Ramea
JF-Expert Member
- Mar 19, 2015
- 2,146
- 4,084
Ndugu walimu na wakufunzi wa shule za sekondari na vyuo tulioajiriwa 2011, tupeane machache hapa kuhusu hatma yetu ya kupanda madaraja kadiri ya taratibu za kiutumishi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2015.
Kiutaratibu tulitakiwa kupanda madaraja july 2014 lakini serikali kupitia TAMISEMI, Ilisema intake hii ya waajiriwa itapandishwa madaraja ifikapo july 2015. Nakumbuka naibu waziri TAMISEMI anayeshughulikia elimu Mh. Kassim Majaliwa alitembea mikoa mbalimbali Tanzania na katika ziara hii alithibitisha hili kwenye mikitano yake na walimu nchi mzima.
Cha kushangaza hadi leo halmashauri nyingi hazijatoa barua za kupandisha madaraja hadi sasa na haijulikani kama july hii tutapata mishahara mipya au la. Nadhani tunachezewa danadana na sababu za kutotoa barua had sasa ni zipi? kuna kitu hapa. Maana kuwa nayo tu ile barua hata mshahara usipobadilika, kuna faida kubwa kiutumishi.
Naomba tuutumie uzi huu kujuzana kama kuna halmashauri zilizotoa barau had kufikia leo hii.
KARIBUNI.
Kiutaratibu tulitakiwa kupanda madaraja july 2014 lakini serikali kupitia TAMISEMI, Ilisema intake hii ya waajiriwa itapandishwa madaraja ifikapo july 2015. Nakumbuka naibu waziri TAMISEMI anayeshughulikia elimu Mh. Kassim Majaliwa alitembea mikoa mbalimbali Tanzania na katika ziara hii alithibitisha hili kwenye mikitano yake na walimu nchi mzima.
Cha kushangaza hadi leo halmashauri nyingi hazijatoa barua za kupandisha madaraja hadi sasa na haijulikani kama july hii tutapata mishahara mipya au la. Nadhani tunachezewa danadana na sababu za kutotoa barua had sasa ni zipi? kuna kitu hapa. Maana kuwa nayo tu ile barua hata mshahara usipobadilika, kuna faida kubwa kiutumishi.
Naomba tuutumie uzi huu kujuzana kama kuna halmashauri zilizotoa barau had kufikia leo hii.
KARIBUNI.