Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Akiongea katika zoezi hilo Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed amesema kuwa kikosi hicho kilitangaza zoezi hilo ambapo ameweka wazi kuwa wameanza operesheni za ukamataji wa magari ambayo haya jakaguliwa na kikosi hicho.
Ameongeza kuwa takwimu zinaonyesha kuna zaidi ya magari 563 ambayo yanatoa huduma kwa wanafunzi ambapo baada ya ukaguzi huo inaonesha bado magari 178 huku akiweka bayana kuwa kuanzia leo Januari 13,2025 wameanza kuwamata madereva waliokaidi ukaguzi huo.
SSP Zauda akatumia fursa hiyo kuwataka wamiliki na madereva kupeleka magari yao katika kikosi cha usalama barabarani ili kufanya ukaguzi na kuweka mazingira salama ya watumiaji wa vyombo hivyo ambao ni wanafunzi huku akisisitiza kuwa watakaoendelea kukaidi watachukuliwa hatua za kisheria.
Pia akatoa wito kwa madereva kutambua kuwa kuna kundi jipya la watumiaji wa Barabara akiwataka kuchukua tahadhari na kufuata sheria za usalama barabarani ili kundi hilo liendelee kuwa salama kipindi chote.