Waliolipwa madai ya kukosa ajira NSSF

Waliolipwa madai ya kukosa ajira NSSF

Ni muda wowote tu unafungua ila angalizo kama ukipeleka maombi baada ya miezi sita ya ukomo wa mkataba wako wa ajira utatakiwa kuandika barua ya kuomba kibali cha kufungua madai kwa Meneja wa NSSF wa mkoa husika unaofungulia maombi. Mfano wa barua utaikuta kwenye ubao wa matangazo wa NSSF.
Asante mkuu, kuna bwana mdogo walisitisha ajira yake mwezi wa tano kutokana na taasisi aliyokuwa akifundisha kufilisika. Lakini pia kwenye michango yake Kuna miezi kadhaa haikulipwa. Hili nalo linaweza kuwaje. Maana yupo radhi apewe kilichopo maana muajiri uwezekano wa kuweza kulipa Ni Kama haupo au Kama atakujaweza kulipa sio Leo wala kesho.
 
Asante mkuu, kuna bwana mdogo walisitisha ajira yake mwezi wa tano kutokana na taasisi aliyokuwa akifundisha kufilisika. Lakini pia kwenye michango yake Kuna miezi kadhaa haikulipwa. Hili nalo linaweza kuwaje. Maana yupo radhi apewe kilichopo maana muajiri uwezekano wa kuweza kulipa Ni Kama haupo au Kama atakujaweza kulipa sio Leo wala kesho.
Kulipwa atalipwa kilichopo kwenye michango yake, kwa maana akiulizwa kuhusu michango mingine atawaeleza hali halisi wakiona haitoshi watawapigia simu waajiri wake.
 
Samahani inakuwaje mtu analipwa nusu ya kiasi cha mafao aliyonayo
Mkuu kuna kulipwa nusu (50%) ya michango yako endapo umechangia chini ya miezi mitano na ikiwa ulikuwa unafanya kazi za kitaaluma, lakini kuna kulipwa kiasi kilichopo ikiwa michango yako haijakamilika hivyo unaomba ulipwe kiasi hicho waati ukisubiri michango mingine kukamilishwa
 
Nssf wako vizur kwenye malipo aisee wamenyooka...ila kimbembe kipo psspf ....wagaigai..
 
Habari yako kiongozi? Mara nyingi haya madai hulipwa ndani ya wiki sita kama documents zote zipo na hazina shaka, na kila hatua jinsi faili linavyoshughulikiwa kama umejiunga na huduma ya NSSF online unakuwa unaona kipi kinachoendelea na mpaka faili likiwa APPROVED na siku ya kulipwa pia inaonekana. Vilevile ukishaingia hapo kwenye USER-PORTAL upande wa STATUS kwa kipengele cha CLAIMS DETAILS ukiona wameweka neno LODGING hapo ujuwe faili lako limeanza kufanyiwa kazi. Likitoka kuwa LODGING linakuja kuwa APPROVED baada ya hapo inakuwa PAID. Usivunjike moyo Kiongozi pesa yako utaipata tu kwani si walikupa tarehe ya kurudi tena iwapo pesa yako itakuwa bado haijaingia kwenye akaunti? Mara nyingi huwa ni kipindi cha matazamio cha miezi miwili, lakini hiyo miezi miwili huwa haifiki inacheza kwenye wiki sita hadi saba. Endelea kuwa na subira kiongozi, nakutakia siku njema.
Na inakuwaje mtu amesubmit madai nssf then kuingia nssf portal akakuta benefit claim status paid, lakini hela haijaingia kwenye bank akaunti 🤣🙉
 
Na inakuwaje mtu amesubmit madai nssf then kuingia nssf portal akakuta benefit claim status paid, lakini hela haijaingia kwenye bank akaunti 🤣🙉
Hiyo huwa ni kawaida kutokea kwani Mara nyingi huwa ni masuala ya kibenki zaidi, yawezekana checque ikawa imepelekwa lkn ikawa bado haijawa cleared na bank husika.
 
Nimefungua madai tr 9 mwezi wa kwanza mwaka 2023 lakini mpaka chapisho ilii hamna majibu yoyotee Kila nikiingia kwenye app Yao michango yote ipo tatizo ni nini hapo wakuu na ni vipi naweza fatilia faili langu la madai Ili kujua niwapi limekwama?
 
Back
Top Bottom