Wamarekani wameichoka Demokrasia?

Wamarekani wameichoka Demokrasia?

Trump anaongelea majenerali ambao watakuwa loyal kwake, sio hayo mambo mengine ambayo hata hayajui.
View attachment 3136141
Trump alimfuta kazi John Bolton aliyekuwa mshauri wa masuala ya kiusalama sababu Bolton alikuwa warmonger.

Bolton ushauri wake ni tulipue Iran, unaona hawa kina nani wamefanya hivi, tuwalipue. Unaona hawa wamekataa demokrasia, tuwalipue. Trumpa akafukuzia mbali hilo jinamizi.
Sasa hao ambao hawakuwa kama Trump ndio akina Obama, kaambiwa apelekee demokrasia Libya akapeleka majeshi. Libya kuna demokrasia sasa?
Obama pia kapeleka majeshi Syria. Bush alishauriwa akaivamia Iraq kutafuta WMD, alizipata?

Trump kafanya mazungumzo na North Korea na Iran, kaondoa majeshi Afghanistan, na palipokuwa na ulazima wa nguvu kamshambulia mkuu wa IRGC General Soleimani.

Trump anaijua katiba ya Marekani, hawezi tegemea loyalty kwake badala ya kwa katiba.
 
Dikteta ni nani? Mbona hao Kina Biden wanamtambua Prince MBS wa Saudia kwani sio dikteta? Au mbona wanamhusudu Kagame kwani sio dikteta? Au dikteta ni pale tu anapokua adui wa USA?
Umewahi kusikia Biden akitoa kauli za kumuhusudu au kumu admire MBS au Kagame? Ukishakuwa kiongozi wa taifa lolote utatambulika tu wewe ndiye kiongozi wa hilo taifa bila kujali uliupataje huo uongozi na kama ni mwendawazimu au timamu.
 
Axis powers- Ujerumani, Italia na Japan.
Pia Ujerumani ilijipatia maeneo mengi kuelekea wakati wa vita kwa sababu ya appeasement policy.
Japan iliisaidia nini Ujerumani vitani.

Au Italy iisaidia nini Ujerumani, Italy hii ambayo ilisababisha Ujerumani waende kuikomboa. Yani badala wapigane kwingine, wanapigana wanaichunga isipigwe.

Appeasement haikuipa Ujerumani maeneo, iliyapata maeneo kwa kupigana au kuyashawishi nayo machache.
 
Trump alimfuta kazi John Bolton aliyekuwa mshauri wa masuala ya kiusalama sababu Bolton alikuwa warmonger.

Bolton ushauri wake ni tulipue Iran, unaona hawa kina nani wamefanya hivi, tuwalipue. Unaona hawa wamekataa demokrasia, tuwalipue. Trumpa akafukuzia mbali hilo jinamizi.
Sasa hao ambao hawakuwa kama Trump ndio akina Obama, kaambiwa apelekee demokrasia Libya akapeleka majeshi. Libya kuna demokrasia sasa?
Obama pia kapeleka majeshi Syria. Bush alishauriwa akaivamia Iraq kutafuta WMD, alizipata?

Trump kafanya mazungumzo na North Korea na Iran, kaondoa majeshi Afghanistan, na palipokuwa na ulazima wa nguvu kamshambulia mkuu wa IRGC General Soleimani.

Trump anaijua katiba ya Marekani, hawezi tegemea loyalty kwake badala ya kwa katiba.
Ugomvi wa Trump na Bolton ni kwa sababu Bolton alikuwa anamuona Trump ni kiazi asiyeelewa kitu chochote kuhusu foreign policy na diplomasia, kama vile alivyoamka tu akataka picha za kuuza sura na Kim Jong Kiduku huku hakuna hata mtu mmoja kwenye baraza lake la usalama wa Taifa anayeelewa huko kukutana kwao kutafanikisha nini.

Trump akuwahi kukumbana na Arab Spring kama Obama au mashambulizi ya September 11 kama Bush kwa hiyo hatujui ange react vipi kama angekutana na changamoto kubwa kama hizo, Changamoto mojawapo kubwa Trump aliyokutana nayo ni COVID-19 ambayo alifeli vibaya sana kui handle mpaka kupelekea kupoteza urais.

