Waliopanda ndege ya Mama kwenda Algeria ni mashabaiki wa Yanga SC au wavaa suti tu wanaokwenda kutalii na kupiga selfie?

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Nitangulize kutoa baraka na kila la heri kwa Yanga SC katika mpambano wa marudiano huko Algeria.

Kongole kwa Mh. Raisi kwa kutoa ndege ya mashabiki na wadau wa mpira kwenda kuisapoti Yanga SC.

NALIA NGWENA najiuliza hao mashabiki waliopanda ndege ni mashabiki wa kuleta morali/kushangilia muda wote au ni mashabiki wa kuvaa suti na kupiga selfii (watalii)?

Nitasikitika sana kama mashabiki lialia/wenye morali ya kushangilia endapo watakua wameachwa.

Nawasilisha hoja.
 
Kk ishu sio kupanda ndege tu, una PASSPORT? Una hela ya kufikia Hotelini?
Serikali imelipia NAULI TU.
Gharama zingine ni zako.

Kabla ya kulaumu muelewe hilo kwanza.
Mashabiki wote wale wanaoambatana na timu wameenda labda wale walikosa passport na pesa za kujikimu, au mlitaka nazo watoe Serikali?
 
Timu haina fungu la kuchukua angalau mashabiki kazaa??

Kuna mashabiki Lia Lia wa timu kila timu inaposafiri hao wapo na timu imechukua shilingi ngapi hela za mama haiwezi kumudu angalau hata mashabiki kadhaa.
 
Mbona wamekuacha mkuu?
 
Ukitaka upande ndege iliyotolewa na Rais wenu uwe na vifuatavyo:
1. CONNECTION

2. Passport
3. Hela ya Hotel
4. Covid 19 Vacvine Certificate


La muhimu kuliko yote ni CONNECTION baba.
Kuna mashabiki wengi pasport wanazo lakini Hilo zali limeishia juu juu tu.
 
Timu haina fungu la kuchukua angalau mashabiki kazaa??

Kuna mashabiki Lia Lia wa timu kila timu inaposafiri hao wapo na timu imechukua shilingi ngapi hela za mama haiwezi kumudu angalau hata mashabiki kadhaa.
Fungu la nini? Mashabiki wote wana haki sawa, yaani timu iweke fungu la kuwalipia mashabiki? Wakijaa pale jangwani utambeba nani?
 
Kuna washabiki wanachama lia lia wako team popote wake ndio wapewe kipaumbele
 
ndugu yng unategemea mashabiki ndo watatuokoa kwenye hii game!!!kule kipigwe tu hatuwezi kwenda na mashabiki watakaohamasisha wachezaji uwanjani coz hatutapata room ya mashabiki wengi wa ivyo uwanjani...ILA NAHISI TUNATOBOA HII GAME
 
Kuna watanzania wengi wanasoma huko Algeria, hili zoezi la kwenda na ndege ya Air Tanzania wala kupeleka mashabiki halikuwa na umuhimu, ni ubadhilifu tu wa mali za umma.

Serikali kama ilitaka kusaidia ingelipia baadhi ya gharama za usafiri wakaenda na mashirika mengine kama kawaida, gharama zingekuwa chini zaidi kuliko kurusha ndege halafu ikapaki siku 4 pale Algiers (na hata hili halina ulazima maana CAF wanatoa mafungu ya kutosha kulipia gharama hizi za usafiri).

Kule Misri mechi na Uganda hatukupeleka mashabiki, waliopo kule wakaja kushangilia tukashinda. Tulivyorudiana hapa Dar, tukapitisha zoezi la kununua tiketi, uwanja ukajaa tukafungwa. Akili kumkichwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…