Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.
Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.
Pia soma: Kesi ya waliojaribu kumteka Tarimo kuendelea Januari 21, 2025 baada ya jalada kutokuwepo Januari 9. Ni mara ya pili mfululizo kukwama
Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.
Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.
Washtakiwa walikana mashtaka dhidi yao huku Anitha akikataa jina lake maarufu la Jack. Mahakama ilikubali ombi la kubadilisha shtaka kutoka "jaribio la utekaji" hadi "utekaji nyara" baada ya ushahidi mpya kuwasilishwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 24, 2025, kwa ajili ya kusikilizwa zaidi.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.
Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu kama Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.
Pia soma: Kesi ya waliojaribu kumteka Tarimo kuendelea Januari 21, 2025 baada ya jalada kutokuwepo Januari 9. Ni mara ya pili mfululizo kukwama
Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa washitakiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.
Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha kama polisi.
Washtakiwa walikana mashtaka dhidi yao huku Anitha akikataa jina lake maarufu la Jack. Mahakama ilikubali ombi la kubadilisha shtaka kutoka "jaribio la utekaji" hadi "utekaji nyara" baada ya ushahidi mpya kuwasilishwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 24, 2025, kwa ajili ya kusikilizwa zaidi.