Pia Trump hakuondoa majeshi ya US Afghanistan aliyeondoa majeshi ni Biden tena baada ya kukuta makubaliano mabovu yaliyokuwisha kufanyika kati ya Trump na Taliban.
 
Adolf Hitler alikuwa mzalendo lakini propaganda ilirnezwa ili tumchukie.
Mzalendo kwa maana ya nationalist ni sahihi, unaweza kwa dikteta na nationalist, wako wengi wa aina hiyo kama Stalin, Khmer Rogue, Iddi Amin, n.k
 
Ugomvi wa Trump na Bolton ni kwa sababu Bolton alikuwa anamuona Trump ni kiazi asiyeelewa kitu chochote kuhusu foreign policy na diplomasia, kama vile alivyoamka tu akataka picha za kuuza sura na Kim Jong Kiduku huku hakuna hata mtu mmoja kwenye baraza lake la usalama wa Taifa anayeelewa huko kukutana kwao kutafanikisha nini.
Then Bolton warmonger akapigwa chini. Baada ya hapo hatukumuona Marekani akivamia ardhi ya yeyote. Tukaona Marekani anapunguza unnecessary military presence in foreign soils kama kuondoa majeshi Afghanistan. Tukamuona Marekani anaendeleza dialogues badala ya kutumia nguvu tu, ndio huko ziara na Kim Jong.

Hao kina Bolton na foreign policy zao wasingeweza shauri hivyo. Badala yake wao ni milipuko na umwagaji damu tu. Sasa unamuitaje Trump kiazi, kisa hajaua bila sababu?
Trump akuwahi kukumbana na Arab Spring kama Obama au mashambulizi ya September 11 kama Bush kwa hiyo hatujui ange react vipi kama angekutana na changamoto kubwa kama hizo,
Kwahiyo Obama kwa kutumia ushauri wa kina Hilary Clinton alikuwa na akili sana kuivamia Libya kisa Arab spring, ila Trump ni kiazi kukutana na wakuu wa nchi nyinginezo wazungumze?

Okay tuseme Obama hakujua namna ya kureact dhidi ya Arab spring akaishambulia Libya mwaka 2011 (na tusimuite kiazi).
Mpaka Obama anaondoka mwaka 2017 miaka 6 yote alifanya nini kuleta hiyo demokrasia walioisema Libya?
Kilaza nani hapo sasa.

Bado Obama kwenye kuishambulia Syria wamezalisha wakimbizi wa Kiarabu mamilioni, ambao wameharibu utamaduni wa nchi na miji ya kizungu. Kuna migrant crisis inaendelea Ulaya, Ulaya hii ambayo ni mshirika mzuri wa kibiashara wa Marekani hivyo Ulaya akifeli na Marekani anapata hasara.

Bush alidai kwamba Iraq kuna magaidi na silaha za maangamizi, na hakuzikuta hata debe moja. Kaipiga Iraq 2003 mpaka leo haijatengamaa iko prone na ISIS, kuna factions za Sunni na Shia. Marekani baada ya kukosa ilichodai lakini bado haikuleta amani iliyoikuta Iraq.
Bado unaona kilaza ni Trump?
Changamoto mojawapo kubwa Trump aliyokutana nayo ni COVID-19 ambayo alifeli vibaya sana kui handle mpaka kupelekea kupoteza urais.
Alifeli vipi dhidi ya COVID-19, haikuenea kwa uzembe wa Trump hata angekuwa Rais nani bado ingeenea. Hakuna Rais angeua virusi kimiujiza. Ila failure ya Marekani kuvamia Iraq kwa visingizo vya silaha za maangamizi ni ya wazi, failure ya kuivamia Libya eti kuleta demokrasia na badala yake kuiharibu ni ya wazi.

Trump angefeli yeye kama yeye kwenye COVID hawa Democrats wangeitumia kama agenda ya kampeni but no one buys this, Trump is leading kwenye maoni.
Pia Trump hakuondoa majeshi ya US Afghanistan aliyeondoa majeshi ni Biden tena baada ya kukuta makubaliano mabovu yaliyokuwisha kufanyika kati ya Trump na Taliban.
Majeshi hayaondolewi kama magunia ya mapera, hata uhuru haukuwa wakoloni wanafyatuka usingizini leo kesho wanaondoka. Majeshi yanaondolewa gradually na aliyesaini kuyaondoa ni Trump, Biden alimalizia utekelezaji na kuenda kwenye misingi ya Trump.

