Walianza kupotosha hotuba ya Dkt. Slaa, na sasa wanapotosha hotuba ya Askofu Shoo, watawala wanajua nini kitafuata?

Walianza kupotosha hotuba ya Dkt. Slaa, na sasa wanapotosha hotuba ya Askofu Shoo, watawala wanajua nini kitafuata?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Mara ya kwanza Dkt. Slaa akitoa maoni yake rasmi kuhusu sakata la bandari za Tanganyika kupewa waarabu wa DP world, aliweka wazi msimamo wake kuupinga mkataba ule.

Jambo la ajabu ni kuwa vyombo rasmi vya habari hapa Tanzania (hususani magazeti) yakaja na upotoshaji mkubwa huku yakitengeneza habari ya kutunga na kusema Dkt. Slaa anaunga mkono uwekezaji wa sasa wa Bandari kwenda kwa DP world.

Kilichofuata sote tunajua, Dkt. Slaa aliamua kuingia front line kuurarua vilivyo huo mkataba katika majukwaa mbali mbali ya kisiasa mpaka watawala wakaamua kumkamata na kumtengenezea kesi ya uhaini iliyokuja kubadilika na kuwa kesi ya uchochezi!

Sasa mchezo huo huo, wapambe wa watawala wameamua kuurudia tena, na sasa wametengenezea maneno ya uongo Askofu mkuu wa KKKT, Dr. Shoo eti anaunga mkono uwekezaji wa bandari zetu kwenda kwa waarabu wa DP world.

Kama mchezo huo mchafu hautadhibitiwa na watawala wenyewe, basi tusishangae KKKT kuja na waraka rasmi (utakaosomwa katika makanisa yao yote hapa Tanzania) kuhusu msimamo na maoni yao dhidi ya kuupinga na kuukosoa mkataba wa bandari na DP world ikiwa ni sehemu ya maoni yao rasmi waliyofikisha Ikulu kwa rais Samia hapo kabla.

Tuvute subira.
 
Bahati nzuri upotoshaji wao hauna maana yoyote, watanganyika sio watoto wanaelewa kila kitu.
 
Mazara ya kutoka kazini kufika nyumbani, na hutoki tena zaidi ya kulala, ila unaanza kujipaka mafuta hata kabla ujaoga.
 
Kwa kosa lipi? Hotuba yake sote tumeisikia na hakuna mahala alipowabariki DpWorld na mkataba wao tata!
Ni fake news ndio wanaotaka kupotosha ujumbe wa Askofu Shoo!
 
Vyombo vyahahabali? Vipi Tanzania hii? Hapa tuna wachumia tumbo tuu, hivi ukiwa makini utasema Askofu shoo aliunga mkono uwekezaji wa bandali? Alichosema yeye nikua kanisa halipingi Uwekezaji, ila pia akasema Raisi akumbuke viongozi wadini walimfata namaoni yao, ikulu. Ilapia akasisitiza kua wanaotoa maoni yao isionekane wanachanganya Dini na Siasa. Kwa wahalili makini vichwa vya habali visingesema Dk Shoo Aunga mkono uwekezaji wa bandali. Alisema wao kanisa hawapingi uwekezaji basi, kama ambavyo hata Wakotoriki hawapingi uekezaji, Wao walichopinga ni namna mkataba ulivyo ndivyohivyo hata KKT Na ndomana DK Shoo anakwambia walikwenda viongozi wote wadini, Bilashaka ilikua kumlalamikia namna mkataba ulivyo. Sasa hivyo utasema anaunga mkono uwekezaji wa bandali. Utakua Mvivu wakufikiri.
 
Wachaga Wengi wanafiki,,labda Mbowe tuuu,,Nyeupe Mwambie Nyeupe ,,Lema namkubari saaana.. Lakini Wengine Wapo kimaslahi saaana
 
Back
Top Bottom