Walokole wanautia aibu Ukristo

Walokole wanautia aibu Ukristo

Ukristò ni dini ya watu wasomi, wagunduzi, wana sayansi, matabibu, wana anga za juu nk.

Sasa siku za karibuni limeibuka kundi la watu wasiofikiria, wasio hoji, wenye ufinyu wa fikra, wenye kupelekeshwa kibwege kabisa na wahuni wanaojiita mitume na manabii.

Nabii akisema leo kamnyime mumeo unyumba, basi nyumbani siku hiyo mtalala mzungu wa nne.

Nabii akisema kalete mbegu, basi humo ndani hakukaliki lazima mbegu nono ipelekwe kwa nabii.

Walokole wanakonda manabii wananenepa. Kila siku ufukara unawaingia kwa kasi. Wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.

Walokole mnatakiwa mbatizwe kwa ubatizo wa moto wa gesi huenda ndipo akili zenu zitafunguka na kuijua kweli ambayo ni neno la Mungu.
Shida yako unashindwa kutofautisha upentekoste na cults au wahuni. Unalazimisha wahuni au Cults wawe wapentekoste.

Na shida unadhani ulokole umeanza kwa akina Mwamposa. Ulokole au Upentekoste kwa Lugha rasmi umeingia Tanzania mwaka 1928. Na makanisa yalikuwa matanoa tu.

Kanisa la Pentecostal Holliness Association la Paul Derr ambalo baadae liliizaa TAG, pia kanisa la UMPT baadae FPCT la akina Mzee Harris Kapiga, Elim Pentecostal na Kanisa la PAG. Hayo makanisa yalianzisha upentekoste Tanzania kuanzia 1920.

Na ndio makanisa yenye misingi imara ya upentekoste mpaka leo , so achana na wasanii kipimo kiwe makanisa waanzilishi.
 
Ulokole ni cult sio dini na imetokana na unrealistic belifs za dini ya Ukristo.
Unaelewa maana ya Cult?. Cult inakuwa na kiongozi mmoja na anasikilizwa yeye pekee yake. Tatizo mnalazimisha Cult za kina Mackenzie ziwe ndio upentekoste.
 
mleta mada walikufanyia nini walokole? sio kwa mishale hiyo. lazima tunguli zako zilifunguliwa.
 
Allah katika qur an anasema....nanukuu

"إِنَّ الدِّينَ عِندَ اللَّهِ الْإِسْلَامُ ۗ وَمَا اخْتَلَفَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْعِلْمُ بَغْيًا بَيْنَهُمْ ۗ وَمَن يَكْفُرْ بِآيَاتِ اللَّهِ فَإِنَّ اللَّهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ

[ AL I'MRAN - 19 ]
Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu(wakiristo na wayahudi) hawakukhitalifiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu...
Akili kichwani mwako
Na wale wakule India nao wanazungumziwajwe? (Wahindu, wabudha, nk)
 
Makanisa yote hayafuati maandiko bali yanafuata mawazo yawachungaji na wazee wa kanisa tu
Punguza uongo wewe. Makanisa yote uliyatemebelea lini wakati wewe muislamu?. Acha utapeli.
 
Wanamtumia Yesu huyo huyo wa Wakristu, shida iko wapi? Labda useme Ukristu kwa ujumla ni biashara. Wengine wanatumia tu falsafa kukupumbaza.
 
Umeandika fact sana mkuu. sisi wakristo inapaswa kujitafakari vzr kwa hili...
 
Back
Top Bottom