Waliotaka kuiba kwenye ofisi za Betting Dar wafariki dunia

Waliotaka kuiba kwenye ofisi za Betting Dar wafariki dunia

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Vijana wawili waliodaiwa kuvamia ofisi ya michezo ya kubahatisha (Premier bet) eneo la Mwenge ITV na kutaka kupora fedha wamefariki kutokana na kipigo walichokipata kutoka kwa wananchi.

Septemba 27, 2022, saa 3:30 asubuhi vijana hao walifika katika ofisi hiyo kama wateja wanaohitaji huduma na kuanza kumshambulia mhasibu kwa kumpiga na jiwe kichwani huku mwingine alijaribu kuvunja shelfu zilizokuwa na fedha bila mafanikio.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema watuhumiwa hao walifariki baada ya kufikishwa hospitalini.

Amesema kifo chao kinetokana na kipigo walichokipata kutoka kwa wananchi, baada ya kuchoshwa na vitendo vya kihalifu.

"Watuhumiwa wote wawili kwa bahati mbaya baada ya kufikishwa hospital walifariki, baada ya kufuatilia tumebaini kijana mmojawapo alikuwa ametoka gerezani miezi minne iliyopita," amesema Muliro.

Aidha, Kamanda Muliro amewataka watuhumiwa wanaotoka gerezani, kwa kumaliza kifungo au kwa msamaha kufuata sheria na kuachana na vitendo vya kihalifu kwani wananchi wamechoka na vitendo hivyo. Hata hivyo, Jeshi hilo linaendelea na operesheni usiku na mchana.

MWANANCHI
 
Ipitishwe tu sheria ujambazi au uporaji kwa kutumia silaha, kitu chenye ncha kali, na zana yoyote inayoweza kufisha, adhabu yake ile ni kifo tu.
 
Vipi huyo dada aliyepigwa jiwe na hao panya road, hali yake inaendeleaje? Maana jana tuliambiwa wakati wananchi wanawashughulikia hao vibaka, huyo dada alikimbizwa haspital! Kweli vibaka hawana huruma, wako radhi kupoteza maisha ya mtu ilimradi wafanikishe wizi wao!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Abdul nondo akafuatilie uchunguzi wake atuletee hapa tuone
 
Mwizi akikamatwa eneo la tukio apate kipigo cha kutosha hadi ajambe cheche.
Ubaya ni kumsingia mtu kitu ambacho hajafanya na kumpiga.
Vijana fanyeni kazi vitu vya bure bure hakuna mtakufa midomo wazi.
 
Mob justice, hatuko mbali na yanayotokea hapo SA,sasa police watawatafuta waliofanya hii mob justice?,tunaishi in a shithole country, wapi sheria za nchi?
 
Back
Top Bottom