Walimu wahitimu kukaa kita zaidi ya miezi 7 haipunguzi ufanisi?

NJALI

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
1,534
Reaction score
1,090
Mimi binafsi sirizishwi na hatua ya serikali sikivu ya CCM kuwakalisha kitaa wahitimu wa vyuo vya ualimu more than 7 months bila sababu za msingi. Hii inaweza kuwaathiri kisaikolojia, kiuchumi na hata kitaaluma. Sioni mantiki ya kufanya hivyo wakati kila siku serikali inawahadaa watanzania kuwa kuna uhaba mkubwa wa walimu!! Kwanini isiwape hata mkataba wa muda wakati wanaweka mambo sawa? Voda fasta wawo mbona walipatikana fasta na fungu likapatikana la kuwalipa? Acheni siasa kwenye elimu jamani.
 

Ukiamua kuajiriwa ni lazima ufuate matakwa ya mwajiri wako, la sivyo jiajiri mwenyewe.
Kuwa mvumilivu ndugu, kwenye sehem ya ufanisi sidhani kama utapungua labda uwe umefaulu kwa uwezo wa chabo.
 
Siyo tu kupunguza ufanisi lakini pia kutakuwa na upungufu mkubwa wa walimu watakao riport katika vituo vya kazi, sababu ikiwa ni kuamua kuweka mikataba na private schools na wengine wakihama kabsa sector na kufanya yao maana ikumbukwe Ualimu ni changuo la mwisho kabsa baada ya mtu kuwa amefeli kufanya aliyokuwa amepanga.

Kitakacho tokea Serikali itatangaza ajira za walimu 26,000 lakini kuna uwezekano wakariport 13,000 hasa Diploma na Certificate na Degree wachache waliosomea masomo ya sanaa (art).

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 

Waziri Jenister Mhagama fanya hima hawa walimu wapangiwe vituo. Mbona safari za wakubwa kuruka angani kama mbayuwayu pesa inapatikana? Mbona kigogo akiugua pesa ya kwenda india inapatikana? Au elimu sio kipaumbele cha jembe na nyundo yenu!
 

Kila mwaka serikali ikiajiri waalimu, 50% ya waalimu huripoti kazini, wengine haijulikani wanapo elekea.
 
Serikali haina pesa kwa sasa,vumilieni mpaka mwezi july.over
 
Mimi Sina Uhakika Lakini Nahis Tatizo Ni Hela Ya Kuwapa Hao Walimu Wapya...Kumbuka Serikali Nayo Inatamani Kuona Walimu Wanaajiriwa Lakini Itafanyaje Hela Hamna???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…