Kweli adui wa mwalimu ni mwalimu.Hapa Chato maafisa elimu ambao kitaaluma ni walimu ndiyo wanakuwa wa kwanza kuwakandamiza walimu.Ni hivi karibuni maafisa elimu hawa wameagiza tena kwa lazima kwamba walimu wote wachangie madawati.Kinachosikitaisha mwalimu anachangia maendeleo kila mwezi kupitia kodi lakini kuna wafanyabiashara wengi ambao hata kodi hawatoi hata kama wanatoa ni kidogo lakini wao hawaambiwi kuchangia madawati.Hivi serikali inawaona walimu ni wanyonge kiasi hiki .Hivi chama cha walimu wilayani Chato hili mnalijua na kama mnalijua mmechukua hatua gani? Walimu hamkeni hacha woga pingine dhuluma hii ya waziwazi. Onyo kwa serikali iliyoko madarakani kuweni makini na viongozi hawa mbubu ambao wanatoa maamuzi ya ajabu vinginevyo mpaka inafika 2015 mtakuwa na kazi ngumu sana.