"... The Trump administration in February 2020 negotiated a withdrawal agreement with the Taliban that excluded the Afghan government, freed 5,000 imprisoned Taliban soldiers and set a date certain of May 1, 2021, for the final withdrawal."

Alafu Trump alitaka kuzuia wahamiaji haramu, ambapo Biden na Kamala wanaruhusu shamba la bibi. Pia Trump anataka kufufua manufacturing ya Marekani, hao Democrats wao wamegeuka wachuuzi wa bidhaa za Kichina.

Trump anamzidi mbali akili Biden na Kamala wake, Obama anamzidi mbali failures Trump. Bush huyo hadi anastahili kuwa prosecuted kama hao majenerali wa Nazi Germany.
 
Mtu yeyote anayejua masuala ya kijeshi na kivita atakwambia anahitaji majenerali kama aliokuwa nao Hitler.

In modern world, halijawahi kuwepo jeshi lenye maofisa wazuri kama Wehrmacht kuanzia Heer (Army), Luftwaffe (Airforce) na Kriegsmarine (Navy).

Hitler alikuwa na maofisa wazuri wa logistics, defensive warfare, offensive warfare, siege, mavazi, mobility, matumizi mazuri ya bajeti, nidhamu, technology na almost kila kitu. Hili hata Allies walilijua na hawakuficha.

Wanajeshi huwa hawadharau maadui zao kisa wamewashinda, labda wanajeshi uchwara. Upate wapi jeshi lenye maofisa walioshindikana kama:

Field Marshal Erwin Rommel (Desert Fox)
Field Marshal Erich von Manstein.
Field Marshal von Paulus
Field Marshal Wilhelm Keiter
Field Marshal Albert Kesselring
Field Marshal Walter Model huyu pekee ndie aliweza kumbishia Hitler na kufanya anavyoona inafaa, na aliisaidia sana Ujerumani dhidi ya Soviets.
General Einz Guderian ndio muasisi wa Britzkrieg.

Ujerumani ilishindwa vita sababu ya siasa ila sio sababu ya jeshi. Nchi gani ingeweza kupigana vita miaka mitano, ikiwa na uchumi sio mkubwa sana alafu ipigane na mataifa makubwa chungu nzima.

Bahati mbaya watu huwa tunasema mabaya ya Hitler tu. Sifa moja ya Hitler, hakuwa anafanya kazi na vilaza.
Maofisa wake wote walikuwa experienced, waliongoza kwenye military schools walifaulu kwa alama za juu, walikuwa na mipango ya maana na walistahili sana nafasi zao.
Mkuu wa jeshi la anga alikuwa rubani WW1 na alipiga ndege nyingi za adui, maafisa wake wengi hawakuwa wazee walikuwa kwenye 45 kwenda 50. Nilisoma nafasi nyingi alizokuwa anateua ni watu wanaojua sio average. Na alikuwa anapandisha cheo mtu anayefanya kazi vizuri.

Hitler hakuwa msomi ila aliwapenda wasomi wanaompa ideas ngumu ambazo hata hajui zinawezekanaje, anawapa nafasi watumikie taifa.
Mkuu, usipovuta ile kitu ya Arusha huwa na nondo mujarabu sana.
 
Yes I admire them too, mbona hao US walivamia Iraq, Afghanistan wanatofauti gani na Hitler au Putin kuvamia Ukraine? Trump sio mnafiki ndio maana mnamchukia ila wapenda haki wanamkubali
Ifike hatua tuanze kuzungumza ukweli kama huu. Safi sana.
 
Then Bolton warmonger akapigwa chini. Baada ya hapo hatukumuona Marekani akivamia ardhi ya yeyote. Tukaona Marekani anapunguza unnecessary military presence in foreign soils kama kuondoa majeshi Afghanistan. Tukamuona Marekani anaendeleza dialogues badala ya kutumia nguvu tu, ndio huko ziara na Kim Jong.

Hao kina Bolton na foreign policy zao wasingeweza shauri hivyo. Badala yake wao ni milipuko na umwagaji damu tu. Sasa unamuitaje Trump kiazi, kisa hajaua bila sababu?

Kwahiyo Obama kwa kutumia ushauri wa kina Hilary Clinton alikuwa na akili sana kuivamia Libya kisa Arab spring, ila Trump ni kiazi kukutana na wakuu wa nchi nyinginezo wazungumze?

