Walinzi wa rais wetu fitness yao vipi?

Walinzi wa rais wetu fitness yao vipi?

Matumbo ya walinzi wa Tanzania ni makubwa mno sijui kama wanaweza kimbia.


swissme


Nakushauri, ukakwapue au ukachukue kitu cha Rais anapokuwa anatembea au katika jukwaa ndiyo utaelewa mbio zako na zao kuwa ni nani ana mbio.

Ila na wakati huo, naomba uwe umeisha gawa urithi au umetoa fedha zako zote kama unazo kule NMB aliposema mkululuo, tuzitunze ili tunaobakia tusitoane roho kwa mali unazoziacha kama baba wa familia.

Ni hayo tu.
 
Daaaahh kiukweli sijui kama mkulu yuko salama sana halafu Mara nyingi huwa wawili wakizidi wanne Jamaa wanene sana kiukweli wapunguze kula Akitokea MTU mwenye speed za Bolt sijui kwakweli MUNGU tuepushe na Balaa
 
acheni ujuaji kwenye ulinzi wa mkuu wa nchi,
mleta mada elewa kuwa ulinzi wowote hasa wa mtu mhimu kama rais uko katika ringi 'ring' kuu tatu mhimu hasa kulingana na mazingira aliyopo mlindwa(esp.rais)
1.Ringi ya tatu.
hii ni ringi ya nje ambayo ndio nguzo mhimu kabisa kwenye ringi zote zilizobaki, ringi hii inajumuisha nguvu kazi ya wanausalama hasa wa intelijensia ambao kazi yao kuu ni kunasa au kupeleleza usalama wa mazingira yaliyo karibu na rais na kutuma taarifa kwenye ringi ya kwanza na ya pili kupitia redio maalum za kiusalama ( huonekana wazi kwenye sikio mojawapo kwa walinzi kama earphone hivi) katika hali tulivu ringi hii haijumuishi silaha nzito bali ni nyepesi kama bastola n.k ila ktk hali isiyo salama huhusisha silaha nzito za kujihami aghalabu submachines kama UZI, AKs (fupi sana) n.k

2.Ringi ya pili
hii ni co-ordination ring kati ya ringi ya tatu na ya kwanza, ringi hii huundwa na kikosi cha kujihami na kushambulia chenye nguvu kazi ya maafisa wachache wenye uwezo wa juu kimapambano ( ELITE PERSONNELS), kazi kubwa ya ringi hii ni kupokea taarifa kutoka C yaani ringi ya 3 na kuzifanyia kazi iwapo inahitajika, mfano mhalifu anaweza kuhisiwa na ringi ya 3 na hivyo ringi ya 2 hujulishwa ili kuchunguza au kureact directly kwa adui, mfano adui anapohisiwa mkutanoni ambapo rais anahutubia nguvu kazi kutoka ringi ya pili humsogelea adui na kukaa naye karibu( kwenye kundi la watu) ili kuweka urahisi wa ku intercept mashambulizi kutoka kwa huyu adui, hii huundwa na nguvu kazi yenye uwezo mkubwa katika medani za kivita na intelijensia mf commandos.

1.Ringi ya kwanza,
Ringi hii ndio iliyozoeleka kuonekana machoni pa wengi, ni ringi inayojumuisha wanaoitwa 'VIP BODYGUARDS' ringi hii humjumuisha mpambe wa rais yaani ADC na nguvu kazi ya wabobezi wa close combat ambao ni commandos, kazi yao kubwa kudhibiti any physical contact kwa rais, wako alerted sana na hupokea miongozo toka kwa wanausalama toka ringi ya 2, na 3, kupitia redio,
Pia iwapo kutatokea fujo au jaribio kumdhuru kiongozi ringi hii hufanya kazi ya uokoaji ( rescue unit) na kumuondosha rais eneo hilo huku wakijbu mapigo na kuondoka nae huku wakiiacha ringi ya pili ikiendelea kudhibiti tishio kwa mapigano ya silaha, endapo mapigano hayo yatakuwa magumu ringi ya pili huhitaji msaada kutoka vyombo vingine vya usalama kama polisi na jeshi.
ikumbukwe kuwa ringi hii ya kwanza pia hubeba silaha ndogo(portable) zenye ufanisi zaidi.
ULINZI WA RAIS SI SUALA JEPESI WALA NADHARIA ZA KISIASA, NI UTENDAJI HALISI

Nb; RINGI HIZI NI KULINGANA NA HALI, SIFA, YA ENEO HUSIKA INAWEZA IKAZIDI HAPO

THAKS, HAVE IT THOUGH SOME OF IT!

Safi kwa.nondo Kali hii.
 
Daaaahh kiukweli sijui kama mkulu yuko salama sana halafu Mara nyingi huwa wawili wakizidi wanne Jamaa wanene sana kiukweli wapunguze kula Akitokea MTU mwenye speed za Bolt sijui kwakweli MUNGU tuepushe na Balaa

Acha kujiogopesha, hao jamaa ni moto wa gesi usicheze na hiyo kitu.

