Walichokifanya CCM Mkutano Mkuu ni uchaguzi, Uteuzi au kuthibitisha Uteuzi? Hivi hiki kilichofanyika

Walichokifanya CCM Mkutano Mkuu ni uchaguzi, Uteuzi au kuthibitisha Uteuzi? Hivi hiki kilichofanyika

Chief Mwigendya

Senior Member
Joined
Nov 28, 2024
Posts
172
Reaction score
136
Hivi hiki kilichofanyika Mkutano mkuu wa ccm Dodoma leo ni uchaguzi , uteuzi au kuthibitisha jina la mteuliwa ?

Uchaguzi ni kuchagua mtu au vitu zaidi ya kimoja sasa mtu yupo mmoja hapo unakuwa umechagua nini?

Wapiga kura wamepiga kumchagua mzee Wasirsa na nani alikuwa mpinzani wake? Kura za ndiyo na hapana ndiyo walikuwa wapinzani wake ?

Yaani chama kikongwe chenye makada chungu nzima hakuna makada wa kuwashindanisha kweli?

Chama kikongwe mpaka wanachama wana kwenda hawajui wanaenda kumchagua nani?

Ajabu kweli aiseeee. Kilichofanyika sio uchaguzi ni kuthibisha uteuzi wa mzee Wasira na uchaguzi . Toa kwanza kibanzi kwenye jicho lako kabla ya kuto boriti kwenye jicho la mwenzio..
 
Uongozi wa Ccm..
mwenyekiti - Tiss
Makamu wenyeviti - Tiss
Katibu mkuu - Tiss
Wajumbe - wanaccm wote (wasindikizaji)
 
Halafu wanadai chama cha majizi ni chama cha mfano kwa demokrasia Africa.
 
Back
Top Bottom