Waliopokea Chanjo ya AstraZeneca ya India kunyimwa pasi maalum ya kuingia Ulaya

Waliopokea Chanjo ya AstraZeneca ya India kunyimwa pasi maalum ya kuingia Ulaya

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Pasi maalumu ya Umoja wa Ulaya, itakayoanza kutumika tarehe 1 mwezi Julai kurahisisha safari kwenda Ulaya kwa wale waliopata chanjo itaanza kufanya kazi lakini ikiwa na sharti moja muhimu.

Mtu yeyote aliyepewa chanjo ya AstraZeneca inayozalishwa na Taasisi ya Serum ya India hatastahiki kupata pasi hiyo- na hiyo inajumuisha raia wengi wa nchi za kipato cha chini na cha kati ambao walipatiwa chanjo zilizosambazwa na mpango wa COVAX uliofadhiliwa na WHO.

Hii ni kwasababu pasi maalumu ya Umoja wa Ulaya itatambua tu toleo la Vaxzevria la chanjo ya AstraZeneca ambayo ilitengenezwa nchini Uingereza au maeneo mengine ya Ulaya, na hivyo kupitishwa na Wakala wa Dawa wa Ulaya (EMA). Kwa upande mwingine, ununuzi na usambazaji mkubwa wa chanjo chini ya mpango wa COVAX unahusisha chanjo ya AstraZeneca, iliyotengenezwa na Taasisi ya Serum ya India.

Wakati hayo yakijiri, Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametahadharisha uwepo "ubinafsi wa chanjo" ulimwenguni lakini akasema "itawaamsha" Waafrika kujitosheleza.

Rais Museveni amesema kuwa Afrika wanahitaji malighafi kuzalisha chanjo zao wenyewe na sio michango ya chanjo kutoka nchi zilizoendelea.

‘’Ni aibu kwetu sisi Waafrika. Kwanini tutegemee kila kitu kutoka nje. Hii ni aibu kwa Afrika, ‘’ aliwaambia wajumbe waliohudhuria mkutano wa Shirika la Afya duniani, Jumapili.

Rais Museveni alisema kuwa nchi za bara la Afrika zinapaswa kuacha kusubiri chanjo za misaada na kutengeneza zao wenyewe.
‘’Ubinafsi duniani ni mbaya, lakini ni vizuri. Ninaupenda kwa kuwa unawaamsha Waafrika. Ni aibu kwa bara zima la Afrika limelala, likisubiri kuokolewa na wengine kama ilivyotokea wakatu wa biashara ya utumwa,’’ alisema.

Rais Museveni amesema Uganda ilikuwa kwenye mchakato wa kutengeneza Chanjo yake yenyewe na ilikuwa inahitaji tu msaada wa malighafi akisema,‘’Msiwe na shaka tutanunua. Hatuhitaji msaada.’’

1624874208416.gif
 
Kwa hiyo Mbowe aliuziwa mbuzi kwenye gunia, si walimchanja hiyo hiyo ya Astrazeneca ?🤣
 
Kuna taarifa ilizagaa mzee mgonjwa kapelekwa kenya tena imekuaje? Au mm sjaelewa mwenye kujua zaidi anipe jibu.
 
mammae hapa ndio utajua rangi halisi ya mzungu,ni njano au nyeupe???

kwamba hoja hapa sio chanjo tena,ila inazalishwa wapi.
 
Ha ha ha, nilisema siku nyingi hapa hizi ni biashara za watu.
 
Waliochanjwa chanjo ya Astrazeneca ni marufuku kuingia nchi za Ulaya kwa sababu chanjo hiyo inayozalishwa India haijasajiliwa!
Ikumbukwe nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Kenya tayari zimeshachanja watu wake na zinaendelea kuchanja kwa chanjo ya Astrazeneca.

Source : BBC
 
Ina maana India walianza kutumia hiyo chanjo worldwide bila kupata ruhusa toka WHO?

Hii itakuwa inasababishwa na mambo ya kibiashara tu, wazungu wana visa sana.
 
Waliochanjwa chanjo ya Astrazeneca ni marufuku kuingia nchi za Ulaya kwa sababu chanjo hiyo inayozalishwa India haijasajiliwa!
Ikumbukwe nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Kenya tayari zimeshachanja watu wake na zinaendelea kuchanja kwa chanjo ya Astrazeneca.

Source : BBC
Aya shangilia sasa wewe kima wa CCM lumumba
 
Waliochanjwa chanjo ya Astrazeneca ni marufuku kuingia nchi za Ulaya kwa sababu chanjo hiyo inayozalishwa India haijasajiliwa!
Ikumbukwe nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Kenya tayari zimeshachanja watu wake na zinaendelea kuchanja kwa chanjo ya Astrazeneca.

Source : BBC
Astrazenica ya India.

Hivi tuulize kuna chanjo 9 wale mbwa wa WHO wameizinisha chanjo za Ulaya na Marekani tuu.Swali je hizo nchi zenye chanjo zao hawaruhusiwi kuingia Ulaya na Marekani?

Maana Hawa mbwa wa kizungu wanataka wajimilikishe biashara ya Chanjo
 
Chanjo zote zinazotumika duniani lazima ziwe zimeidhinishwa na WHO....kama unachanjo ambayo haijasajiliwa na WHO maana yake ni fake hiyo..... Hata leo ukianza utafiti kwa ajili ya dawa au chanjo kwa ugonjwa wowote na una intention itumike dunia nzima lazima uisajili WHO na kushare kila hatua ya utafiti wako n mwisho lazima uithibitishe kwa WHO kama inafanya kazi na wao lazima wajilidhishe.....Kama hiyo ya INDIA haijasajiliwa WHO basi haifai kuwepo mtaani...
 
Waliochanjwa chanjo ya Astrazeneca ni marufuku kuingia nchi za Ulaya kwa sababu chanjo hiyo inayozalishwa India haijasajiliwa!
Ikumbukwe nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Kenya tayari zimeshachanja watu wake na zinaendelea kuchanja kwa chanjo ya Astrazeneca.

Source : BBC

Tofautisha waliochanjwa chanjo AstraZeneca na AstrsZeneca kutoka India.

Hii inawahusu waliochanjwa ya kutokea India tu.
 
Chanjo zote zinazotumika duniani lazima ziwe zimeidhinishwa na WHO....kama unachanjo ambayo haijasajiliwa na WHO maana yake ni fake hiyo..... Hata leo ukianza utafiti kwa ajili ya dawa au chanjo kwa ugonjwa wowote na una intention itumike dunia nzima lazima uisajili WHO na kushare kila hatua ya utafiti wako n mwisho lazima uithibitishe kwa WHO kama inafanya kazi na wao lazima wajilidhishe.....Kama hiyo ya INDIA haijasajiliwa WHO basi haifai kuwepo mtaani...
Hizo data za utafiti za chanjo zilizotengenezwa na mabeberu ziko wapi? acha uzwazwa wa kuhoroja kama kasuku...
 
Hizo data za utafiti za chanjo zilizotengenezwa na mabeberu ziko wapi? acha uzwazwa wa kuhoroja kama kasuku...

Ingia website ya WHO kaangalie kila chanjo na dawa iliyosajili na hatua iliyofikia kwenye utafiti... hapo inaongelewa status au stages ya utafiti...
 
Back
Top Bottom