Ni bora ukachezee chui au simba kule mbuga za.Serengeti na siyo hao . Utakufa ukijiona aisee.
 
Mwingine alipiga KARATE siku ya uhuru, wanasema ni mwl wa makomandoo na ANABONDA kichizi pamoja na kwamba ana kitambi cha hatari.

Nb"Sijabisha kwamba anabonda balaa.
Hayo majamaa yana vitambi lakini mepesi kinyama
 
Ndugu wana jamvi
Ningependa kujadili masuala haya makubwa mawili

1. Nakumbuka kipindi cha kampeni rais alikuwa na vijana wanamlinda akiwa bado hajawa rais cha kushangza ni kuwa baada ya kupata nafasi hiyo vijana wale wale wameendelea kuwa walinzi wake, ningependa kuhoji ubora wao katika maswala ya ulinzi.

2. Kama tujuavyo ulinzi wa rais unahitaji umairi mkubwa ila cha kushangaza ni kuwa walinzi w rais wengi ni wenye vitambi na nyama zembe je wapo vizuri kwa mapambano kama ikihitajika?

Ukweli ni kuwa walinzi hawa wanaonekana kuwa wachovu na wasio jua mambo ya kiulinzi na mapambano. Tujadiliane


Aiseee,

Wewe umeisha fariki japo bado unatembea kama hayo ndiyo mawazo yako .
 
Amenena vyema ila hajajibu swali langu la ubora wa walinzi wetu

Hao jamaa,. Ni bora.ukachezee simba na chui pale Serengeti ila.siyo hao.

Na ukumbuke, hao hawafundishwi kupiga bali ni kuua tu , akikupiga ukapona hilo anakuwa amekosea sana, kwa mikono, siraha, kung"oa kucha bila ganzi mbio na n.k.
Is.kumbuka, wana vitengo vingi pia.
 
Mzee Mwinyi aliposhambuliwa alikuwa analindwa na watu gani? Kinachowasaidia viongozi wetu ni utulivu na nidhamu ya Watanzania.
Lkn natabiri, kwa matendo ya viongozi wetu wa leo, siku zinakuja tutaanza kuona wakishambuliwa...

Unaarika msiba nyumbani kwenu au nyumbani kwako.
Toa tu urithi ili usiache vita home/ nyumbani kwako ya kugombea Mali mfano , gari, nyumba , mashamba , n.k .
 
Mzee Mwinyi aliposhambuliwa alikuwa analindwa na watu gani? Kinachowasaidia viongozi wetu ni utulivu na nidhamu ya Watanzania.
Lkn natabiri, kwa matendo ya viongozi wetu wa leo, siku zinakuja tutaanza kuona wakishambuliwa...

Unaarika msiba nyumbani kwenu au nyumbani kwako.
Toa tu urithi ili usiache vita home.
 
Kwa muda sasa nimekuwa nikifuatilia Kwa umakini muonekano wa walinzi wa rais wetu mpendwa ukilinganisha na walinzi wa Marais wengine

Katika kufatilia huko nimegundua kuwa muonekano wa walinzi wa Marais wengine ni wa kikakamavu sana ukilinganisha na walinzi wa Marais wetu hapa tanzania ambao ni watu wazima hv wenye vitambi vyao ambao wananipa shaka kama wanaweza kukurukakara za kukabiliana na mtu mkakamavu au mbio za kukimbizana na mhalifu anayetoroka,nimejaribu kuweka picha za walinzi wa Marais mbalimbali na hawa wa kwetu mjinee.

Karibuni wadau mchangie mnauonaje monekano wa walinzi wetu wa rais na kama unakidhi mahitaji ya unyeti wa kazi yao.
fb7c9b2738e6778f9aed2032f906170d.jpg
6570690413ab8d7a85875c7e88450598.jpg
e64ed5027ecf9d9d306536146ca4f181.jpg
cc32319f0cdca3be5b42367f3568e392.jpg
a136d6739cd96780537f29cdbc387582.jpg
bcf673b8cb295cee2be67913f9bbe88d.jpg
7415a0e13b58ca090e55e18a5fbdadd6.jpg
7bebe71c99da2725de08fe07acfffa3b.jpg
aa54520e6f8c2216765b8aab1164d954.jpg
37c07be31bd74ffea1cedb2c4b9f193a.jpg
57cbdf148150eb6fdbf3795800ec381a.jpg
da82b071800d9795a3cc37f0792246a1.jpg
c46e702012fe044456fe4b4b0d297229.jpg
Nakushauri wee nenda kawajaribu ili uijue fitness yao ilivyo maana vyakuambiwa bado hutaviamini na usiogope kuijarbu sheria
 
Namkubali capten Mrope, alipigwa na ubao mwili mzima pale uwanja wa taifa hata damu hakutoka, yaani mkomao balaa.
 
Back
Top Bottom