Tsh
JF-Expert Member
- Aug 26, 2021
- 17,022
- 36,936
Kuna dada mmoja ana uzuri wake akiwa mjini na gari yake utadhani labda ana mwanaume anamtunza, ila huyu dada ukimkuta mwanza ziwani akigombana na wavuvi hutaamini, ananuka shombo hafai. Inasemekana ana tenda za samaki za mahoteli makubwa na ana wavuvi wake ziwani hivyo akiwa na tenda anasimamia mchakato wote kuanzia kuparua mpaka kuwapaki ila akiwa mjini hajulikanagi anafanya nini. Huyu ni mfano hai kabisa na ukimuona akiwa dar anaamka na kuendesha gari yake utakachohitimisha ni kuwa anadanga tu ila uhalisia ni dada ni jembe haswa kwenye kupiga kazi na kuchungulia fursa.
Tukiachana na madawa na ufreemason sijui kuuza mwili, pengine huyo mtu anachukua mabelo mjini hapo yanasafirishwa mikoani huko kwa jumla na ana wateja wake singida, iringa, njombe, makambako ambao akipakia mizigo inalipa frem ambayo ni ofisi tu pa kukutania na watu.
Tusikatishwe tamaa na mawazo negative, tuwe positive.
Tukiachana na madawa na ufreemason sijui kuuza mwili, pengine huyo mtu anachukua mabelo mjini hapo yanasafirishwa mikoani huko kwa jumla na ana wateja wake singida, iringa, njombe, makambako ambao akipakia mizigo inalipa frem ambayo ni ofisi tu pa kukutania na watu.
Tusikatishwe tamaa na mawazo negative, tuwe positive.