Waliojaribu kumteka Tarimo walitaka kumlawiti na kumsababishia maumivu. Kesi kuendelea Februari 24, 2025

Waliojaribu kumteka Tarimo walitaka kumlawiti na kumsababishia maumivu. Kesi kuendelea Februari 24, 2025

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Screenshot_20250212_203054_Instagram.jpg

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.

Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.

Pia soma: Kesi ya waliojaribu kumteka Tarimo kuendelea Januari 21, 2025 baada ya jalada kutokuwepo Januari 9. Ni mara ya pili mfululizo kukwama

Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.

Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.

Washtakiwa walikana mashtaka dhidi yao huku Anitha akikataa jina lake maarufu la Jack. Mahakama ilikubali ombi la kubadilisha shtaka kutoka "jaribio la utekaji" hadi "utekaji nyara" baada ya ushahidi mpya kuwasilishwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 24, 2025, kwa ajili ya kusikilizwa zaidi.
 
Wakuu,

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.

Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.

Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.

Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.
Kumbe kwenye hili tukio jeshi letu la polisi walionewa tu bure. Matukio mengi ya haya utekaji ni dhulma na kugongeana wake, michepuko na madem za watu. Lakini pia jeshi letu siyo eti wasafi kivile nao wanahusika na mengine.

Nyau de adriz
 
Wakuu,

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.

Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.

Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.

Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.

Washtakiwa walikana mashtaka dhidi yao huku Anitha akikataa jina lake maarufu la Jack. Mahakama ilikubali ombi la kubadilisha shtaka kutoka "jaribio la utekaji" hadi "utekaji nyara" baada ya ushahidi mpya kuwasilishwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 24, 2025, kwa ajili ya kusikilizwa zaidi.
Yani huyo kijana mdogo Frenk Nsato miaka 21 tu naye mtekaji.
 
Kumbe kwenye hili tukio jeshi letu la polisi walionewa tu bure. Matukio mengi ya haya utekaji ni dhulma na kugongeana wake, michepuko na madem za watu. Lakini pia jeshi letu siyo eti wasafi kivile nao wanahusika na mengine.

Nyau de adriz
hao ni polisi! sema msala umewakuta kwa hiyo wamewaruka tu!
 
Kumbe kwenye hili tukio jeshi letu la polisi walionewa tu bure. Matukio mengi ya haya utekaji ni dhulma na kugongeana wake, michepuko na madem za watu. Lakini pia jeshi letu siyo eti wasafi kivile nao wanahusika na mengine.

Nyau de adriz
Mkuu hao polisi wanajitakia wenyewe. Wangekuwa ni watu wasafi haya ya kuhisiwa yasingetokea.
 
Wakuu,


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.

Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.

Pia soma: Kesi ya waliojaribu kumteka Tarimo kuendelea Januari 21, 2025 baada ya jalada kutokuwepo Januari 9. Ni mara ya pili mfululizo kukwama

Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.

Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.

Washtakiwa walikana mashtaka dhidi yao huku Anitha akikataa jina lake maarufu la Jack. Mahakama ilikubali ombi la kubadilisha shtaka kutoka "jaribio la utekaji" hadi "utekaji nyara" baada ya ushahidi mpya kuwasilishwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 24, 2025, kwa ajili ya kusikilizwa zaidi.
Kumbe🙆
 
Kumbe kwenye hili tukio jeshi letu la polisi walionewa tu bure. Matukio mengi ya haya utekaji ni dhulma na kugongeana wake, michepuko na madem za watu. Lakini pia jeshi letu siyo eti wasafi kivile nao wanahusika na mengine.

Nyau de adriz
Ukiona wahusika wanahukumiwa basi jua hawakua na mkono wa polisi.

Wale watu wasiojulikana ndio huwa na mkono wa polisi.
 
Du. Hivi wale kumbe hawakuwa polisi? Inaonekana kulikuwa na issues nyingine eg kudaiana au kuchukuliana wanawake hivyo wakapanga kumkomoa. Huu ni ujinga wa hali ya juu na wanatakiwa wapate adhabu kali kama ikidhibitika.
Kuna uwezekano mkubwa walikua polisi maana walijaribu kumfunga pingu, sio rahisi raia kuwa na pingu. Uenda sio wote ni polisi lakini possibly kulikua na polisi angalao mmoja kati yao
 
Ningekuwa mimi hakimu ningeamrisha wasababishiwe maumivu kama waliyokusudia kusababisha kwa bwana Tarimo.
 
Back
Top Bottom