Walimu wa Tanzania, hebu tazama hapa


Wewe Una Akili sana!
 
Kwa swala la mgomo kwa walimu kupitia cwt hyo ni ndoto cwt hawana hoja zaid tutawatengenezea pesa mgomo ukishamiri wanaitwa chemba kina mukoba wanalamba chao kwisha kabisa kama cwt wako serious waanzishe kamati ya kuratbu mgomo zen cwt wabaki kama waangalizi wa pembeni kuona mgomo utaendaje sio porojo
 
Mbona hamuongelei mshahara ya wahasibu, au maafisa raslimali
hao wanalipwa kidogo kuliko hata waalimu enewei ntatafuta data niweke
pia wako katika risk ya kufungwa kwa sababu ya wizi wa wakubwa
 
Hawa walimu ndo kichefuchefu kabisa! kwanza walimu jina 2 hawafundishi wameshiriki kusimamia wizi wa kura miaka yote wameifanya ccm ifanye inavyotaka ikijua wapo walimu watasimamia wizi wa kura
 

una uhakika na hayo yenye rangi nyekundu? Ok,wacha wagome kwa sababu wana matokeo mabovu. tuone kama hamtapiga mayowe mkidai hawana huruma na watoto. Wacheni hizo bwana, wote wanaishi ktk nchi hii hii yenye hali ngumu ya maisha.
 
muuguzi cheti anasoma miaka 2 pia,diploma miaka 3,

cheti cha uuguzi cha miaka 2 aka yeboyebo, wahitimu wameingia sokoni tangu mwaka jana mwezi octoba, kabla ya hapo ilikuwa miaka mitatu ya uuguzi pamoja na mwaka mmoja wa ukunga. Hata hivyo kuna tetesi za hao wa miaka miwili kurudishwa shule kwani wanaua hao sio mchezo! Rais dhaifu ametegeneza wauzi dhaifu!
 
kujichoma sindano ni sawa na kula unga wa chaki.
-kurukiwa na damu=na kumwagikiwa na tindikali maabara wakat unaandaa practical
-kupigwa na kichaa=kupigwa na mwanafunz anaekula bange,,,,kila mtu ana riski zake

Kuna hii kitu wenyewe wanaita 'LAST OFFICE' kuusitiri mwili wa marehemu baada ya kufa, jiulize watu wanavyoogopa maiti hata kama ni ya nduguyo na mbaya zaidi ukute mtu mwenyewe aliugua hadi kuwa sklepa, tundu saba za mwili zinatoa usaha.....nesi anakunja huo mzigo. Wanafunzi wa uuguzi huwa wanakimbia fani siku ya kwanza wanapoingia wodini!
 
Ifuatayo ni tofauti ya mishahara kwa watumishi wa umma( ajira mpya) .

ngazi ya cheti;

mwalimu 244,400/=
afya 472,000=,
kilimo/mifugo 959,400/=
sheria 630,000/=.

ngazi ya diploma

mwalimu 325,700/=
afya 682,000/=
kilimo/mifugo 1,133,600/=
sheria 871,500/=

ngazi ya degree

mwalimu 469,200/=
afya 802,200/=
kilimo/mifugo 1,354,000/=
sheria 1,166,000/=

walimu ni wito?
 
Naanza mgomo sasa hivi
mana haiwezekani kudharaulika kiasi hichi fedha dusko sasa
hapo utafanya nini na huwezi fanya ufisadi wowote
 
its pain sana kama hivi ndivyo ilivyo basi cjui kwa cc tunaosomea ualimu kama tutakua na hari ya ufundishaj maana huo mshahara na kama hela ya chai ya baadhi ya wafanya kazi kama madaktri na wanasheria
 

Mkuu, hizi scales za nchi gani?
 
mnazungumzia mshahara?

huyu mwalimu hana allowance hata moja

nyumba hana, bado house allowance hapewi

gari, baikeli, pikipiki hana bado anakaa mbali sana

hana standing allowance kiti darasani hawekewi hata sitting hatapewa

hana chochote

CWT inanyonya kwenye kamshahara hako kadogo

PAYE kubwa sana, akisitaafu lazima akondeane

bora polisi anaishi mabatini mwalimu hana hata hilo pipa

wataalam wazuri wanaikimbia hii ajira kama pepo na kus na kaskaz
 
Dodoma walimu wanaanza rasmi mchakato jinsi watakavyogoma leo,wanakutana wilayani mwao.
2nawatakia maandalizi mema walimu.Arusha pia wanaanza leo maandalizi mpaka kieleweke mwaka huu
 

inauma lakini hivyo viwango ulipata wapi...?
 
Mwalimu anafanya kazi 24 hrs,shule za boarding walimu wanakuwa na zamu za usiku.Kimsingi walimu wanapaswa kulipwa kama kada zingine,maana kada zote zinategemeana.Mfano: nesi akipigwa na mgonjwa wa akili lazime atafute msaada wa kisheria,wanataaluma wote hao wamepitia mikononi mwa waalimu.
Nashauri mishahara ingekuwa sawa ila marupu rupu yangetofautiana kulingana na mahitaji ya kada husika,sio swala la kutunishiana misuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…