Walioshambuliwa na wanyama walilia kifuta machozi

Walioshambuliwa na wanyama walilia kifuta machozi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Wananchi Wilaya ya Sengerema wamelalamikia idara ya wanyamapori kutokuwalipa kifuta machozi watu waliopoteza maisha na wengine kujeruhiwa baada ya kuliwa na wanyama wakali tangu mwaka 2019 hadi mwaka 2020.

Mmoja wa waathiriwa hao, Sanda Deus anayeishi Kijiji cha Nyamasale kata ya Busisi Wilayani humo aliyejeruhiwa mguu na mamba wakati anaogelea ziwa Victoria Agosti 17, 2020 amelalamika kutokupa kifuta machozi hadi Sasa.

Amesema licha ya taarifa zake kufikishwa idara ya Maliasili wilaya ya Sengerema tangu alipopata dhahama hiyo hadi sasa hajapata chochote.

“Tunaziomba mamlaka husika zitusaidie ili tupate kifuta machozi," amesema Deus alipozuingumza na Mwananchi wilayani humo.

Ofisa Maliasili wilayani humo, Paul Pontian amesema tangu mwaka 2019 hadi mwaka 2020, watu watano wamepoteza maisha kwa kuliwa na mamba na mmoja amejeruhiwa huku mbuzi 12 na kondoo 3 wameliwa na fisi.

Amesema taarifa hizi amekwisha zifikisha ofisi ya wanyamapori Kanda ya Ziwa nab ado anasubiri taratibu za malipo ya watu hao.

Kwa upande wake ofisa wanyamapori Kikosi cha Kupambana na Ujangili Kanda ya Ziwa, Godifrey Raisi amesema suala hilo wanalifanyia kazi na wahanga hao watalipwa kifuta machozi hicho.

MWANANCHI
 
Mamlaka husika inunue leso za kutosha Kama kifuta machozi kwa waathirika

Nawasilisha
 
Na yule aliekua anaogelea kwa starehe zake mwenyewe nae kadai fidia jamann
 
Back
Top Bottom