Wamechelewa kuanza Mazoezi ya Pre Season ila leo wamekipiga kwa Mkaburu, na tuliowatangulia Kutwa tunacheza Mechi Mazoezi tu huko wa Farao

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Najua tunataka Kumlinda Kocha Mgeni asianze na Nuksi, ila tunaomba nasi hata Mechi moja tu ya Kirafiki hata kama tutapigwa 9 kwa 0 poa ili mradi nasi tukione Kikosi chetu na tujue je, yaliyomo yamo au ni yale yale ya kuendelea Kuteseka. Sasa katika Mechi Mazoezi hapo Kocha anagundua nini? Hebu tuthubutuni kama Wenzetu leo.
 
Kweli kabisa chief
 
Daah mzee Leo umeongea fair Sana Yanga kweli imejitahidi kiasi chake leo
 
Heri inyeshe mjue panapo vuja!
 
Magoma alianzaga vivi hivi .
 
Mnawasifu bure hao watoto wa Mzee Magoma. Walizusha Simba kala 6 kwa sababu walikuwa matumbo joto na mechi hizi walizoenda kucheza SA, walitaka kutengeneza mazingira wakichapwa waseme na nyie mmefungwa 6 kwa mechi waliyoitunga. Wamezoea kujitekenya na kucheka wenyewe.

Usiku wa leo watalala unono baada ya kuchapwa 2 tu, wanaweza hata kujikojolea vitandani hawa vyura.
 
Ulitaka tufungwe 5 kama nyie?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…