Wamachinga hawasaidii Tanzania!

Wamachinga hawasaidii Tanzania!

Tanzania mtu kasomea udaktari Kapewa masharti magumu kufungua zahati, alafu mganga wa kienyeji karuhusiwa kutoa huduma hata kwenye banda la nyasi. Kijana tulimsomesha wenyewe kapigwa vikwazo mapaka hapo acha wajazane kwenye umachinga.
Mtu kasomea sheria lakini hawezi kuwa mwanasheria mpaka aende shule ya sheria, kwa mini musiunganishe vyote kuwasaidia vijana? Alafu akiwa wakili wa kujitegemea halipwi na serikali lakini bado tumeweka vikwazo kibao, Dili ni umachinga na bodaboda tu hakuna jinsi.
Mwalimu haruhusiwi kufungua shule, mpaka awe na hekari kadhaa, majengo ya kisasa, vikwazo vya usajili mpaka basi. Waaache wajazane kwenye umachinga na bodaboda, tena tukiwasumbua tutegemee siku moja Yale ya Afrika ya kusini.
Jamani watu wana taaluma zao wako kwenye umachinga, angalieni sheria zinazozuia watu wasijitegemee. Mnazungumza habari za watu kujiajiri lakini mazingira ya watu kujiajiri yamefungwa na wanasiasa. Tatizo wanasiasa hawajuai maisha ya watu, wanaamua kwa kupapasa.
 
3. Vijana wengi ni wa vivu. Ni lini vijana wamekutana kama kikundi na kuomba mashamba ya ujasiliamali kwa serikali wakanyimwa. Lakini kitu kingine vijana sio waaminifu wanafikiria kuiba sana na hili linawarudisha nyuma kwenye kazi za kufanya pamoja.
'Theme' ni ile ile, "vijana ni wavivu"; halafu baadae inapanda - "WaTanzania ni wavivu",!

Ulishalisikia hili likisemwa na akina nani? Akina 'kamundu' kama hutaki kujibu swali.

Tatizo lako ni moja siku zote, na ni tatizo kwelikweli. Sijui uraia wa nchi yako hii uliupata vipi, lakini kuna kitu katika damu yako kinakataa kabisa kukuondoa kwenye jamii uliyoamua kuiacha nyuma na kuchukua uraia wa nchi nyingine.
Hii ina maana, huu uraia wa kupewa ni gheresha tu, ya kukupa nafasi ya kila mara kutanguliza maneno "Nchi yetu Tanzania", huku kwenye damu ukibaki kuwa raia halisi wa nchi yako ya asili.

Niseme, unajitahidi sana kuonyesha uTanzania wako, lakini katika mawazo unayowasilisha mara kwa mara yanakusuta jinsi usivyoridhishwa na mambo mengi ya nchi yako hii mpya, huku ukitamani yale yaliyoko kwenye nchi uliyoiacha ndiyo yawepo hapa. Sijui kama siku moja itakuwa hivyo, sijui. Itakuwa bahati sana kwako ikitokea iwe hivyo.
 
'Theme' ni ile ile, "vijana ni wavivu"; halafu baadae inapanda - "WaTanzania ni wavivu",!

Ulishalisikia hili likisemwa na akina nani? Akina 'kamundu' kama hutaki kujibu swali.

Tatizo lako ni moja siku zote, na ni tatizo kwelikweli. Sijui uraia wa nchi yako hii uliupata vipi, lakini kuna kitu katika damu yako kinakataa kabisa kukuondoa kwenye jamii uliyoamua kuiacha nyuma na kuchukua uraia wa nchi nyingine.
Hii ina maana, huu uraia wa kupewa ni gheresha tu, ya kukupa nafasi ya kila mara kutanguliza maneno "Nchi yetu Tanzania", huku kwenye damu ukibaki kuwa raia halisi wa nchi yako ya asili.

Niseme, unajitahidi sana kuonyesha uTanzania wako, lakini katika mawazo unayowasilisha mara kwa mara yanakusuta jinsi usivyoridhishwa na mambo mengi ya nchi yako hii mpya, huku ukitamani yale yaliyoko kwenye nchi uliyoiacha ndiyo yawepo hapa. Sijui kama siku moja itakuwa hivyo, sijui. Itakuwa bahati sana kwako ikitokea iwe hivyo.

