Walokole nchini Uganda ' wamchefua ' Rais Museveni na Yeye bila kuwachelewesha kawatolea ' uvivu ' kwa makavu!

Walokole nchini Uganda ' wamchefua ' Rais Museveni na Yeye bila kuwachelewesha kawatolea ' uvivu ' kwa makavu!

ukweli in kwamba hon. Museven ajatoa hayo maneno ila kuna clip moja ya mchekeshaji wa Uganda anajiita teacher mpamile ndio aliyemuigiza mseveni
 
Walokole wanakera sana asee, for sure as if sir God hasikii.
 
Kwani nyinyi mkiwa bar au disco hamuwezi kumwambia dj apunguze sauti ya mziki ili msikilizane badala ya kufungulia kwa sauti? Mnadhani ni wote wanao furahishwa na hali hiyo? Na wenyewe hao walokole ndio starehe yao hiyo
 
Muulize Museven kati ya anayo yafanya kwa wana Uganda na wanavyo fanya hao walokole anadhani kipi ambacho Mungu ana furahia?
 
Ki ukweli makelele yanakera sana
Haya ni mambo ya rohoni sana! Kwako ni kelele lakini kwa Mungu ni manukato according to the Bible maombi ya watakatifu wake ni manukato mazuri
 
Baada ya Rais Museveni kuwepo katika Mkutano wake wa hadhara wa Kisiasa nchini Kwake alikumbana na adha ya makelele ya ' Kimaombi ' kutoka kwa Walokole waliokuwa wakisali karibu na Uwanja ambao na Yeye alikuwepo hivyo kusababisha kutokusikilizana ndipo akaamua kuwapa ' makavu ' yao ' mubashara ' kabisa.

Rais Museveni baada ya kuonekana amekasirishwa na makelele ya Walokole ndipo akasema hii Kauli ambayo nainukuu hapa..." Hivi hawa Walokole hivi wanavyokuwa wanapenda Kuomba kwa Kupiga Makelele waliambiwa kwamba Mwenyezi Mungu wetu ni Kiziwi kiasi kwamba hata wakiwa wanaomba au wanamwomba tu Kimoyomoyo hawezi kuwasikia na hata Kuwabariki? Mbona madhehebu mengine Waumini wao huwa wanaomba kwa nidhamu, taratibu bila fujo na makelele na bado wanabarikiwa? Kuna Mlokole mmoja labda aliwahi kwenda Mbinguni akakutana na Mungu na akagundua kuwa ni Kiziwi hivyo alivyorudi akawaambia Walokole wote kuwa wawe sasa Wanasali kwa Makelele hadi Kuwasumbua na Kuwaudhi Watu wengine? Wabadilike tafadhali! "

Shikamoo Rais Yoweri Kaguta Museveni.

Walokole nchini Tanzania mpo?

Nawasilisha.
Kwa tunaoishi mitaa ya huku Ghana, Ohio, hapa DSM mnajua jinsi wahindi wana vyotutesa na kipindi chao hiki cha diwali, yaani wanapiga mikelele usiku kucha hatulali, kibaya nashangaa ikulu ipo karibu naamini na wao lazima wanasikia hizi kelele ila wanawaachia. Swali je kuna mswahili unaweza kwenda kuishi india ukawa na uhuru wa kuabudu???
 
Halafu kuna wengine watakwambia huwezi kumuelewa, inahitaji akili kubwa kumwelewa mtu fulani.
 
Ndugu yangu GENTAMYCINE naona unazidi kujifedhehesha na post zako zilizokuwa za 'kutukuka' hapo awali siku hizi zimegeuka na kuwa za 'mipasho' embu angalia utazidi kupoteza 'credibility hapa jukwaani
 
Huyu huyu Museveni waliyekosea kuandika umri wake wakati wa kipaimara?
 
Kwani ina maana wao hawaiheshimu mamlaka iliyowekwa ya pale Uganda.
 
Kuomba wa sauti sio kwamba Mungu ni Kiziwi ila wao wanawalenga binadamu wanaopita wavutiwe nao waokoke
 
Back
Top Bottom