Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni jambo jema sana serikali kuwakata walimu mishahara. Tena 25,000/- isiwe mwezi mmoja. wakatwe miazi 3 ili seriakli ipate hela za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ajli ya maonyesho ya ccm kwenye chaguzi zijazo. Na kwa sababu watanzania wenyewe wakiwamo walimu ni wajinga wajinga tu, watakuwa wakipiga makofi na vigeregere pale wagombea wa ccm Tanzania nzima watakpokuw awakijinadi kwamba ccm imejenga shule na maabara tz nzima na hivyo kuleta maendeleo. Na hili halitakuwa ajabu ikiwa leo hii wanajivunia ujenzi wa barabara kwamba ccm imejenga wakati ni fedha za hao wajinga walalahoi wakiwemo walimu wanazolipa kama kodi, na kwamba hata mishahara ya wafanyakazi wote waliopo na wale wa hewa, wanalipwa na kodi hizi.
Kwa hiyo michango hii isimamiwe na jeshi la polisi ambao wawe na uwezo wa kupita fisi kwa ofisi na kufannya makusanyo ya michango hiyo kama kukata juu kw ajuu itakuwa ngumu.
Wale watakaohoji, wapigwe picha ili waitwe na kamati wahojiwe ili ifahamike adhabu yao sahihi ni ipi kati ya kufutwa kazi, kukolimbwa, kumwangosiwa, kufunguliwa mashtaka ya ugaidi, ama kung'olewa meno na kucha. Adhabu hizi zitekelezwe mapema kabla hawajaeneza sumu kwa wengine ili wabaki walimu misukule safi isiyo na midomo.
Lingine, ninadhani ni vizuri wakatambua seriakli sasa haina fedha kwa sababu ya matumizi makubwa yasiyotija na sasa inabidi ianze kunyag'anya misharaha ya wafanyakazi ili kuwekeza kwenye mipango ya seriakli ya maendeleo.
Deni la taifa limeongezeka kuliko kiwango na hatukopesheki tena na hivo lazima wachangie ili seriakli iweze kuendeshwa. Bahati mbaya kina Kafulila wameunguza picha na sasa wafadhili wanasita kutupa fedha zingine.
Lakini pia wanatakiwa walimu waonyeshe uzalendo kama washirika wakuu wa serikali ambayo inahitaji kuwa na fedha nyingi kwa ajil ya ccm ili ipate kuhonga vizuri wapiga kura katika chauguzi zijazo.
Kwa weli wlaimu mna mioyo yakuigwa na endeleeni na moyo huo huo!..
Misukule Hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!
Naomba kuuliza!Walimu na watanzania ni mijingamijinga tu umesema.Katika hiyo mijingamijinga ujue na baba,mama,shangazi na wajomba zako wamo wakiwa kama watanzania.Nakushauri kama una busara waombe radhi hao wazazi wako uliowatusi na siku nyingine usirudie kutukana wazazi wako.Sisi wengine huku tushakushusha thamani kwa kutokuweza kufikiri sawasawa ktk haya matusi.Kweli utubusara-ujingahasara.