kuwa Ni wachezaj wazuri Sana na wanaupiga mwingi balaaa.
Mimi hata nikiwa na washakaji zangu wale wa Simba na yanga hua nawambia wazi kuwa yanga nawakubal wachezaj wanne pekee ndio hunivutia nao Ni Aucho ,Bangala ,Yassin na Kibwana ,huyo fei mm sijawah mwelewa maana Ni overrated Sana wakat Hana uwezo wa kuibeba timu kwenye mechi ngumu.
Ajabu Sasa Wana yanga wao Ni kuponda tu kila mchezaji wa Simba ,ukimuuliza Ni mchezaji gan unamkubal toka Simba atakwambia hayupo hata mmoja Wala Sion mchezaji wa Simba wa kupata no kwa yanga ya Sasa[emoji15][emoji15] unabak unahamak.
 
Nilitaka nishangae usije na siredi ya kujisifia ,enewei mara nyingi unachambua vizuri na kwa 90% maono yako yanakuwa kweli kama kwa Dickson Job na wengine.
 
Huyo jamaa ananikera ushangiliaje wake,yaani wenzake wanaenda kumpa support anapofunga halafu yeye anawakwepa au pengine anawasukuma Kwa likono lake!
Ndio maana jana watu wakamwacha ashangilie Peke yake!
 
Huyo jamaa ananikera ushangiliaje wake,yaani wenzake wanaenda kumpa support anapofunga halafu yeye anawakwepa au pengine anawasukuma Kwa likono lake!
Ndio maana jana watu wakamwacha ashangilie Peke yake!
Ndo style yake, itabidi umuelewe tu hivyo unamwacha ashangilie mwenyewe!!

Itafika wakati atajishtukia na kuacha hiyo tabia ya kushangilia mwenyewe, ni kweli ana hulka ya kukwepa wenzake akifunga

Sent from my A37fw using JamiiForums mobile app
 
Huyo jamaa ananikera ushangiliaje wake,yaani wenzake wanaenda kumpa support anapofunga halafu yeye anawakwepa au pengine anawasukuma Kwa likono lake!
Ndio maana jana watu wakamwacha ashangilie Peke yake!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ndo style yake, itabidi umuelewe tu hivyo unamwacha ashangilie mwenyewe!!

Itafika wakati atajishtukia na kuacha hiyo tabia ya kushangilia mwenyewe, ni kweli ana hulka ya kukwepa wenzake akifunga

Sent from my A37fw using JamiiForums mobile app
Wamwache awe anashangilia mwenyewe mpaka ajirekebishe!
Ni mchezaji mzuri though
 
Huyo jamaa ananikera ushangiliaje wake,yaani wenzake wanaenda kumpa support anapofunga halafu yeye anawakwepa au pengine anawasukuma Kwa likono lake!
Ndio maana jana watu wakamwacha ashangilie Peke yake!
yeye anashangilia na jukwaa. anaweka chill kwenye mchuzi. kushangilia na kina Kibu inataka moyo anaweza kukurukia ghafla ukavunja mgongo
 
yeye anashangilia na jukwaa. anaweka chill kwenye mchuzi. kushangilia na kina Kibu inataka moyo anaweza kukurukia ghafla ukavunja mgongo
Akiwa anaweka chill kwenye mchuzi ukamsogelea unakutana na bonge Moja la push,hutamani kumrudia!
Nani anataka kadhia hiyo,ndio maana wakamwacha ashangilie mwenyewe!Na akiendelea hivyo,kila akifunga wanamwacha anaenda kushangalia,wao wanarudi Kati!
 
Uongozi wa Simba SC ubadilike na uache nao kufanya 'Uswahili' Kwetu Sisi Mashabiki.

Sihitaji kumtizama Mchezaji kwa dakika 90 au Mechi 3 au 5 ila Kwangu Mimi GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE nikimuona tu Mchezaji kwa dakika 5 mpakae 15 zinatosha kujua Uwezo wake.

Namheshimu sana Kiungo Shiboub ila kwa sasa na anavyocheza nitaulamu mno Uongozi wa Simba SC ukimsajili kwani Simba SC ya sasa ina Viungo wazuri wa Kumzidi.

Huyu Mchezaji Moukoro Tenena ( Ivory Coast ) ndiyo bure ( hovyo ) kabisa kwani nae anazidiwa Vitu vingi na Mzawa Yusuph Mhilu.

Poti wangu Crescetius Magori najua 'unanifolo' na kunisoma sana hapa JamiiForums tafadhali achaneni na Shiboub na huyo Moukoro bali mwambie Mo aache Ubahili ( Ulugume ) wake na atusajilie Majembe ya maana siyo Vituko hivi.

Nakubaliana na wewe The Antibiotique[emoji119][emoji119]
 
Bado sijamkubali
Mwepesi sana anaanguka anguka kila wakati.
Body physic ni 10%
Akikutana na timu zenye wachezaji wenye nguvu ataishia kudondoka dondoka tu kama Morrison.
Kukaba ni 13%
Mshambuliaji wa timu kubwa lazima awe na nguvu ya kupangua mabeki.
Afadhali na Maukolo kidogo ana stamina nzuri.
 
Back
Top Bottom