Unapenda kutupotezea muda na kwenye nje ya hoja. Ongelea hoja nimekuja na list pale kama unakubaliana au una mawazo tofauti badala ya kujifanya unanijua sijui mimi ni Nurse … hunijui na wala sina shida ya kukujua twende na hoja za kusaidia wananchi badala ya kila topic yangu kujaribu kuibadilisha na kuniongelea mimi badala ya hoja!. Hunijui na mimi sikujui tuishie hapo.
 
Huenda hawasaidii Tanzania kama unavyosema lakini wanahudumia familia zao na kusaidia ndugu ambao ni watanzania.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app

..hudhani kwamba kundi hili lisiposaidiwa litakuja kutuletea matatizo huko mbeleni?

..naamini ni vibaya kuwashambulia , lakini ni vibaya zaidi kukaa kimya huku serikali haichukui hatua stahiki kupunguza ukubwa wa tatizo la wamachinga.
 
Unapenda kutupotezea muda na kwenye nje ya hoja. Ongelea hoja nimekuja na list pale kama unakubaliana au una mawazo tofauti badala ya kujifanya unanijua sijui mimi ni Nurse … hunijui na wala sina shida ya kukujua twende na hoja za kusaidia wananchi badala ya kila topic yangu kujaribu kuibadilisha na kuniongelea mimi badala ya hoja!. Hunijui na mimi sikujui tuishie hapo.
Hoja ni ipi hapo, au hujui maana ya hoja ni nini!

Hivi ngoja nikuulize, wale vibaka wa CBD Nairobi wanaonyang'anya watu mali zao mchana kweupe unadhani ni bora zaidi ya hawa waTanzania wanaojihangaikia kupata ridhiki yao kwa jasho lao kihalali? Ndiyo, shughuli inayofanywa na hawa vijana ni halali kabisa, wewe usiyekuwa na ufahamu wowote juu ya jambo hilo ndiye unayeimba upuuzi hapa.

Ni orodha ipi uloiyoweka pale ijadiliwe, mbona siioni?

-" Hawalipi kodi"? Unajuwa maana ya kodi ni nini wewe? Wao hawanunuwi vitu kwa mahitaji yao? Hili nalo hulijui?

-" wachafuzi wa mazingira"? Hao walioajiriwa kuweka usafi unataka wakaajiriwe wapi, au unataka mpaka tuwaite jina unalolijuwa wewe kutokana na huko ulikotokea -"Kazi Vijana Mitaani"; ndipo utambue kwamba kuna watu walioajiriwa kufanya kazi ya usafi?

-"wanauza vitu vya kijinga"? Angalia ulivyo mpuuzi. Unataka wauze vinavyotokea huko kwenu ndio utambue kwamba wanauza vitu vizuri? Na kwa maana hiyo, una maana waTanzania wanaonunua vitu vya "kijinga" na wao unawadhyarau? Una akili timamu wewe? Eti unasema tujadili orodha!

-"wanasaidia viwanda vya China" Unajitokeza hapa kutaka wasaidie viwanda vya Kenya?

Uchafu huu ndio unaotaka tuujadili?

Sitaki unijue, kwa sababu huna msaada wowote kwangu, na kusema kweli, huna msaada wowote kwa Tanzania. Upo tu ukijitangaza uraia wako wa makaratasi ukisubiri kwamba siku moja Tanzania itamezwa na Kenya. Hilo halitatokea hata siku moja.
.
Sijasema popote kwamba wewe ni "Nurse" na wala kazi unayofanya haina msaada wowote kwangu.
 
Sibiri watimuliwe waje wale kwako

Shida ni nyie wasomi wa kiafrika na elimu yenu ya kudesa
 
Watanzania wengi hawajui kwamba Wamachinga hawasaidii nchi yetu badala yake wanatumika kwa siasa pekee. Watanzania wanashangilia wamachinga ambao hawalipi kodi halafu wanalalamika wenyewe kuongezewa kodi!

1. Hawalipi kodi yeyote ya maana na vibali vya machinga ni kama kukejeli Watanzania.

2. Wachafuzi wa mazingira. Hivi hizi gharama za usafi analipa nani hasa kwa watu wasio lipa kodi.

3. Wanauza vitu vya kijinga ambavyo havina msaada wowote wa maana kwa viwanda vyetu wala sera muhimu kama kilimo, elimu au afya.

