Wallace Karia ndiye kiongozi wa muda wote wa mpira nchini mwenye mafanikio bora zaidi

Wallace Karia ndiye kiongozi wa muda wote wa mpira nchini mwenye mafanikio bora zaidi

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Embu tuwe wakweli kidogo, jumuisha Marais wote wa Nchi, Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu wa Wizara, Marais na Wenyeviti wa TFF na FAT, hakuna hata mmoja ukichukua mafanikio ya mpira nchini katika kipindi chake ambaye anamfikia Wallace Karia.

Sikubaliani na kila anachofanya au kilichofanyika katika kipindi chake cha uongozi ila kuna mengi mazuri ya kujivunia ambayo yamefanyika.

Leo hii timu zetu za taifa zinaenda sehemu mbalimbali duniani bila wasiwasi na zinarudi na makombe. Kwa watoto wa 2000 wasiojua, kuna kipindi timu zetu zilikuwa zinashindwa kusafiri inabidi kamati ziundwe zichangie pesa.

Vilabu hasa vya Simba na Yanga vimekuwa tishio katika mashindano ya CAF hadi tumeanza kuyachukulia poa mafanikio yao.

Mpira wa wanawake umekua sana na naamini nguvu ikiongezeka kule wanawake wengi sana watafaidika kupitia mpira, na hapa naongelea chain nzima kuanzia kwenye uongozi, ufundi, uchezaji na maeneo mengine.

Ubora wa viwanja vinavyotumika katika ligi kuu nao hakuna anayeweza kubisha katika hilo.

Hapo sijaongelea Maafisa Ubashiri waliotapakaa nchi nzima wanaotimiza ndoto zao za kuwa mabilionea, mkeka mmoja at a time.

Big up sana kwake.
 
Hongera sana kwa Bwana Karia. Amesimama Imara sana pamoja na figisu zetu za Ubaguzi nk.

Sisi watu weusi ni ngumu sana kumsifia Binadamu angali hai. Kwa HESHIMA KUBWA MIMI PIA NAMPONGEZA BW. KARIA KWA JITIHADA, USIMAMIZI THABITI NA MIPANGO YENYE MANUFAA KWA SOKA LETU.
Lkn tu viongozi wangu wa TFF punguzeni Umimi mnaharibu dhana ya Uongozi.

JAMAL Malinzi alipeleka Mradi wa FIFA kwao BUKOBA akaweka nyasi Kaitaba.

WALLACE Karia amepeleka Mradi wa FIFA kwao Tanga amejenga kituo cha Michezo huko. Tabia hizi zimeanza kuota mizizi hadi kwa Viongozi wa Nchi. Tulianza kuiona Msoga, Tukaja Chato na sasa ni zamu ya Kizimkazi.
Haipendezi, haifurahishi bali inakutieni doa katika uongozi wenu, achaneni na hizi mambo zinaharibu mazuri yenu.
 
Kuna ule upande wa wengi wasio na akili kasoro wawili hawakumwelewa karia. Walikuwa kutwa kucha kukalamika jamaa anaipendelea simba wakati timu yao ilikuwa mbovu. Mpaka serikali ilipoiingilia kati kuwapatia mfadhili wa kuijenga timu Sasa hivi wanaona aibu hata kulitaja jina la karia.
 
Embu tuwe wakweli kidogo, jumuisha Marais wote wa Nchi, Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu wa Wizara, Marais na Wenyeviti wa TFF na FAT, hakuna hata mmoja ukichukua mafanikio ya mpira nchini katika kipindi chake ambaye anamfikia Wallace Karia.

Sikubaliani na kila anachofanya au kilichofanyika katika kipindi chake cha uongozi ila kuna mengi mazuri ya kujivunia ambayo yamefanyika.

Leo hii timu zetu za taifa zinaenda sehemu mbalimbali duniani bila wasiwasi na zinarudi na makombe. Kwa watoto wa 2000 wasiojua, kuna kipindi timu zetu zilikuwa zinashindwa kusafiri inabidi kamati ziundwe zichangie pesa.

Vilabu hasa vya Simba na Yanga vimekuwa tishio katika mashindano ya CAF hadi tumeanza kuyachukulia poa mafanikio yao.

Mpira wa wanawake umekua sana na naamini nguvu ikiongezeka kule wanawake wengi sana watafaidika kupitia mpira, na hapa naongelea chain nzima kuanzia kwenye uongozi, ufundi, uchezaji na maeneo mengine.

Ubora wa viwanja vinavyotumika katika ligi kuu nao hakuna anayeweza kubisha katika hilo.

Hapo sijaongelea Maafisa Ubashiri waliotapakaa nchi nzima wanaotimiza ndoto zao za kuwa mabilionea, mkeka mmoja at a time.

Big up sana kwake.
Karia anakuja kwa TFF ambayo tayari imewekewa misingi ya uongozi wa kitaasisi kutoka kwa akina Tenga. Pia kwa sasa tuna wawekezaji wa kueleweka katika vilabu vyetu vikubwa jambo linalofanya club zetu kuweza kusajili wachezaji wazuri hata kutoka nje ya nchi. Kingine soka la Afrika halina tena wale vigogo, yoyote akikomaa anaweza kupata matokeo.
 
