Walipiza kisasi cha kuua kijana baada ya mwenzao kuuawa na sungusungu Mburahati

Walipiza kisasi cha kuua kijana baada ya mwenzao kuuawa na sungusungu Mburahati

Lady Mwali

Senior Member
Joined
Nov 15, 2018
Posts
147
Reaction score
333
Wanabodi,
Siku za nyuma niliweka thread kuhusu mauaji ya kijana Jumanne Jongo kuuawa na sungusungu maeneo ya Beach Boy Mburahati.Kijana huyu anaishi maeneo ya Banda Mabibo.
Kijana aliyeuawa anaitwa Abdu ana umri wa miaka 19.
Kilichotokea ni kwamba kijana aliyeuawa alikwenda kwenye mziki maeneo ya Banda.Huyu kijana anakaa maeneo ya Bongo Beach alipouawa Jumanne Jongo.

Baada ya kufika katika mziki huo kwenye sherehe ya ushindi wa bondia wa Banda, mabaunsa walimuona huyo kijana wakaanza kumshambulia kwa kumpiga visu maeneo mbalimbali ya mwili,kooni,tumboni na kichwani.

Kijana alifia hospitali ya Mwananyamala baada ya kuvuja damu nyingi.

Sungusungu walichukua sheria mkononi kwa kuua kijana Jongo
wahuni wa Banda nao wamelipiza kisasi kwa kumuua huyu kijana anayehisiwa yeye au baba yake walihusika katika mauaji ya Jongo kwa kivuli cha
sungusungu.

Hii inatokana na uhasama mkubwa uliopo kwa wakazi wa maeneo haya dhidi ya sungusungu.

Hatujui atafata nani, ila hao sungusungu wa Jitegemee na Mburahati waache kiherehere kwani wako hatarini kushambuliwa na hawa wahuni wa Banda na kuuawa.

Kuna haja kuwe na upatanisho kati ya sungusungu na vijana wa Banda, bila hivyo maafaa yatatokea zaidi.
 
Du Banda n mitàa ya nyumban kabisaa..jumanne Ni kijana nnaemfahamu tangia akiwa na umri wa miaka mitano..na Mama ake mzaz namfahamu babu yake pia na rafiki zake kina marehemu Sande...inshort hakuna haja ya visasi..naomba wakae chini wayamalize tu..mana revenge haiwez kuwa dawa...

Leo anakufa huyu kesho anakufa yule...mwisho wa siku vijana wataisha..
 
Kitu kama hiyo imetokea maeneo ya Goroka karibu na Toangoma ila Sungusungu walikimbia... Ugomvi na wahuni haujawahi acha mtu salama... Mhuni hana FUTURE wala PRESENT participle tense 😀😀😀, popote Kambi and they got nothing to loose.. Kwahiyo unapotafuta tifu nao agana na familia kabisa..
 
Kweli mkuu Wuondruok, wahuni si watu wakushindana nao,wengi bhang na unga umewaharibu.

Wamekata tamaa ya maisha kabisa,
wako tayari kwa lolote...
 
Wanabodi,
Siku za nyuma niliweka thread kuhusu mauaji ya kijana Jumanne Jongo kuuawa na sungusungu maeneo ya Beach Boy Mburahati.Kijana huyu anaishi maeneo ya Banda Mabibo.
Kijana aliyeuawa anaitwa Abdu ana umri wa miaka 19.
Kilichotokea ni kwamba kijana aliyeuawa alikwenda kwenye mziki maeneo ya Banda.Huyu kijana anakaa maeneo ya Bongo Beach alipouawa Jumanne Jongo.

Baada ya kufika katika mziki huo kwenye sherehe ya ushindi wa bondia wa Banda, mabaunsa walimuona huyo kijana wakaanza kumshambulia kwa kumpiga visu maeneo mbalimbali ya mwili,kooni,tumboni na kichwani.

Kijana alifia hospitali ya Mwananyamala baada ya kuvuja damu nyingi.

Sungusungu walichukua sheria mkononi kwa kuua kijana Jongo
wahuni wa Banda nao wamelipiza kisasi kwa kumuua huyu kijana anayehisiwa yeye au baba yake walihusika katika mauaji ya Jongo kwa kivuli cha
sungusungu.

Hii inatokana na uhasama mkubwa uliopo kwa wakazi wa maeneo haya dhidi ya sungusungu.

Hatujui atafata nani, ila hao sungusungu wa Jitegemee na Mburahati waache kiherehere kwani wako hatarini kushambuliwa na hawa wahuni wa Banda na kuuawa.

Kuna haja kuwe na upatanisho kati ya sungusungu na vijana wa Banda, bila hivyo maafaa yatatokea zaidi.

serikali ipo wapi ? enzi za makufuli upumbavu huu haukuwepo ila waambie jummanne muriro yupo na hao watu wa banda wataenda banda la mchanga
 
ume furahi sasa mwali maana kile kifo cha yule kibaka uli toa chozi bahati mbaya halikufika kwa hangaya
 
Kwani maeneo hayo hakuna ofisi ya mwenyekiti wa serikali za mitaa, hakuna kituo cha polisi au hata mjumbe? Ikiwa hao wote niliowataja hapo juu wapo je wana kazi gani? Yani mauaji yanatokea kiholela na wauaji wanajulikana, lkn hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya wauaji kana kwamba wanao uwawa ni nguruwe!
 
Back
Top Bottom