Okay tuseme Obama hakujua namna ya kureact dhidi ya Arab spring akaishambulia Libya mwaka 2011 (na tusimuite kiazi).
Mpaka Obama anaondoka mwaka 2017 miaka 6 yote alifanya nini kuleta hiyo demokrasia walioisema Libya?
Kilaza nani hapo sasa.

Bado Obama kwenye kuishambulia Syria wamezalisha wakimbizi wa Kiarabu mamilioni, ambao wameharibu utamaduni wa nchi na miji ya kizungu. Kuna migrant crisis inaendelea Ulaya, Ulaya hii ambayo ni mshirika mzuri wa kibiashara wa Marekani hivyo Ulaya akifeli na Marekani anapata hasara.

Bush alidai kwamba Iraq kuna magaidi na silaha za maangamizi, na hakuzikuta hata debe moja. Kaipiga Iraq 2003 mpaka leo haijatengamaa iko prone na ISIS, kuna factions za Sunni na Shia. Marekani baada ya kukosa ilichodai lakini bado haikuleta amani iliyoikuta Iraq.
Bado unaona kilaza ni Trump?
Sasa Trump angevamia vipi nchi nyingine wakati hajawahi kupata changamoto kubwa zinazompa uvamizi kama chaguo mojawapo?! Kwani Obama aliamka tu akasema sasa tuivamie Libya au Syria??, Bush aliamka tu kutoka usingizini akasema sasa tuivamie Afghanistan na Iraq ?? Trump hajawahi kukutana na geopolitical events ngumu za kumfanya aumize kichwa. Obama alikuwa ofisini anashuhudia Gaddafi anaua raia wake waandamanaji kama mende na hao waandamanaji wanamuomba azuie hilo, Wakati Assad anawapulizia Sarin, Bush alikuwa ofisini magaidi wakilipua Marekani na kuua raia elfu tatu na wamarekani wanataka majibu ya show of strength kutoka kwake baada ya hayo matukio, Clinton alikuwa ofisini wakati Rwanda genocide inatokea, Somalia inaingia kwenye civil war na vita vya Bosnia vinazuka. Bush Snr alikuwa ofisini wakati Iran inaivamia Iraq. Yani ni sawa na kumlaumu mtu aliyeenda kumsaidia jirani yake aliyevamiwa na majambazi baada ya mke wa jirani kufa katika harakati za kupambana nao ukimlinganisha na mtu ambaye hajawahi kuhitajika kwenda kwa jirani yake kwa sababu hakujawahi kutokea tukio kama hilo, it doesn't make much sense.

Ziara ya Trump kukutana na Kim Jong haikuwa kuhusu dialogue, kila mtu mmarekani anayejua masuala ya foreign policy anafahamu hilo, karibia wote ukiacha chawa wachache wa Trump wanasema ile ilikuwa ni kwa ajili kuuza sura zaidi kama Rais wa kwanza wa Marekani kukutana na Kiduku, ndio maana hata wahusika wakuu katika huo mzozo ambao ni Korea Kusini na Japan waliachwa gizani na Trump.

Kipimo cha Trump kilikuwa COVID-19 ambayo alishindwa vibaya sana kui handle.
 
Kwahiyo Obama kwa kutumia ushauri wa kina Hilary Clinton alikuwa na akili sana kuivamia Libya kisa Arab spring, ila Trump ni kiazi kukutana na wakuu wa nchi nyinginezo wazungumze?

Okay tuseme Obama hakujua namna ya kureact dhidi ya Arab spring akaishambulia Libya mwaka 2011 (na tusimuite kiazi).
Mpaka Obama anaondoka mwaka 2017 miaka 6 yote alifanya nini kuleta hiyo demokrasia walioisema Libya?
Kilaza nani hapo sasa.
Kwanza Obama hakuwa na wajibu wa kuleta demokrasia Libya au Syria, lengo la operations katika nchi hizo ilikuwa kuzuia mauaji ya raia yaliyokuwa yakifanywa na Gaddafi na Assad kwa waandamanaji, hilo suala la kwamba walipeleka demokrasia ni kuongezea chumvi tu na propoganda.
 