Karia anakuja kwa TFF ambayo tayari imewekewa misingi ya uongozi wa kitaasisi kutoka kwa akina Tenga. Pia kwa sasa tuna wawekezaji wa kueleweka katika vilabu vyetu vikubwa jambo linalofanya club zetu kuweza kusajili wachezaji wazuri hata kutoka nje ya nchi. Kingine soka la Afrika halina tena wale vigogo, yoyote akikomaa anaweza kupata matokeo.
Tungeitaja kwanza hiyo misingi waliyoiweka hao watangulizi wake ambayo imemuwezesha karia kufanya haya anayoyafanya ingekuwa vizuri zaidi.

Maana nikirejea kwa malinzi zaidi ya ufisadi alioufanya akiwa TFF hadi takukuru kuingilia Kati hakuna cha Maana alichokifanya.
 
Tungeitaja kwanza hiyo misingi waliyoiweka hao watangulizi wake ambayo imemuwezesha karia kufanya haya anayoyafanya ingekuwa vizuri zaidi.

Maana nikirejea kwa malinzi zaidi ya ufisadi alioufanya akiwa TFF hadi takukuru kuingilia Kati hakuna cha Maana alichokifanya.
Kama unaikumbuka FAT ya akina Ndolanga basi huhitaji kuuliza mageuzi yaliyoletwa na Tenga.
 
Tungeitaja kwanza hiyo misingi waliyoiweka hao watangulizi wake ambayo imemuwezesha karia kufanya haya anayoyafanya ingekuwa vizuri zaidi.

Maana nikirejea kwa malinzi zaidi ya ufisadi alioufanya akiwa TFF hadi takukuru kuingilia Kati hakuna cha Maana alichokifanya.
Kwa upande wangu, Leodgar Chilla Tenga ndiyo rais bora wa wakati wote wa TFF mpaka sasa.
Kwanza ni kiongozi ambaye enzi za uongozi wake; hakuendekeza makundi, ubaguzi, majungu, ubadhirifu, upigaji, na siasa za uccm kama huyo Karia na mwenzake Malinzi!
 
Kwa upande wangu, Leodgar Chilla Tenga ndiyo rais bora wa wakati wote wa TFF mpaka sasa.
Kwanza ni kiongozi ambaye enzi za uongozi wake; hakuendekeza makundi, ubaguzi, majungu, ubadhirifu, upigaji, na siasa za uccm kama huyo Karia na mwenzake Malinzi!
Mengine unaweza kuwa upo sahihi, ila Kwenda against ccm = serikali sio kweli hasingeweza kudumu vipindi vyote viwili na kuendelea kuheshimika mpaka Sasa
 
Mengine unaweza kuwa upo sahihi, ila Kwenda against ccm = serikali sio kweli hasingeweza kudumu vipindi vyote viwili na kuendelea kuheshimika mpaka Sasa
Mimi sijasema alikuwa against ccm! Maana sina shaka kwamba yeye ni kada mtiifu wa hicho chama.

Ninachokisema, enzi za uongozi wake alijitahidi sana kuifanya TFF kuwa chombo huru cha mpira wa miguu nchini, ukimlinganisha na hao watu wawili niliowataja.
 
Kuna tofauti kati ya kupata mafanikio na kuleta mafanikio (kusababisha mafanikio) Karia ni kiongozi anayeongoza kwa kupata mafanikio lakini sio kiongozi aliyesababisha mafanikio.
Mafanikio ya mpira wa miguu kwa Tanzania,
Credit ya kwanza inaenda kwa Azam media.ow Ukweli uliowazi, Azam media ujio wao umeleta mapinduzi makubwa kwenye soka la Tanzania, thamani na ushindani ukaongezeka na kuoneshwa kwa ligi ikaifanya ligi yetu kupendwa na kufatiliwa Tanzania nzima.
Credit ya pili ni matajili mbalimbali wakaona ni fursa kuwekeza na kudhamini timu mbali mbali kama Simba, Yanga n.k.
Uwekezaji huu ndio unaoleta tija kwa vilabu, na kufanya tupate wachezaji wazuri wanaochezea ligi yetu
 
Karia anakuja kwa TFF ambayo tayari imewekewa misingi ya uongozi wa kitaasisi kutoka kwa akina Tenga. Pia kwa sasa tuna wawekezaji wa kueleweka katika vilabu vyetu vikubwa jambo linalofanya club zetu kuweza kusajili wachezaji wazuri hata kutoka nje ya nchi. Kingine soka la Afrika halina tena wale vigogo, yoyote akikomaa anaweza kupata matokeo.
Siyo kweli Karia kaleta mabadiliko makubwa,kabla yake hata suala la udhamini wa ligi ulikuwa unasuasua halafu mdhamini akipatikana anaweka hela kiduchu,leo haki ya matangazo tu TFF na Vilabu vinaingiza hela,Simba juzi wanataka kumzingua Mo na kuwa na kiburi maana wawekezaji wapo,hivo hivo hata Yanga sasa hivi GSM akizingua haichukui mda kumpata mwingine,kina Tenga na Malinzi walifanya nini na la maana hata kwenye viwanja?Karia kaongeza idadi ya wachezaji wa kigeni kimataifa imekuwa pambio kila mwaka,leo hata wachezaji wa ndani wana mishahara mizuri huko yanga na Simba ndo wana hadi madinga na majumba,leo soka imegeuka kama ajira.
 
Back
Top Bottom