Wale wote wanaotumia bidhaa za kampuni ya Xiaomi tukutane hapa ili kupeana ujanja

Mr mobile nipe mchango wako hapa
Kati ya Mi A3 na redmi note8 nijitose wapi???
Ikiwa AMOLED display na In Display Fingerprint sensor ni vitu unavyopenda chukua Mi A3 lakini ujue resolution yake ni ndogo 720p wakati Note 8 ina 1080p.
Mi A3 haina Macro lens lakini Note 8 inayo. Mi A3 ina selfie kamera bora zaidi.
Ikiwa wewe ni mpenzi wa screen ndogo basi Mi A3 ndio simu ya kuchukua. Ikiwa wewe ni mpenzi wa Stock Android chukua Mi A3 lakini ujue utakosa utamu wa features za MIUI😁

Kwa mimi, Nadhani ningechukua Redmi Note 8 kuliko Mi A3 😉
 
Bei hii ni ya AliExpress?
Hapana mkuu. Nimecheki kwenye website mbalimbali ila inaweza kuwa juu ya hapo. Maana bei waliyoitaja kule Madrid ni €549 yenye 6+128GB na €649 yenye 8+256GB.
N.B kwa china bei inaweza kuwa pungufu zaidi.
 
Bei hii ni ya AliExpress?
Hata Aliexpress ni mil 1.2 tu kwa Mi france
Xiaomi Mi Note 10 (CC9 Pro) 108MP Penta Camera 6GB 128GB MIUI 11 Qualcomm Snapdragon 730G.
Around TZS
1,128,000
Hujakosea ndio bei pia ya Aliexpress
Mi France store inauzwa milioni na laki 6
Hii ya mil 1.6 kwa Mi france ni premium version. Lakin anayo pia kwa bei ya mil 1.2 tembelea page yake uone, au seach note 10 zije zote zilizopo hapo A-xps
 
Asante Mkuu
Hapana mkuu. Nimecheki kwenye website mbalimbali ila inaweza kuwa juu ya hapo. Maana bei waliyoitaja kule Madrid ni €549 yenye 6+128GB na €649 yenye 8+256GB.
N.B kwa china bei inaweza kuwa pungufu zaidi.
 
[emoji120][emoji120]
Hata Aliexpress ni mil 1.2 tu kwa Mi franceHujakosea ndio bei pia ya AliexpressHii ya mil 1.6 kwa Mi france ni premium version. Lakin anayo pia kwa bei ya mil 1.2 tembelea page yake uone, au seach note 10 zije zote zilizopo hapo A-xps
 
Wakuu hivi mzigo Wangu utakuwa umepigwa hapa au... Maana nilinunua Redmi note 7 64gb, 6 ram

Lakini haijafika mpaka sasa, tangu nimenunua mwezi uliopita tarehe 11.

Huyu jamaa wa posta Dar kanicheki ndio Kanipa hili jibu.
Naomba uzoefu maana katika tracking mzigo unaonesha haujafika Tanzania. Kwa uzoefu wangu ilitakiwa ufike mpaka nilipo lakini hili jibu limenistua sana. Maana upigaji wa mzigo umerudi au nini hii.
 
Pale JNIA kuna shida sana ila kama wamejua tatizo uwe na tumaini utafika tu.
 
Aisee niko hapa nasikia hadi njaa nimeagiza hiyo hiyo rn7 na tarehe kama yako ila nikiangalia tracking haina update yoyote,,,,hata sijui inakuaje
 
Hata mimi kuna mzigo wangu ulikwama hapo. Baada ya siku 15 nikaanza kupigia simu posta Dar es Salaam wakanijibu kuwa mzigo wangu uli-miss kwenye bag lilipokelewa. Baadae nika-open dispute nikalipwa.
Na kweli mpaka leo sijaupata toka mwezi wa tisa. Ulitumwa kwa standard shipping
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…