VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Hakuna kukosea.Hakuna kubahatisha. Kila kitu ni mipango. Mipango asubuhi,jioni mahesabu. Ndivyo alivyofanya Mwenyekiti wetu, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete. Ameteuwa 'Wa-jembe' wa Katiba. Amehakikisha kuwa maandalizi ni ya kuvutia kupitisha kila hoja na msimammo wa chama chetu cha Mapinduzi. Mwenyekiti ametisha. Rais halazimishwi kufuata tafsiri za watu Sheria inayosimamia Bunge la Katiba.
Makada machachari na 'waliokunywa maji ya bendera' wakiongozwa na Mzee Kingunge Ngombare Mwiru ni wa muhimu katika Bunge hilo hasa kwa upande wetu. Ni mfano wa Wa-jembe wa Katiba.Yuko pale kwa ajili ya kutengeneza njia ya kupitisha hoja za kichama. Yeye si 'Mjumbe'. Ni M-jembe (kwa kutengeneza njia).
Ndiyo maana kuna usanii ilibidi utumike. Wateuliwe kimtindo.Kutoka katika kundi 'tata' la watu wenye malengo yanayofanana. Kwakuwa hakuna tafsiri rasmi juu ya kundi hilo,na wala haikuhitajika, Mwenyekiti ameteua Wa-jembe wote 'kihalali' kabisa. Wapo wasio na hata NGO wala Shirikisho lolote.Lakini,wana malengo yanayofanana: kupitisha maoni na msimamo wa chama bila kikwazo. Wa-jembe!
Kazi yao itonekana Bunge la Katiba likianza. Mtajionea.Mtafurahia.Sasa roho zetu zimetulia. Tuna uhakika.Uhakika wa ushindi wa kimbunga. Mnaotaka uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba mtatusamehe. Chama kwanza, nyinyi baadaye!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Makada machachari na 'waliokunywa maji ya bendera' wakiongozwa na Mzee Kingunge Ngombare Mwiru ni wa muhimu katika Bunge hilo hasa kwa upande wetu. Ni mfano wa Wa-jembe wa Katiba.Yuko pale kwa ajili ya kutengeneza njia ya kupitisha hoja za kichama. Yeye si 'Mjumbe'. Ni M-jembe (kwa kutengeneza njia).
Ndiyo maana kuna usanii ilibidi utumike. Wateuliwe kimtindo.Kutoka katika kundi 'tata' la watu wenye malengo yanayofanana. Kwakuwa hakuna tafsiri rasmi juu ya kundi hilo,na wala haikuhitajika, Mwenyekiti ameteua Wa-jembe wote 'kihalali' kabisa. Wapo wasio na hata NGO wala Shirikisho lolote.Lakini,wana malengo yanayofanana: kupitisha maoni na msimamo wa chama bila kikwazo. Wa-jembe!
Kazi yao itonekana Bunge la Katiba likianza. Mtajionea.Mtafurahia.Sasa roho zetu zimetulia. Tuna uhakika.Uhakika wa ushindi wa kimbunga. Mnaotaka uteuzi wa Wajumbe wa Bunge la Katiba mtatusamehe. Chama kwanza, nyinyi baadaye!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam