Walimu kutumia Vishkwambi ni mpaka wapewe semina na elimu kutoka Wizarani?

Walimu kutumia Vishkwambi ni mpaka wapewe semina na elimu kutoka Wizarani?

Mwanajeshi/Polisi utamjua kwa sare zake.

Vivo hivyo Mwalimu utamtambua kwa kishkwambi chake. Yani hata awe na bag mgongoni kishkwambi lazima ashike mkononi.
Ndo nnacho hapa kwenye gari natype[emoji6][emoji6][emoji6][emoji6][emoji6][emoji1][emoji1]
 
Mwanajeshi/Polisi utamjua kwa sare zake.

Vivo hivyo Mwalimu utamtambua kwa kishkwambi chake. Yani hata awe na bag mgongoni kishkwambi lazima ashike mkononi.
Sasa kishikwambi chake ,begi lake, aliyebeba ni yeye ,mgongo wa kwake!! Tatizo nn!?? Hivi wazeee hamna kazi au!!
 
Walimu moja ya maombi yao ni kufunindishwa kutumia kishkwambi, mama Samia yeye ndio akakubali hayo maombi yao
Sio kweli kama walimu wanahitaji seminar. Kuna wahuni watapata perdiem na safari. Wanatumia ububu walionao walimu hawana wakuwasemea.

Cwt ndio muhuni namba moja, viongoz wao walimu ni genge la pili. Hapa kuna deo,reo na huko wizarani. Mwalimu anajua haya mambo na wanaelekezana wenyewe
 
Dah mwalimu kila siku iitwayo leo anazidi kulofazwa
 
Mambo mengine hayahitaji hata akili nyingi kuyang'amua.
Watu wanatumia smartphones walizonunua alafu inatokea mtu anaseme hajui kutumia smartphone aliyopewa na serikali.

Huyu Mh.Rais kuna namna mambo yamemzidi mpaka sasa anashindwa kung'amua upigaji mdogo.

Hapo zitaandaliwa semina watu watajilipa pesa kitakachoendeshwa kwenye hizo semina ni kuwasha kuzima also kufungua files(stupid).
 
Ijulikane kwamba matumizi ya kishkwambi hayana tofauti yoyote na simu janja. Sioni kama ni kipaumbele cha muhimu kwa walimu kupewa mafunzo ya matumizi ya kishkwambi.

Walimu waboreshewe miundombinu ya utendaji kazi, mshahara na posho za ufundishaji.
Aidha, ifahamike kwamba elimu ya tehama hutolewa vyuoni tangu ngazi za cheti hadi elimu ya juu.

Kama mwalimu hawezi kutumia WPS kwenye simu yake huo ni uzembe kwani simu zote huwa na program hii ambayo ina ms word, excel, power point nk.

Hivyo basi hakuna sababu ya kuwaona walimu kama watu wasiojua chochote au huenda ni uzembe wao tu wa kutopenda kujiongeza!
 
Serikali imewaongezea shida nyingine.

Wengi wanavitumia kubet. Pia ni mzigo kuvibeba maana wakiwa njiani wanatembea utadhani wamebeba bunduki(bega moja limeshuka).
reyzzap njoo huku tafadhali!!! Ha hahaa eti bega limeshuka!
===
Hii Habari kumbe ni kweli.
 
Sio kweli, maombi ya walimu ilikua ni kufundishwa kutumia vishkwambi. Wakati maombi yakitolewa mbona ilikua live na hata raisi alipokubali maombi mbona ni live?

Alafu walimu mnapaswa muelewe kishwambi ni smartphone tu Kama zilivyo smartphone zote, utofauti yenyewe Ina screen kubwa tu.
Sawa hivi Kwa akili ya kawaida walimu hawawezi kutumia smartphone?? Ninacho amini kama waliombwa wafundishwe ni kwenye mambo ya kitaalamu zaidi sio kwenye matumizi ya kawaida.
 
Hao lengo lao ni posho, unafikiri hawajui , posho zinawasumbua tu
 
Sawa hivi Kwa akili ya kawaida walimu hawawezi kutumia smartphone?? Ninacho amini kama waliombwa wafundishwe ni kwenye mambo ya kitaalamu zaidi sio kwenye matumizi ya kawaida.
Mambo ya kitaalamu mfano yapi? Tutolee tu mfano
Nakukumbusha tu kishkwambi ni smartphone kama uliyo nayo, utofauti ni screen tu
 
Back
Top Bottom