4. Wanasaidia viwanda vya china sio Tanzania hebu tukaangalie kama vitu vya machinga ni vya Tanzania! Utakuta ni majalala ya kichina hivyo tunasaidia wachina na sio Tanzania.

5. Wanaua wafanyabiashara wadogo ambao wanalipa kodi maana wameweka magenge ambayo hayana mpangilio mbele ya biashara nyingine
Sawa kabisaaa. Sasa nenda pale kariakoo ukawahutubie hao machinga hizo propaganda zako bilashaka watakuelewa zaidii
 
Wamachinga ndio sector inayokuwa kwa kasi hapa Tanzania serikali ingekuwa makini wangekusanya pesa nyingi sana mpk sasa wamekusanya biliion 43 kwa vitambulisho uchwala ni pesa ndogo sana kwanza hili neno wamachinga linamaana linatumiwa vibaya sana, machinga ni yule anaebeba bidhaa mkononi na kutembeza tu... lakini wengine wote ni wafanya biashara wakatiwe Leseni ya biashara walipe kodi hakuna machinga mwenye kibanda, mwenye sehemu ya kudumu ya biashara hawa ni wafanyabishara wahuni na wakwepa kodi .
 
Watanzania wengi hawajui kwamba Wamachinga hawasaidii nchi yetu badala yake wanatumika kwa siasa pekee. Watanzania wanashangilia wamachinga ambao hawalipi kodi halafu wanalalamika wenyewe kuongezewa kodi!

1. Hawalipi kodi yeyote ya maana na vibali vya machinga ni kama kukejeli Watanzania.

2. Wachafuzi wa mazingira. Hivi hizi gharama za usafi analipa nani hasa kwa watu wasio lipa kodi.

3. Wanauza vitu vya kijinga ambavyo havina msaada wowote wa maana kwa viwanda vyetu wala sera muhimu kama kilimo, elimu au afya.

4. Wanasaidia viwanda vya china sio Tanzania hebu tukaangalie kama vitu vya machinga ni vya Tanzania! Utakuta ni majalala ya kichina hivyo tunasaidia wachina na sio Tanzania.

5. Wanaua wafanyabiashara wadogo ambao wanalipa kodi maana wameweka magenge ambayo hayana mpangilio mbele ya biashara nyingine


Kama kawaida tunaona mbali hii tulisema mwezi wa saba
 
Huyo jamaa huwa ana mada zake za ajabu ajabu sana.

Sijui kama huwa anamkakati wowote na hizi mada au la, lakini kuna aina fulani ya mfanano ukizifuatilia vizuri.

Kuna wakati aliandika kulaumu vijana wa kiTanzania wasivyojituma na kuchangamkia fursa, akilinganisha na vijana wa nchi aliyozaliwa yeye. Leo analalamika kwa hawa vijana kujishughulisha na kilichopo wanachoweza kukifanya.

Sasa sijui kama ni kwa bahati mbaya, au ndivyo zilivyopangiliwa.
Kuna waliosema nina mada za ajabu ajabu tujiulize leo hii Raisi wa Tanzania kasema yote niliyosema!!
 
Kuna waliosema nina mada za ajabu ajabu tujiulize leo hii Raisi wa Tanzania kasema yote niliyosema!!
Kwanza eleza rais kasema nini, halafu tuone kama ndicho ulichosema wewe.

Nina hakika kabla hata sijakiona hicho unachodai rais amekisema kitakuwa ni tofauti na wewe ulichowahi kukisema wewe, tena kwa maksudi ya kuwadharau hao vijana wa kiTanzania ukilinganisha na hao wa huko kwenu.
 
Kwanza eleza rais kasema nini, halafu tuone kama ndicho ulichosema wewe.

Nina hakika kabla hata sijakiona hicho unachodai rais amekisema kitakuwa ni tofauti na wewe ulichowahi kukisema wewe, tena kwa maksudi ya kuwadharau hao vijana wa kiTanzania ukilinganisha na hao wa huko kwenu.



Kwetu ni Uninio mbele ya Tegeta! hapa USA ni mtafutaji tu!
 
Hoja ni ipi hapo, au hujui maana ya hoja ni nini!

Hivi ngoja nikuulize, wale vibaka wa CBD Nairobi wanaonyang'anya watu mali zao mchana kweupe unadhani ni bora zaidi ya hawa waTanzania wanaojihangaikia kupata ridhiki yao kwa jasho lao kihalali? Ndiyo, shughuli inayofanywa na hawa vijana ni halali kabisa, wewe usiyekuwa na ufahamu wowote juu ya jambo hilo ndiye unayeimba upuuzi hapa.

