Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naona haelewi kuwa mipaka ilitengenezwa na watuTembea uone, Wahutu wana vuka mpaka na kuja kuishi Tanzania kama tu wamakonde wanaotoka nachingwea na kwenda kuishi mbagala.
Kwahiyo wale wamasai waliokuwa wanashukuru kuhamishiwa makazi Msomera kumbe walikuwa na jambo lao mioyoni? 🤣 🤣 🤣Katika jambo la kustaajabisha kabisa ni tukio la wamasai waliohamishwa kutoka Ngorongoro na kupelekwa kule Handeni, Tanga eneo la Msomera wameonekana pia Ngorongoro wakati huu wa sakata la wamasai kuungana kudai haki ya kuendelea kuishi Ngorongoro.
Tulielezwa kuwa wakati wa zoezi la kuhamia Tanga, wamasai walipewa bure usafiri wa kubeba familia na mali zao, wakajengewa nyumba za kisasa, kuletewa huduma muhimu na kupewa posho nzuri ya kuanzia maisha huku wakishukuru kwa wema na fadhili za serikali ya mama.
Kwa kifupi serikali ilitumia nguvu-kazi kubwa, muda, pesa na kila namna ili kujenga mazingira ya wamasai kwenda kuishi Tanga, na wamasai wajanja wakatumia fursa hiyo kuvuna kirahisi huku akili na mioyo yao ikiendelea kubakia Ngorongoro.
Kwa sasa wamasai wale wana makazi sehemu mbili, kule Msomera na Ngorongoro. Huku ndiko kula keki ya taifa. Na kwa jinsi wamasai walivyo huenda wakatapakaa Handeni yote na kuwafurumusha wenyeji taratibu ili kuhodhi eneo lote kwa ajili ya kuishi na kufuga.
Safari hii mmasai kamuingiza mjini mswahili. Kumbe mjini kuna wajinga wengi ambao wanaweza kutapeliwa na washamba wa porini.
Soma Pia:
Pole sana mama, hawa watanganyika waache kama walivyo hivyo hivyo, wapambane na hali yao, wanakuchosha bure, hawana shukrani kabisa!
Kama walichojengewa ni kibanda ni afadhali kuliko ngorongoro wanaishi kwenye vichuguuHivyo vibanda walivyojengewa ndiyo unaita nyumba za kisasa?Kwanza umeandika uongo mtupu.