Alafu Trump alitaka kuzuia wahamiaji haramu, ambapo Biden na Kamala wanaruhusu shamba la bibi. Pia Trump anataka kufufua manufacturing ya Marekani, hao Democrats wao wamegeuka wachuuzi wa bidhaa za Kichina.
Trump hajawahi kutaka kuzuia wahamiaji haramu, hakuna Rais wa Marekani anayeweza kuzuia wahamiaji haramu bila sheria za bunge la Marekani, kwa mara ya kwanza katika historia ya Marekani baada ya miongo mingi sana Biden ndiye ameweza kuwafanya maseneta wa Marekani wa Democrats na Republicans wakubaliane mswaada mzuri na mkali zaidi wa sera kuwahi kutokea wa sera ya uhamiaji (Bipartisan border deal) lakini Trump akawapigia chawa wake wa House of Representatives wasiupitishe kwa sababu utampa Biden credit na kumfanya yeye Trump kukosa agenda ya uchaguzi.

Hilo suala la Trump kutaka kufufua manufacturing ya Marekani ndio umepotoka zaidi. Trump amewahi kufanya nini katika utawala wake zaidi ya tariffs tu? Hajawahi kuwa na mpango au sera yoyote inayohusu kuimarisha manufacturing USA. Biden amekuja na CHIPS and Science Act, na Bipartisan Infrastructure bill.
 
Kwa mujibu wa demokrasia
Kila mtu na nchi ina tafsiri yake juu ya democracy sio razima waitafisri kama wamagharibi ,mfano mtu anaweza kusema Uingereza inatawaliwa kidkiteta kwa sababu imeongozwa na familia moja kwa karne za miaka.
 
Alifeli vipi dhidi ya COVID-19, haikuenea kwa uzembe wa Trump hata angekuwa Rais nani bado ingeenea. Hakuna Rais angeua virusi kimiujiza. Ila failure ya Marekani kuvamia Iraq kwa visingizo vya silaha za maangamizi ni ya wazi, failure ya kuivamia Libya eti kuleta demokrasia na badala yake kuiharibu ni ya wazi.

Trump angefeli yeye kama yeye kwenye COVID hawa Democrats wangeitumia kama agenda ya kampeni but no one buys this, Trump is leading kwenye maoni.
Kutokana na uzoefu wa Ebola Obama wakati anaondoka madarakani aliacha Pandemic Playbook/Pandemic Response plan na Pandemic unit katika baraza la usalama wa taifa(NSC), Trump alipoingia akafuta hiyo timu na kutupulia mbali plan nzima iliyokuwepo, miaka mitatu baadaye COVID-19 hii hapa akabaki anarukaruka tu hajui aanzie au aishie wapi, anasema hii ni flu tu ya muda mfupi itaisha, watu waote jua. Wataalamu wote wa Pandemic wanasema hatua za mwanzo kudhibiti ndio muhimu zaidi, ukikosea hapo huko mbele ni majanga matupu na ndicho kilichowakuta USA tofauti na China. Sababu mojawapo kubwa ya Trump kupoteza urais ni vifo na uharibifu wa uchumi na maisha kutokana na COVID-19.
 
Adolf Hitler alikuwa mzalendo lakini propaganda ilirnezwa ili tumchukie.Ona saivi wa Israeli wanavyoua hovyo watoto huko gaza.kwa maovu wanayoyafanya Hawa Israeli unaona kabisa Hitler alikuwa sahihi kuwasdhibu
Ni nini hasa kilisababisha Hitler kuwaua Wayahudi? Why yeye na sio Wayahudi wa nchi zingine za Ulaya but German and Poland, why not waliokua USA, Canada, Russia etc. Huaga natamani kujua sababu but sijawahi kufanikiwa kujua hi
 
Kila mtu na nchi ina tafsiri yake juu ya democracy sio razima waitafisri kama wamagharibi ,mfano mtu anaweza kusema Uingereza inatawaliwa kidkiteta kwa sababu imeongozwa na familia moja kwa karne za miaka.
Kwenye tafsiri za mambo kuna vitu tunaita "key" au "fundamentals". Unaweza kuitafsiri Tanzania upendavyo lakini kuna vitu key mfano "Jamuhuri" "muungano", "East Africa" n.k, ni hivyo pia kwa demokrasia, so stop this bullshit ya kusema kila taifa lina demokrasia yake na mataifa yote duniani ni ya kidemokrasia.
 
Back
Top Bottom