Ni orodha ipi uloiyoweka pale ijadiliwe, mbona siioni?

-" Hawalipi kodi"? Unajuwa maana ya kodi ni nini wewe? Wao hawanunuwi vitu kwa mahitaji yao? Hili nalo hulijui?

-" wachafuzi wa mazingira"? Hao walioajiriwa kuweka usafi unataka wakaajiriwe wapi, au unataka mpaka tuwaite jina unalolijuwa wewe kutokana na huko ulikotokea -"Kazi Vijana Mitaani"; ndipo utambue kwamba kuna watu walioajiriwa kufanya kazi ya usafi?

-"wanauza vitu vya kijinga"? Angalia ulivyo mpuuzi. Unataka wauze vinavyotokea huko kwenu ndio utambue kwamba wanauza vitu vizuri? Na kwa maana hiyo, una maana waTanzania wanaonunua vitu vya "kijinga" na wao unawadhyarau? Una akili timamu wewe? Eti unasema tujadili orodha!

-"wanasaidia viwanda vya China" Unajitokeza hapa kutaka wasaidie viwanda vya Kenya?

Uchafu huu ndio unaotaka tuujadili?

Sitaki unijue, kwa sababu huna msaada wowote kwangu, na kusema kweli, huna msaada wowote kwa Tanzania. Upo tu ukijitangaza uraia wako wa makaratasi ukisubiri kwamba siku moja Tanzania itamezwa na Kenya. Hilo halitatokea hata siku moja.
.
Sijasema popote kwamba wewe ni "Nurse" na wala kazi unayofanya haina msaada wowote kwangu.


Namshukuru Raisi kuwa mkweli na mwenye maono na kukubaliana na mimi "" Hawalipi kodi"
 
Mleta mada utakuwa mfanyakazi wa serikali siku ukifungua Duka la jumla ukitumbuliwa nk ndio utajua machinga ni nani kuwa wanachukua bidhaa toka eneo lako choka Mbaya lisilo na wateja kupeleka eneo la wateja ili wewe ujidai kulipa pango na kodi na kujitia majidai kuwa uko prime business area ambalo hata TRA wanatolea mimacho kumbe hawajui wanaolimbatisha chati hilo eneo sio location walipo ni machinga wabeba bidhaa kuzunguka nazo masoko yaliko
 
Namshukuru Raisi kuwa mkweli na mwenye maono na kukubaliana na mimi "" Hawalipi kodi"
Kwa hiyo hilo la "kutolipa kodi" ndilo unalonitafutia nije hapa nikubali kwamba wewe na rais mnakubaliana?

Ni lini ulisikia nikitetea wasiolipa kodi, tena akheri ya hao wamachinga, kuna wengi wasiolipa kodi wanaotakiwa walipe kodi hasa!
 
Kwa hiyo hilo la "kutolipa kodi" ndilo unalonitafutia nije hapa nikubali kwamba wewe na rais mnakubaliana?

Ni lini ulisikia nikitetea wasiolipa kodi, tena akheri ya hao wamachinga, kuna wengi wasiolipa kodi wanaotakiwa walipe kodi hasa!


Mimi sikutafuti hii topic ni yangu!. Nimesema ukweli tu. Tusipoteze muda kubishara ukweli badala yake toa mawazo yako kama unapingana na mimi na Raisi Samia kwenye hili jambo ili tusaidie nchi yetu.
 
Huo ndio ukweli mchungu. Wamachinga wanaelemea taifa na kuchukua haki za walipa kodi wengine. Ni muda sasa kama Taifa kuwatafutia shughuli nyingine ya uzalishaji itakayo walipa na kuwaondoa barabarani.
Wazo zuri,kulitekeleza ndo kazi ngumu,hii ni nchi maskini sana yenye raia kama milioni60
 
Sawa waweza sema machinga hawalipi kodi lakini ndio wasababishaji wa stock turnover ya wafanya biashara wakubwa walipa VAT kwenda haraka na kuagiza mzigo mwingine VAT and custom duty taxable ndio wanakimbiza tax turnover kwa Kukimbiza haraka sales turnover
Mleta mada ukikariri notice hukuelewa masomo
 
Back
Top Bottom