Walioshindwa maisha mjini tukutane hapa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mimi nilikuwa fundi rangi lakini sasa kazi za kupaka rangi zimepungua Sana, nina mke, watoto wawili na wazazi wote wako hai wananitegemea. Kodi ya chumba, chakula na maji na umeme vimeninda.

Nifanye kazi gani ingine au nirudi kijijini nilikotoka?
 
Jemedari alishasema ikifika July bado uko mjini wewe mwanaume.
 
Na bado Jiwe ana zaidi ya miaka 6 from now.Watu watanyooka.Na kwa mwendo huu ikifika 2025 anaeza kugoma kutoka kama kina Nkurunziza.Kuna watu mpaka muda huo wasipojiongeza watakua hoi
 
Mjini unashindwaje maisha mkuu. Haja nenda kalime sasa
Nipe maujanja mkuu mbali na rangi nifanye kitu gani ili niendelee kuwepo mjini?

Kazi ya kupaka rangi imenibumia, watu wepunguza kujengga na viwanja vinakoposhwa siku hizi malipo ni kwa kidogokidogo.
 
Sentesi tata "wazazi wote wako hai wananitegemea"
hukuelewa nini hapo? ni wazee sana hawana uwezo, nilikuwa napiga rangi kupata riziki yangu na yao pia. Akili yako.....
 
hukuelewa nini hapo? ni wazee sana hawana uwezo, nilikuwa napiga rangi kupata riziki yangu na yao pia. Akili yako.....
"Bado wako hai" ndio utata, ulitakaje kwa kusema bado wapo hai?
 
Mimi nilikuwa fundi rangi lakini sasa kazi za kupaka rangi zimepungua Sana, nina mke, watoto wawili na wazazi wote wako hai wananitegemea. Kodi ya chumba, chakula na maji na umeme vimeninda.

Nifanye kazi gani ingine au nirudi kijijini nilikotoka?

Mathayo : Mlango 11

28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
 

Attachments

  • 36663295_651992365163836_5072768388493737984_n.jpg
    24.1 KB · Views: 20
Tumia simu yako,tafuta scoops ukawauzie kina Eric shigongo
 
Mjini ukiweza kuhudumia tumbo tu inatosha,pakulala hata kibarazani kwa mama bite panatosha
Ni mwendo wa kuridhisha tumbo tu usife....hayo mengine yatajijuuu
 
Mkeo ana ujuzi gani? Kwanini msisaidiane kutafuta?
Hilo ndilo balaa kabisaa, "mpemba" na rafiki zangu wenye ahueni kifedha wanaitumia hali yangu kumnyapia wife. Nikitoka kuhangaika huko na huko wao wanahamia kwa shemeji yao kumjaza ujinga. Naona iko siku tutakufa kwa maradhi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…